Subscribe:

Tuesday, June 30, 2009

Nimewasili Iringa Usiku Huu

Safari ya Dar mpaka Iringa siku hizi inachukua zaidi ya saa 10 kutokana na ujenzi wa barabara unaoendelea. Nimefurahi kurudi Iringa yenye baridi.
Maggid
Reactions::

Polisi Wavunja Shughuli Ya Harusi Tanga!



Tukio lisili la kawaida limeripotiwa leo kupitia TBC 1 kwamba polisi mkoani Tanga wameingilia kati na kuvunja shughuli ya harusi kwenye moja ya vijiji vya mkoa huo. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, polisi wameingilia kati kwa vile ndoa hiyo ilihusu msichana wa miaka 17 na aliyekatishwa masomo yake kuolewa na bwana wa umri wa miaka 50.

Polisi waliingia mahali hapo wakati Bi. Harusi, ndugu na waengine walioudhuria walipokuwa... soma zaidi; http://www.kwanzajamii.com
Reactions::

Utamu Wa Chungwa.....



Hausimuliwi kwa kula nanasi! Huu ni msimu wa machungwa, na yapo bwelele, chungwa moja linaanzia shilingi hamsini. Pichani ni Mtaa wa Jamhuri, Dar, jana mchana.
Reactions::

Mtoni Mtongani

Reactions::

FC Vito Malaika Ya Newala Wako Helsinki

Please inform the Tanzanian society that FC Vito Malaika from Newala plays in Helsinki Cup 2009. Matches start on 6th July. We will put all fixtures on www.liike.fi as soon as we get them from Helsinki Cup.



Karibuni wote cheer up the Malaika from South!



Br. Ari





Ari Koivu
Toiminnanjohtaja - Executive Director
LiiKe - Sport & Development

Radiokatu 20
00093 SLU, Helsinki, Finland
Telephone: +358 9 3481 2610
Fax: +358 9 3481 2602
Mobile: +358 40 765 9900
e-mail: ari.koivu@liike.fi
www.liike.fi
Reactions::

FC Vito Malaika Ya Newala Wako Helsinki

Please inform the Tanzanian society that FC Vito Malaika from Newala plays in Helsinki Cup 2009. Matches start on 6th July. We will put all fixtures on www.liike.fi as soon as we get them from Helsinki Cup.



Karibuni wote cheer up the Malaika from South!



Br. Ari





Ari Koivu
Toiminnanjohtaja - Executive Director
LiiKe - Sport & Development

Radiokatu 20
00093 SLU, Helsinki, Finland
Telephone: +358 9 3481 2610
Fax: +358 9 3481 2602
Mobile: +358 40 765 9900
e-mail: ari.koivu@liike.fi
www.liike.fi
Reactions::

Monday, June 29, 2009

Picha Moja,Tafsiri Elfu Moja!



Ukiitazama vema picha hiyo utaona noti ya shilingi elfu kumi aliyopewa msichana huyo mwanafunzi. Hapo ni eneo la Polisi Chang'ombe,jana Jumapili( Picha:KWANZA JAMII)
Reactions::

Yote Ya Mungu



Mitaa ya kati,Temeke jana Jumapili.
Reactions::

Mchumia Juani



Temeke,jana mchana.
Reactions::

Kichina!

Reactions::

Bora Mkono Huende Kinywani

Reactions::

KWANZA JAMII Juma Hili



Soma KWANZA JAMII mitaani na mtandaoni; http://www.kwanzajamii.com
Reactions::

Sunday, June 28, 2009

Tufanyeje Ili Turidhishane Kimapenzi?



Ilibainishwa humu hivi karibuni kuwa utafiti ulionyesha kuwa baadhi ya wanaume wana haraka ya kufanya sex. Habari ile bado inawafanya baadhi yenu kuendelea kunitumia mails zenye michango ya hoja na maswali pia. Soma zaidi; http://www.kwanzajamii.com
Reactions::

Sheikh Suleiman Gorogosi Amefariki Dunia Jana



Kaimu Mufti Mkuu, Sheikh Suleiman Gorogosi amefariki dunia katika ajali ya gari jana akiwa safarini akitokea Mtwara kwenda Lindi. Anatazamiwa kuzikwa leo. Sheikh Gorogosi ameacha pengo kubwa kwa uongozi wa BAKWATA, Waislamu na Jamii ya Watanzania kwa ujumla wake. Mungu Amlaze Mahala Pema Peponi,AMEN.
Reactions::

8-1: Namna Gani Bongo FC?!



Timu ya Watanzania waishio Sweden Kilimanjaro Stars iliwachabanga wenzao wa Bongo FC wa Finland kwa mabao 8-1. Ilikuwaje? Tunasubiri simulizi!
Reactions::

Prof. Haroub Othman Hatunaye Tena



PROFESA HAROUB OTHMAN ( PICHANI) AMEFARIKI DUNIA. NI KWA MUJIBU Wa TAARIFA ZILIZORIPOTIWA KWENYE MICHUZI BLOG NA MWANA WA MAREHEMU, TAHIR OTHMAN. MAREHEMU ALIKUTWA AMEFARIKI ASUBUHI HII AMBAPO JANA ALILALA AKIWA BUHERI WA AFYA.
ATAKUMBUKWA KWA MCHANGO WAKE MKUBWA KWA TAIFA LETU.
Reactions::

What is Development? Colonialism Deconstructed



Makala hii ya Profesa Mbele ilichapwa katika toleo la kwanza la ' KWANZA JAMII' chini ya kichwa cha habari; ' Maendeleo ni nini'. Mwandishi ameifanyia tafsiri na kuchapwa na gazeti la The Urban Fly la nchini Marekani. Tunamshukuru Profesa Mbele kwa jitihada zake za kusambaza maarifa hata yakafika Kasulu Kigoma, Marekani na kwingineko.

By Dr. Joseph Mbele
The Urban Fly
The concept of development is everywhere, in our personal lives and in the lives of communities and countries in general. We all believe that we need development. If we do not strive to develop, we get pressured in one way or another to do so. Other people try to force development on us. Soma zaidi; http://www.kwanzajamii.com, au http://www.theurbanfly.com
Reactions::

Saturday, June 27, 2009

Ngoma Afrika Band



Ras Makunja na Mzimu wake "The Ngoma Africa Band aka FFU,
wamejinyakulia nafasi ya pekee katika maonyesho ya mziki ya kimataifa ya "MASALA World Beat Festival, yaliyofanyika mjini Hannover,Ujerumani siku ya Jumapili ya 14-Juni-2009. Soma zaidi; http://www.kwanzajamii.com
Reactions::

Afro-Music Live In Stockholm



Lilla Wien Bar and Restaurant Present's
Afro-Music Soukous and Rumba with:
Maestro Vumbi Dekula and Sammy Kasule.
Date:03-04 July 2009 (Friday-Saturday) from 21-01
Address:Swedenborgsgatan 20 Södra Station Pendeltåg
Welcome and dance with us "Soukous Mashariki na Kati"
Reactions::

Ghorofa La Kwanza Kinondoni Biafra!



Ni la Bwana Majaliwa, kuna mnaomkumbuka.
Reactions::

Consultancy

Salaam Kaka Mjengwa

Hongera kwa kutupa habari za Bongo. Hapa tumeanzisha Firm ya Consultancy ya Biashara na taaluma, tunaomba uwahabarishe wadau kwa utambuzi. Tovuti yetu ni www.zabacco.com.

Kheri nyingi ziwe nawe

President
Zanzibar Business and Academic Consultancy
Reactions::

Friday, June 26, 2009

Mwinyi" Eeh Michael,Unaionaje Tanzania Yetu?"



Rais Mstaafu Mzee Ali Hassan Mwinyi alipata kukutana na Michael Jackson alipotembelea Tanzania.
Reactions::

Michael Jackson Amefariki Dunia



Akiwa na miaka 50. Michael Jackson ni legend; aliishi na kufanya mengi yaliyo mbele ya wakati wake. Atakumbukwa.

Michael Jackson aliwahi kufika Tanzania kwa ziara ya kitalii miaka ya 90. Inasimuliwa, kuwa pale Kilimanjaro Hotel alipofikia alisikia kelele za washabiki jioni ile. Akachungulia dirishani na kuuliza kama wamekuja kumwona yeye. Akajibiwa; ” Hao ni washabiki wa klabu ya Simba wanarudi wakishangilia ushindi wa timu yao wakitokea Uwanja wa Taifa na kwenda kukiwahi kivuko. Katika wakati ule ambapo televisheni hazikuwapo, Michael Jackson hakuwa maarufu sana kuizidi Simba na Yanga!
Reactions::

Haya Tena!



Ni kwenye Vodacom Dar Half Marathon hivi karibuni.
Reactions::

Thursday, June 25, 2009

Picha Hii Na Maadili: BAP Anachambua Kwa Kina



“Je, ni makosa kwa mpiga picha endapo mtoto huyu ataliwa na tai?Au si kosa kwa mpiga mpicha kwani ametusaidia kufahamu ukubwa wa tatizo. Kwamba eneo hilo limekubwa na ukame na njaa kali kiasi cha mama kufa au kuondoka na kumwacha mtoto wake.”

Swali na tamko hilo hapo juu ni mojawapo ya viini muhimu vya uandishi (journalism) na usambazaji (dissemination) wa habari na mawasiliano. Yote hayo mawili yana utata wake:

Mosi, wanahabari wanakabiliwa na maswali, matatizo, na kero za ki-taaluma. Wakati mwingine huwa ni vigumu sana kuweza kueleza habari bila kuingilia kati, ingawa wataalamu wa taaluma ya habari hujigamba kuwa mwanahabari hawezi kuwa sehemu ya habari! Soma zaidi; http://www.kwanzajamii.com
Reactions::

Huduma Mpya! AIR ZARA INTERNATIONAL!



Kuanzia kesho kutakuwa na huduma mpya ya usafiri wa ndege kwa abiria ( Scheduled Commercial flights)kwenda na kutoa Zanzibar, Mafia, Iringa na kwingineko. Kwa habari zaidi tembelea; http://www.airzara.com
Reactions::

Wanaume Waoga Wa Kutongozwa!



Baadhi ya wanaume ni waoga wa kutongozwa na wanawake. Hii ni kwa mujibu wa tafiti na uzoefu uliopo. Hapa kuna sababu za kijamii ikiwamo malezi, mila na desturi.
Bado inaonekana na wengi kama kitendo cha ajabu kwa mwanamke kuanza kuchukua hatua za kumtongoza mwanamme anayempenda ama kuvutiwa naye.Soma zaidi; http://www.kwanzajamii.com
Reactions::

" Nimepunguza Kidogo!"


Mmoja wa walishiriki wa Vodacom Dar Half Marathon Jumapili iliyopita.
Reactions::

Muhogo Huu!


Mahitaji ya muhogo yameongezeka hususan katika Jiji la Dar Es Salaam na vitongoji vyake. Tafiti zaidi zinahitajika kufanywa ili kuboresha zao hili.
Reactions::

Wednesday, June 24, 2009

Changamoto Ya Kimaadili



Je, ni makosa kwa mpiga picha endapo mtoto huyu ataliwa na tai?Au si kosa kwa mpiga mpicha kwani ametusaidia kufahamu ukubwa wa tatizo.Kwamba eneo hilo limekubwa na ukame na njaa kali kiasi cha mama kufa au kuondoka na kumwacha mtoto wake. Picha hiyo iliyopigwa na mpiga picha mahiri barani Afrika ( Marehemu Mohammed Amin) ndiyo iliyouamsha ulimwengu na kutambua kuwa Ethiopia ilihitaji msaada wa haraka kutokana na kukumbwa na ukame na njaa.
Reactions::

Kambona Alikuwa Na Mvuto Kwa Wanawake



Wanawake waliiga staili yake ya nywele!

Na Born Again Pagan

BADO tunajenga muktadha wa matukio ya ki-mataifa, ki-ukanda (regional) na ki-taifa (Tanzania) uliozalisha msimamo mkali wa baadhi ya wanafunzi vijana wa Mlim,anai miaka ya 1960-hadi 1970. Soma zaidi; http://www.kwanzajamii.com
Reactions::

Wabunge Fungeni Virago Mwende Kwenu!



Wabunge Fungeni Virago Mwende Kwenu!

Na Padri Privatus Karugendo

KATIKA hali ya kawaida hakuna Mtanzania aliyekuwa na imani kwamba Wabunge wetu wangeweza kukwamisha Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka 2009/2010; wengi tuliamini ingepitishwa kama zinavyopitishwa zote kila mwaka. Kuna sababu nyingi za kuamini hivyo: Idadi kubwa ya Wabunge ni ya chama tawala, Bajeti inaandaliwa na serikali, na !serikali inaongozwa na chama tawala: Haiwezekani chama kikajikwamisha hata kama bajeti ingekuwa mbaya namna gani. Rais wa nchi anatoka chama tawala yeye ndiye mwenyekiti wa chama hicho tawala; hotuba yake kabla ya bajeti ilikuwa inatengeneza njia; uchaguzi mkuu ni mwaka kesho, wabunge wote wa chama wanapita katika mchakato wa chama, hivyo ni lazima kuwa “watoto” wazuri ili wateuliwe kugombea tena katika uchaguzi mkuu ujao; hata hivyo hakuna historia ya Bunge la Tanzaniaa kukwamisha bajeti. Soma zaidi; http://www.kwanzajamii.com
Reactions::

Hata Kama Kutangulia Si Kufika...



Pamoja na kuongoza kundi hilo kwa kasi nzuri ya kuanzia, baada ya km 10 hivi nilimkuta kijana huyo mwenye namba 301 akitembea kama mtu anayekwenda dukani pale maeneo ya Kivukoni Front. Natumaini aliweza kumaliza km 21 hata kwa kutembea. Naam. Hata kama kutangulia si kufika, ni bora ufike salama.
Reactions::

Chupa Hii Tupu Inampatia Senti Ishirini Na Tano!



Pichani ni mama anayetafuta riziki yake ya siku kwenye Vodacom Dar Half Marathon hivi majuzi. ( Picha ya KWANZA JAMII)
Reactions::

Tuesday, June 23, 2009

Wote Wana Makosa



Kijana huyo pichani amekutwa akiiba kioo cha pembeni cha gari. Ni kosa. Vijana hao nao nimewakuta wakiwa wamejichukulia sheria mkononi na kutoa hukumu, ni kosa pia. mahali ni Pamba Road, Dar leo mchana. Je, wengine mnasemaje?
Reactions::

Kivumbi Jumamosi,Finland!



FC Bongo will host KILIMANJARO FC from stockholm this saturday of 27th june 2009 at 12 to 2.00 afternoon at KÄPYLÄ URHEILUPUISTO Helsinki.
This will be the first time FC BONGO Hosting KILIMANJARO FC and the second time meeting.
The first time was last summer when FC BONGO visited KILIMANJARO in stockholm and KILIMANJARO won the trophy by winning 4-3. This time the winner will be awarded the same trophy.
The team which is going to win the trophy 3 times in a row will be awarded the trophy permanently.

FC BONGO have manage to win all prevention cup games last year and won the trophy, but it was hard to win KILIMANJARO in stockholm.

Is it gonna be the same story this time?

Please forward this invitation to all friends around.

Regards: Ezza
Reactions::

MKUTANO WA WATANZANIA ROME, ITALIA

Reactions::

Tuwaache Watoto Wawe Watoto



Tuwaache watoto wawe watoto, wafurahie maisha ya utoto. Hutajafanya ya kutosha kuwafanya watoto wengi wa Kitanzania wafurahie maisha ya utoto ikiwamo kuwatengea viwanja na bustani za michezo.Pichani ni watoto wa Bagamoyo.
Reactions::

Nanasi La Bagamoyo



Moja unalipata sokoni kwa shilingi mia sita. Ukilikata unapanda idadi hiyo ya vipande vya nanasi. Kuongezeka au kupungua kwa idadi ya vipande inategemea na mkataji. Hilo nimelikata mimi!
Reactions::

Soko Kuu Bagamoyo Jana Mchana

Reactions::

Monday, June 22, 2009

Korosho Za Mapinga



Mama akiuza korosho na kusuka ukili. Korosho paketi shilingi mia mbili. Bagamoyo mjini jana Jumapili.
Reactions::

Huduma


Jana Jumapili kwenye Vodacom Dar Half Marathon.
Reactions::

Pumzi Anazo!


Mmoja wa washiriki wa mbio za riadha za Vodacom Dar Half Marathon, jana Jumapili. ( Picha: KWANZA JAMII)
Reactions::

Joto Liliwachemsha Wengi Jana



Vodacom Dar Half Marathon ya jana ilikuwa ngumu kwa wengi kutokana na joto kali kwa siku ya jana.
Reactions::

Sunday, June 21, 2009

Niko Bagamoyo!



Baada ya kumaliza mbio za Vodacom Dar Half Marathon asubuhi hii, niliondoka moja kwa moja na kuja hapa Bagamoyo. Pwani ya Bagamoyo ni nzuri, nimetumia muda mwingi wa leo nikiwa pwani, kujisomea na kutembea kandokando ya bahari. Nilipata nafasi pia ya kutembelea mitaa ya kati ya mji wa Bagamoyo. Hakika Bagamoyo ni kuzuri!
Reactions::

Pwani Ya Bagamoyo


Leo jioni.
Reactions::

Mh.Kawambwa: "E Bwana Njoo Karibu!"



Leo kwenye mitaa ya Bagamoyo nilipata bahati ya kukutana na Mh. Shukuru Kawambwa, Mbunge wa Bagamoyo na Waziri Wa Miundo Mbinu. Pichani Mh. Kawambwa akimsogeza karibu mmoja wa ' wapiga debe' wake kwenye picha ya ukumbusho.
Reactions::

Bagamoyo Umefika Hapa!

Reactions::

CCM Kijiji Cha Mapinga


Bagamoyo,leo.
Reactions::

KWANZA JAMII Liko Tayari


Litakuwa mitaani na mtandaoni kuanzia keshokutwa. Tembelea; http://www.kwanzajamii.com
Reactions::

Nimevunja Rekodi Yangu!



Ya mwaka jana ni kilomita 21 kwa saa moja na dakika 52. Mwaka huu nimetumia saa moja na dakika 49. Mbio zilikuwa ngumu kutokana na jua na joto kali kama ilivyotazamiwa. Tulianza saa mbili na robo asubuhi. Zilikuwa ni mbio za kuvutia. Kuiona Dar Es Salaam kwa njia ya marathon ni kitu cha kipekee kabisa. Na mazoezi yangu ya mchangani pale Oysterbay Beach jana jioni na huko nyuma bila shaka yameniongezea pumzi nilizohitaji kuweza kukimbia kilomita 21 bila kusimama.
Reactions::

Kumbukumbu!

Reactions::

Kijiwe Cha 'Black Wizard' Kinondoni



Jana jioni. Pichani ni kaka zangu; Kushoto ni Mwemba Mtokambali Mwilima na kulia ni Mbaruku.
Reactions::

Saturday, June 20, 2009

Ng'ombe Hanenepi Siku Ya Mnada!





Kesho asubuhi nitakimbia Vodacom Dar Half Marathon, ni kilomita 21. Lengo ni kuivunja rekodi yangu mwenyewe ya mwaka jana ( Coca-Cola Dar Half Marathon). Nilitumia saa moja na dakika 52. Mwaka jana tulianza saa kumi na mbili na nusu asubuhi. Mwaka huu mbio zitaanza saa mbili asubuhi, ni kiyama,maana Dar ina joto kali kwa sasa,na kesho kutakuwa na jua kali na joto kali pia. Soma zaidi; http://www.kwanzajamii.com
Reactions::