
Askai Polisi wakitoa jiwe kubwa lililotegwa na wanafunzi wa Kibasila ili magari yasipite

Wanafunzi wa Kibasila wakiwasaidia wenzao na kuwapepea baada ya kuzirai kutokana na ,mabomu ya machozi na kipigo kutoka kwa askari.

Wanafunzi wakiwasaidian wenzqao kwa kuwapepea.

Wanafunzi wakitoa msaada kwa wenzao baada ya kipigo.

Wanafunzi wa Kibasila wakiwapeleka wenzao waliozidiwa hospitali.
POLISI wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam leo wamelazimika kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Kibasila waliokuwa wamefunga barabara ya Mandela na Chang’ombe kwa kutumia mawe makubwa yaliyokuwa kandokando ya barabara hizo.
Kikosi hicho chenye askari 11 walilazimika kutumia mabomu ya machozi kutokana na wanafunzi hao zaidi ya 200 wa Sekondari hiyo kupinga hatua ya kugongwa kwa mwananafunzi mwenzao Emmanuel Mapande.
Tukio hilo limettokea leo majira ya saa 3:30 asubuhi, kwenye makutano ya barabara hizo zilizopo karibu na kituo cha Polisi cha Chan’gombe.
Tanzania Daima lilikuweko kwenye eneo hilo baada ya kupata taarifa kutoka kwa baadhi ya askari kufuatiwa kugongwa mwanafunzi hiyo na basi la abiria aina ya Toyota Coaster ambalo lilitoweka baada ya kufanyika kwa tukio hilo, hata hivyo namba zake badi hajizafahamika bado.
Tanzania Daima lilishuhudia kiongozi wa askari hao akiwaamrisha askari kutumia mabomu zaidi kwa wanafunzi hao kutokana na kukaidi kuondoka eneo la barabara huku wakizuia magari kuendelea na safari, mengine kuvunjwa vioo.
“Tutumia mabomu ya machozi wanafunzi hawa wanakaidi amri ya Polisi, basi na sisi tunatumia nguvu kuwaondoa” alisema Kiongozi huyo.
Amri hiyo iliwafanya askari wenye silaha hizo kurusha mabomu hadi kwenye eneo la shule ya sekondari hiyo, huku wanafunzi hao wakijibu mashambulizi kwa kuwarushia mawe kwa askari hao.
Hata hivyo walionekana wanafunzi hao wakitokwa na machozi kutokana na madhara ya mabomu hayo na wengine ambao idadi yao haijafahamika mara moja wamekimbizwa kwenye hospitali ya Temeke kwa matibabu zaidi.
Walikimbizwa hospitali ni;Agatha Kivuvyro, Yusta Herman, Fani Abdul, Kuruthum Athanas, Jackline Gades na Mary Richard.
Wengine ni pamoja na Janeth Kagoa, Anet Kiyogoa na Mary Shao wote wa kidato cha nne na tano.
Baadhi ya wanafunzi waliiambia Tanzania Daima kuwa, mwanafunzi huyo wa kidato cha sita, aligongwa majira ya asubuhi wakati akivuka barabara akitokea shuleni.
“Amegongwa wakati akitoka maeneo ya shule kuelekea nje, hata hivyo ilikuwa ni makusidi ya dereva kwani yeye (dereva), anafahamu kuwa barabara hii inatengenezwa kwa sasa” alidai mwanafunzi huyo ambaye hakitaka kujata jina lake.
Wakizungumza leo wanafunzi wanaosoma katika shule hiyo waliziomba mamlaka zinazohusika kuweka taa za kuongozea magari ili kupunguza ajali katika eneo hilo ambalo pia ni maarufu kama "machinjioni"
Chanzo: Issa Michuzi)