

Ndani ya Manispaa ya Iringa kuna msitu ulio kwenye milima ya Gangilonga. Msitu huu una miti na uoto asilia. Matunda mengi asilia yanapatikana humu. Huvutia ndege na wanyama wadogo wadogo kama vile digidigi na ngedere. Uwepo wake ndani ya Manispaa, msitu huu uko hatarini kuangamizwa na mwanadamu kutokana na mahitaji ya nishati yanayopelekea watu kutamani kukata miti. Juhudi za makusudi zinatakiwa kufanyika kuhifadhi msitu huu.




Tanzanian Shilling Converter
1 comments:
Madhali ni nzuri inapendeza. Inaitaji kuangaliwa pasipo hualibifu wa mazingira, haya ni mazingira ya asili yanapendeza kama yalivyo
Post a Comment