
Pichani: Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Kuu ya Taifa ya Takwimu,(NBS) Dkt, Albina Chuwa akihudhuria Mkutano wa 45 wa Kamisheni ya Takwimu ya Umoja wa Mataifa (UNSD). Mkutano huo uliofanyika kwa siku nne uliwakutanisha Wakurugenzi Wakuu wa Takwimu na Wataalamu wa takwimu kutoka nchi 192 Wanachama wa Umoja wa Mataifa. Katika Mkutano huo, ajenda iliyoibua mjadala mkali kati ya wataalamu hao na sekretarieti ya Kamisheni ya Takwimu ya Umoja wa Mataifa, ilikuwa ni ile iliyohusu Taarifa ya Maendeleo ya Watu Duniani ya Mwaka 2010. aliyekaa nyuma ni Bi Redegunda Maro, Mkurugenzi wa Idara ya Operesheni za Takwimu kutoka Idara kuu ya Takwimu, Mkutano huo pia ulihudhuriwa na Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Bw. Mohamed Hafidhi hayupo pichani.
·
NI YA MWAKA 2010 WASEMA IMAJAA KASORO KIBAO
Na Mwandishi Maalum
New York-Kasoro kadhaa zikiwamo za upotoshaji mkubwa wa takwimu zilizomo
katika Taarifa ya Maendeleo ya Watu Duniani ya Mwaka 2010( Human Development
Report) kumewafanya Wakurugenzi Wakuu wa Takwimu kutoka nchi za Umoja wa
Mataifa kugeuka mbogo na kuzijia juu Taasisi zilizoandaa taarifa hiyo.
Wakuu wa maswala ya takwimu walikutana hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa,
wakihudhuria mkutano wa 45 wa Kamisheni ya Takwimu ya UM ( UNSD). Mkutano
huo wa siku nne, uliomalizika ijumaa, ulijadili ajenda mbalimbali zikiwamo hiyo ya
Taarifa ya Maendeleo ya Watu Duniani ya mwaka 2010.
Kwa ujumla
hali katika
chumba cha mkutano wa Kamisheni hiyo, ilikuwa ya
sintofahamu, huku kila mjumbe aliyechangia taarifa hiyo,
akishindwa kudhibiti
hasira, uchungu na masikitiko ya waziwazi ya kutoridhishwa na namna taarifa hiyo
ilivyoandaliwa huku ikiwa na mapungufu yasiyo yakawaida.
Licha ya kwamba takwimu zilikuwa ama zimekosewa ama zimepotoshwa nchi kadhaa
hazikutokea kabisa kwenye taarifa hiyo.
Ujumbe wa Tanzania katika mkutano huo ulijumuisha Mkurugenzi Mkuu wa Idara
Kuu ya Taifa ya Takwimu, Dkt. Albina Chuwa, Bw. Mohamed Hafidhi Mtakwimu
Mkuu Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Bi. Radegunda Maro Mkurugenzi wa Idara ya
Operesheni za Takwimu.
Akichangia mjadala wa Taarifa hiyo, Dkt. Albina Chuwa anasema.“ Serikali yangu
inaungana na wasemaji waliotangulia, kuhusu upotoshwaji mkubwa wa takwimu
zilizoonyeshwa kwenye taarifa hiyo zikiwamo za nchi yangu Tanzania, sijui UNDP
wamezitoa wapi takwimu hizi , sisi kama wenye dhamana na masuala yote yahusuyo
takwimu, hatukushirikishwa ni wazi kwamba UNDP wametumia takwimu ambazo sisi
hatukuziridhia na wala hazina baraka ya ofisi yangu.
1
Akiongea kwa hisia kali, Dkt. Chuwa amesema . “Ni wazi kwamba zoezi zima
la maandalizi ya taarifa hiyo yameishia katika ukiukwaji wa kanuni na taratibu
zilizokubalika kimataifa za uchambuzi na usambazaji wa taarifa za takwimu za nchi
wanachama”.
Akasema kuwa Tanzania ingependa kuona, Kamisheni ya Takwimu ya Umoja
wa Mataifa ( UNSD) ikizifanyia kazi hoja zilitotolewa na nchi wanachama kuhusu
mapungufu yaliyomo katika Taarifa hiyo ambayo ilizinduliwa mwaka uliopita.
Wajumbe wa Kamisheni hiyo wameeleza na kusisitiza kwamba, wakati wanatambua
umuhimu wa Taarifa ya Maendeleo ya Binadamu kama nyenzo muhimu katika
uendeshaji wa mijadala ihusuyo maendeleo ya watu
kitaifa na kimataifa. Lakini
wamelazimika kuelezea masikitiko yao kuhusu vyanzo vya takwimu na mbinu
zilizotumiwa kuaanda taarifa hiyo.
Watakwimu Wakuu kutoka Serikali za Afrika ya Kusini, na Suriname na ambao majina
yao hayakupatikana mara moja. Pamoja na kuelezea masikitiko yao juu ya taarifa
hiyo. Wametaka masikitiko na maelezo yaliyotolewa na wajumbe ya kutoridhishwa
na taarifa hiyo, maelezo na malalamiko hayo yajitokeze kama yalivyoelezwa na
wajumbe katika majumuisho ya mwisho ya mkutano huo.
“ Ujumbe wangu unasisitiza kwamba hisia zilizoonyeshwa na wajumbe wa mkutano
huu, za kutoridhishwa na taarifa hii, zijitokeze kwenye taarifa ya mwisho ya mkutano
huu kama zilivyotolewa, sisi ni wataalam wa takwimu na si wanadiplomasia hakuna
kupindisha lugha hapa” akasisitiza Mjumbe huyo wa Suriname. Kauli iliyoungwa mkono
na wajumbe wengi.
Wajumbe wameipa miezi mitatu Kamisheni ya Takwimu ya Umoja wa Mataifa, kutoa
taarifa yenye majibu ya hoja zilizotolewa na wajumbe kuhusu kasoro za taatia hiyo.
Aidha katika mambo mengine yaliyolalamikiwa na wajumbe katika taarifa hiyo ni
pamoja kutoridhishwa na matumizi ya takwimu ambazo hazikuwa rasmi na ambazo
zimepatika kutoka vyanzo visivyo rasmi.
2
Kwa sababu hiyo wamesisitiza kuwa pale ambapo takwimu rasmi zinakosekana, basi
matumizi ya takwimu zisizo rasmi razima yapate ridhaa ya nchi husika.
Halikadharika washiriki wa mkutano huo, pia wameelezea masikitiko yao kuhusu
utofauti na upishanaji mkubwa wa taarifa za kitakwimu kati ya Taasisi moja na
nyingine ndani ya Umoja wa Mataifa. Na wakatoa wito wa kutaka kurekebishwa kwa
tofauti hizo haraka.
Vile vile Watakwimu hao wamezitaka taasisi zinazoandaa taarifa hiyo ya maendeleo ya
binadamu duniani, kuwasiliana na wataalamu wa takwimu wa kila nchi kabla ya kutoa
hadharani taarifa hiyo ili kuepusha kujirudia kwa matatizo na makosa yaliyojitokeza
katika taarifa ya mwaka jana.
Taarifa ya Maendeleo ya Watu Duniani huandaliwa na Mfuko wa Maendeleo wa
Umoja wa Mataifa (UNDP) kwa kuzishirikiana na taasisi nyingine za kimataifa na
kwa kufanya kazi kwa karibu na nchi husika kupitia Idara za Takwimu. Lakini katika
hali ya kushangaza, taarifa zinaonyesha kuwa taarifa ya mwaka jana, utaratibu huo
haukuzingatiwa hasa eneo la ushirikishwaji nchi husika.
Wakati huo huo, Tanzania kupitia Mkurugenzi Mkuu wa Takwimu, imetoa taarifa
kwamba, sensa ya idadi ya watu na makazi itafanyika mwakani (2012).
Katika hatua nyingine Idara Kuu ya Taifa ya Takwimu ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania imechaguliwa kuwa Mjumbe katika Kamisheni ya Takwimu ya Umoja wa
Mataifa ikiwakilisha Bara la Afrika. Tanzania itakuwa mjumbe wa Kamisheni hiyo kwa
kipindi cha miaka minne kuanzia mwakani 2012.