Huo ni mchele au Mpunga, Wasukuma hawajui kutofautisha mchele na mpunga wao au shamba au umekobolewa wanaita mamichele na wale Jamaa ambao wamebahatika kuwa na mchele unanukia vizuri wale Malafyale nao kwao ni Mpunga tu.Naomba mnisaidie mchele ni upi na mpunga ni upi?
Malafyale, mchele ni ule uliokwishakobolewa, na mpunga ni ule uliokuwa bado haujakobolewa. Na kuhusu kuchagua au kuchambua, pwani mpunga unachaguliwa sio kuchambuliwa! Ndio maana tunapoalikana shughuli zetu ambazo zinahitaji maandalizi ya chakula, huambizana "kesho kuna kazi ya kuchagua mchele!"
Kaka Maggid umenikumbusha ile methali ya "Amekula wali wa chuya kwa uvivu wa kuchagua". Baada ya mchele kukobolewa masalio ya mpunga katika mchele huitwa "chuya" Wa Tanga.
6 comments:
MPUNGA WA KWETU UNA RANGI YA KAHAWIA KWA SABABU YA MAGANDA YAKE NA MCHELE HUWA MWEUPEE, MPUNGA HUU UKIKOBOLEWA UTAKUWA NA RANGI YA KAHAWIA?
Huo ni mchele au Mpunga, Wasukuma hawajui kutofautisha mchele na mpunga wao au shamba au umekobolewa wanaita mamichele na wale Jamaa ambao wamebahatika kuwa na mchele unanukia vizuri wale Malafyale nao kwao ni Mpunga tu.Naomba mnisaidie mchele ni upi na mpunga ni upi?
Mpunga, mchele, wali...?
Mchele mzuri ni ule wenye rangi ya kikahawia ingawa wengine wanapendelea mchele mweupe!
kaka mjengwa mchele unachambua siyo unachagua.....
Malafyale, mchele ni ule uliokwishakobolewa, na mpunga ni ule uliokuwa bado haujakobolewa. Na kuhusu kuchagua au kuchambua, pwani mpunga unachaguliwa sio kuchambuliwa! Ndio maana tunapoalikana shughuli zetu ambazo zinahitaji maandalizi ya chakula, huambizana "kesho kuna kazi ya kuchagua mchele!"
Mdau Mswahili
Kaka Maggid umenikumbusha ile methali ya "Amekula wali wa chuya kwa uvivu wa kuchagua". Baada ya mchele kukobolewa masalio ya mpunga katika mchele huitwa "chuya"
Wa Tanga.
Post a Comment