Subscribe:

Thursday, June 30, 2011

Mwenyekiti Wa CCM Iringa Atiwa Mbaroni Kwa Kujifanya Afisa Wa TAKUKURU

TAASISI ya kupambana na kuzuia Rushwa nchini (TAKUKURU) mkoa wa Iringa imemfikisha mahakamani mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) mtaa wa Kihodombi katika Manispaa ya Iringa Aldo Kaduma (50)kwa tuhuma za kujifanya afisa wa taasisi hiyo na kuomba rushwa ya shilingi 400,000 kutoka kwa paroko wa Ihemi Iringa vijijini asifukuzwe nchini ndani ya masaa 24 kwa kosa la kumtetea mfanyakazi wake aliyemweka kinyumba mwanafunzi.
Mwanasheria wa Takukuru, Nitume Mizizi alisema leo mahakamani hapo kuwa Kaduma alikamatwa Septemba 28, 2009 baada ya taasisi hiyo kupokea taarifa kutoka kwa Padri Pio Callegari (72) kuhusu mtuhumiwa huyo kuomba rushwa hiyo ili kusaidia kuendelea kuwepo nchini kabla ya taasisi hiyo kuwekea mtego wa rushwa uliozaa matunda.
Alisema kuwa mtuhumiwa huyo aliomba kuongezwa fedha kiasi cha shilingi 100,000 ili kufikia shilingi 400,000 ambazo aliomba awali na baadhi hya fedha hizo kupewa kabla .
"Kaduma alimtisha Padri huyo kwamba ofisi ya Takukuru mjini Iringa ambako yeye anafanya kazi imepokea taarifa ikumuhusu Padri huyo kutoa rushwa kwa askari wa kituo cha Polisi Ifunda ili kuzima kashfa ya mfanyakazi wake kumtorosha mwanafunzi huyo na kuishi naye"
Hata hivyo kabla hajapewa fedha hizo, Padri huyo na wasaidizi wake walibaini kwamba Kaduma si afisa wa taasisi hiyo na nyingine yoyote ya usalama kwani walipokwenda katika ofisi ya Takukuru mjini Iringa ili kuomba msaada wake ilibainika kwamba hakuna mfanyakazi mwenye jina kama hilo katika ofisi hiyo.
Alipotafutwa kwa njia ya simu aliwaomba wakutane katika maeneo ya hotel ya Staff Inn Annex iliyopo mjini Iringa ili wamalize suala hilo ambalo bila kujua tayari suala hilo liliripotiwa Takukuru .
Kaduma aliingia mikononi mwa Takukuru kirahisi baada ya Padri huyo na Takukuru kutengeneza mtego uliowezesha kukamatwa kwake baada ya kukubali kupokea Sh 150,000 kati ya Sh 400,000 alizoomba.
Padri Callegari ambaye anafanyashughuli zake katika Kanisa la Romani Katoliki, Parokia ya Ihemi Iringa Vijijini ambaye mmoja wa wafanyakazi wake alikuwa akituhumiwa kumweka kinyumba mwanafunzi wa darasa la tano wa shule ya msingi Ihemi kabla ya paroko huyo kumsaidia .
Hata hivyo wengine wanaodaiwa kutishwa na mtuhumiwa huyo kuwa ni pamoja na Velenci Nhyengelo (44) ambaye ni mzazi wa mwanafunzi huyo ,Antony Maginga(37) ambaye ni mtumishi wa shamba la Paroko huyo na mkuu wa shule ya Ihemi Edga Mkwama ambao walitishwa kuwa kama hawatamshawishi paroko huyo kutoa fedha hizo baada ya paroko huyo kuondoldewa nchini ndani ya masaa 24 kurudi kwao Italia wao watafungwa jela miaka 30 kila mmoja. Imeandikwa na Francis Godwin kutoka Iringa.
Reactions::

Muungano Wa Afrika Waishutumu Ufaransa

Kamishna wa tume ya Muungano wa Afrika Jean Ping amesema kuwa uamuzi wa Ufaransa kuwarushia silaha waasi wa Libya kutoka angani ni hatari na kuwa mtindo huo unahatarisha eneo zima.
Ameiambia BBC kuwa hatua hii huenda ikaitumbukiza Libya katika matatizo sawa na yale yanayoonekana katika nchi ya Somalia ambayo imekabiliwa na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe kwa miaka mingi.
Ufaransa imekiri kuwa iliwapa silaha wapiganaji wa Berber kwa kuzirusha toka angani katika milima ya kusini-mashariki mwa mji mkuu wa Tripoli.
Wadadisi wanasema kuwa hatua hiyo huenda inakiuka vikwazo vilivyowekwa na baraza la usalama la Umoja wa Mataifa kupinga silaha kupelekwa Libya.
Bw Ping alikuwa anazungumza kutoka Equatorial Guinea ambako viongozi wa Afrika wanakutana katika kikao cha kikele cha Muungano wa Afrika.       
Suala la Libya inatarajiwa kupewa kipaumbele katika mkutano huo.
Bw Ping amesema kuwa mpango wa amani wa Muungano wa Afrika kwa Libya ulioafikiwa mwezi Marchi bado upo na unafaa. Mpango huu unahusu utaratibu wa amani unaonuiwa kufungua njia ya mazungumzo ya kisiasa.
Taarifa kuhusu Ufaransa kuwapa silaha waasi zilifichuliwa na gazeti la Le Figaro hapo jana.Gazeti hilo liliongeza kusema kuwa Ufaransa haikuwafahamisha wenzake katika kikosi cha kujihami cha Nato kuhusu hatua yake hiyo.

Hofu ya kuendelea kwa mapigano

.
Taarifa hiyo imesema silaha hizo ni pamoja na makombora ingawa maafisa wa Ufaransa wanasisitiza na kuthibitisha kuwa silaha zilizorushiwa waasi hao zilikuwa ndogo ndogo.
Uwamuzi huu inaarifiwa uliafikiwa baada ya mkutano wa mwezi Aprili kati ya Rais Sarkozy wa Ufaransa na kiongozi wa wapiganaji wa waasi Jenerali Abdel Ifatah Younis.
Ufaransa imekuwa ikionesha wasiwasi wake kuhusu kuendelea kwa mapigano haya ya Libya yalioanza mwezi February.
Waasi wameonekana kupiga hatua na wanatumai kuelekea Tripoli kutokea maeneo ya milimani ya Nafusa kilomita 65 kutoka mji mkuu huo.
Urusi na Uchina zimeshutumu mashambulio ya Nato, zikisema kuwa yamevuka mipaka ya azimio la Umoja wa Mataifa la mwaka 1973 linaloruhusu hatua za kijeshi kuchukuliwa nchini Libya.
Hatahivyo Marekani inasema kuwa azimio la mwaka 1973 linaruhusu nchi kuwapa waasi silaha licha ya azimio la awali la mwaka 1970 ambalo liliiwekea Libya vikwazo vya silaha. BBC
Reactions::

Balozi Wa Ireland Atembelea Maonesho Ya Sabasaba

Balozi wa Ireland nchini  Lorcam Fullam akiweka saini kitabu cha wageni leo mchana katika Jengo la NDC, alipotembelea jengo hilo.

Meneja ufundi wa kiwanda cha  Uzalishaji  Chuma Ghafi, Maganga Matitu  kilichopo Ludewa Mkoani Iringa, akimwelekeza  Balozi wa Ireland nchini, aina mbali mbali ya Chuma Ghafi inayopatikana Ludewa, wakati Balozi huyo alipotembelea Jengo la NDC kwenye Maonesho ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea  jijini Dar es Salaam.



Mtaalamu wa Miamba, Alex Sostanes, akitoa maelekezo ya aina mbali mbali za miamba kwa Balozi wa Ireland katika jengo la NDC leo mchana kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea jijini Dar es Salaam. Picha zote na Victor Makinda
Reactions::

Mengi Atembelea Sabasaba

Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP Media Reginald Mengi na Mwenyekiti wa EOTF wakimsikiliza mmoja wa waonyeshaji wa biadhaa kutoka Zanzibar wanaoshiriki maonyesho ya 35 ya kimataifa ya biashara ya Dar es salaam chini ya banda la EOTF.

Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Media Reginald Mengi(kulia) na Mwenyekiti wa EOTF Mama Anna Mkapa(kushoto) wakibadilishana mawazojana jijini Dar es salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa EOTF Stephen Emmanuel (katikati) mara baada ya Bwana Mengi kutembelea banda la EOTF jana wakati wa maonyeasho ya 35 ya kimataifa ya biashara ya Dar es salaam yanayoendelea jijini Dar es salaam.
Picha na Tiganya Vincent-MAELEZO-Dar es salaam
Reactions::

Wakala Wa Vipimo Watoa Somo

 Afisa Vipimo Mkuu, Wakala wa Vipimo wa Serikali, akiwaelekeza wananchi namna sahihi ya kutumia mzani leo mchana kwenye maonesho ya Kimataifa ya Biashara ya (Sabasaba) jiji Dar es Salaam.  Afisa huyo alibainisha mbinu mbalimbali zinazotumiwa na wafanyabishara kuwapunja wateja  ikiwa ni pamoja na kutumia feni za juu kupuliza eneo la mzano hali ambayo hufanya kipimo kutokuwa sahihi.Picha na Victor Makinda
Reactions::

Nape Atembelea Mwananchi Na Global Publishers

Nape akizungumza na wafanyakazi wa Global Publishers katika chumba cha habari cha Global. Wengine ni Mrisho, Ndauka, Sixtus na Ally.

Nape akiwa katika ofisi za Global Publishers.Kushoto ni  Abdallah Mrisho Wengine kutoka kulia ni, Sixtus Mapunda, Maloto,Ndauka na Mhariri kiongozi wa michezo wa Global Saleh Ally.

Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akisalimiana na Meneja Mkuu wa Kampuni ya Global Publishers, wachapishaji wa magazeti ya Uwazi, Kiu, Ijumaa na Champion, Abdallah Mrisho, baada ya kuwasili Ofisi za kampuni hiyo,Mwenge, Dar es Salaam.jana. Wapili kulia ni Mhariri Kiongozi wa kampuni hiyo    na Mhariri Kiongozi Oscar  Ndauka na Mwandishi wa kampuni hiyo Luqman Maloto na wapili kushoto ni Katibu Msaidizi Mkuu wa Idara ya Itikadi na Uenezi, Sixtus Mapunda. Picha na Bashir Nkoromo.
Reactions::

JK Yuko Malabo, Equatorial Guinea


1. Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na baadhi ya marais wakuu wa nchi za Umoja wa Afrika AU wakimpongeza Rais mstaafu wa Brazil Lula Da Silva kwa hotuba yake aliyoitoa wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa 17 wa Wakuu wa nchi za AU uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Sipopo,jijini Malabo,Equatorial Guinea leo asubuhi.Hotuba hiyo ya kusisimua ilitilia mkazo kwa nchi za Afrika kushirikiana ili kujiletea maendeleo na kuepuka misaada yenye masharti inayolididimiza bara la Afrika katika lindi la umaskini.
 
2.Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akishiriki katika ufunguzi wa Mkutano wa 17 wa Umoja wa Afrika unaofanyika jijini Malabo, Equatorial Guinea(Picha: Freddy Maro)
Reactions::

Siku Kafulila Alipounguruma Jimboni Kwake!

Kigoma Kusini. Picha: Richard Mwaikenda
Reactions::

Ngoma Za Asili Zipo, Zina Hadhi Na Nafasi Kubwa; Lasema BASATA

Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limesema kwamba,ngoma za asili bado zina hadhi na nafasi kubwa katika jamii zetu ingawa kwa maeneo ya mijini mwamko wa sanaa hiyo unaonekana kupungua tofauti na zamani.
Akizungumza kwenye Jukwaa la Sanaa linalofanyika kila wiki makao makuu ya Baraza hilo Ilala Sharif Shamba,Katibu Mtendaji wa BASATA,Ghonche Materego alisema kwamba,ngoma za asili zipo kama kawaida na zimekuwa na nafasi kubwa mikoani ambako zimekuwa zikivuta watu wengi.
“Kuna matamasha makubwa ya ngoma za asili kama yale ya Makuya, ya kale yanapokutana na ya sasa, Bujora na Chamwino.Matamasha haya yamekuwa yakivuta watu wengi sana hivyo,dhana kwamba ngoma za asili zimetoweka si sahihi” alisema Materego.
Aliongeza kwamba,kinachotokea kwa sasa ni athari za utandawazi kwenye ngoma za asili ambazo zimebadili upepo wa sanaa hiyo maeneo ya mijini lakini akasisitiza kwamba,bado hata maeneo ya mijini kuna vikundi vingi vya ngoma za asili vinavyofanya vizuri.
“Utandawazi kwa kiasi fulani umeathiri ngoma za asili hasa maeneo ya mijini lakini bado hata hivyo kuna vikundi vingi Baraza limevisajili na kuvisimamia mijini kama hiki kilichotuburudisha leo cha Jivunie Tanzania” Alisisitiza Materego.
Alitoa wito kwa wakuzaji sanaa kujikita kwenye kuandaa matamasha mbalimbali ya sanaa za asili ili kuzidi kuisambaza sanaa hiyo ambayo ni muhimu sana kwa utambulisho wa utamaduni wetu na kwa muda mrefu imelijengea heshima taifa letu.
“Ni kweli tuna matamasha mengi ya ngoma za asili lakini ni wazi juhudi nyingi zinahitajika ili kujenga mwamko zaidi katika sanaa hizi.Ni muhumu ikaeleweka kwamba,sanaa hizi zinabeba kila kitu ndani ya jamii” alimalizia Materego.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kundi la Sanaa la Jivunie Tanzania,Bi.Mariam Ismail alisema kwamba, watanzania wasiache kupenda ngoma za asili na kupapatikia vitu vya nje kwani kufanya hivyo ni kupuuza malezi na historia za jamii zao.
Jukwaa la Sanaa kila mwisho wa mwezi linapambwa na burudani mbalimbali na kwa mwezi huu Kundi la Sanaa la Jivunie Tanzania kutoka Temeke Dar es Salaam lilitoa burudani kedekede za asili.
Reactions::

Maonesho Ya Kimataifa Ya Biashara(Sabasaba); Tembelea Wizara Ya Fedha Na Uchumi Uelimike

Ikiwa unaingia ndani ya Viwanja vya Mwalimu Nyerere, Maonesho ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) Jengo la Wizara ya Fedha na Uchumi sio la kukosa kuingia. Mengi utajifunza na utapata maelekezo mbali mbali muhimu  kutoka kwa wafanyakazi walio na ujuzi na ukarimu. Hapo utajifunza  na kuelewa jinsi Wizara hii nyeti inavyofanya shughuli zake katika kuimarisha na kuboresha uchumi hapa nchini. Utapata maelekezo juu ya jinsi ya kutambua fedha Bandia, Utaelekezwa namna ya kufuatilia na kupata madai kutoka hazina, utapata ufafanuzi kuhusu bajeti ya serikali na mengi mengine.

Mapokezi utakutana na Da' Mary na Dada Ingiaheri Mduma ambaye ni aAfisa uhusiano na Msemaji Mkuu wa Wizra ya Fedha na Uchumi, hapo utafaidi ukarimu wa hali ya juu na maelekezo muhimu.

Afisa uhusiano, Wizara  ya Fedha na Uchumi,na Mesmaji Mkuu, Ingiahedi Mduma akitoa maelekezo kwa mwananchi aliyetembelea Wizara ya Fedha na Uchumi kwenye Maoenesho ya Kimataifa ya Biashara(Sabasaba) jijini Dar es Salaam jana.

Mtaalamu wa Uchumi, Idara ya Bajeti, Adamu Msumule akifafanua jambo kwa wananchi waliotembelea Jengo la Wizara hiyo jana.

Pia katika Jengo la Wizara ya Fedha kuna huduma za Kibenki kutoka Benki Kongwe nchini, Benki ya Posta. Hapo unaweza kuweka na kuchukua kiasa chochote cha fedha,. Pia huduma ya Western Union inapatikana.

Wananchi Mbali mbali wakipata maelezo kutoka kwa wafanyakaz wakarimu wawIWizara ya Fedha na uchumi. Picha zote na Victor Makinda
Reactions::

Mo Blog Inahujumiwa

TAARIFA YA MO BLOG KWA WADAU

MO BLOG INAPENDA KUWAFAHAMISHA WADAU NA WASOMAJI WA BLOG HII KUWA TUMESIKITISHWA
NA KUHUZUNISHWA NA TABIA INAYOENDELEA YA KUHUJUMIWA NA WAPINZANI WASIOPENDA
MAENDELEO YETU KWA SABABU ZAO BINAFSI.

KWA MUDA MREFU TUMEKUWA KATIKA HARAKATI NA MSTARI WA MBELE KUHAKIKISHA
TUNAWAHABARISHA, ELIMISHA NA KUJADILIANA NA WADAU MBALIMBALI WA BLOG HII BILA KUINGIA
UHURU WA WENGINE WALA KUKOSOA WENGINE, KWANI MAENDELEO YA KWELI YANATOKANA NA
KUJIAMINI.

KWA MANTIKI HII TUNAOWAMBA RADHI WADAU WETU KWA KUTOKUWEPO HEWANI KWA SAA
KADHAA LAKINI SASA MO BLOG IMERUDI NA ITAENDELEA KUWALETEA HABARI NA BURUDANI
MBALIMBALI NANYI MSISITE KUTUSHAURI NA KUTUONGOZA KWA MAWAZO YA KUJENGA.

IKIWA NI MARA KWA MARA TATIZO HILI LA KUPOTEA NA KUPOTEZA KAZI ZETU KUTOKEA KATIKA BLOG
YETU ,TUNAJIULIZA NI WAPI TUNAKOSEA AU KUHARIBU KATIKA UHABARISHAJI WETU WA HABARI NA
MATUKIO ,AU KUFANYA HIVI NI MAKOSA..?!!!

KWA KIFUPI MOBLOG INATEMBELEWA NA WATU 20,000 KWA SIKU NA HILI LINATUPA NGUVU
NA KUFAHAMU KUWA WADAU WETU WANARIDHISHWA NA KUPENDEZWA NA HABARI ZA KITAIFA,
KIMATAIFA, BIASHARA, MICHEZO, BURUDANI NA INTERVIEWS ZA WATU MAARUFU WANAOJULIKANA
NA WALE PIA WENYE VIPAJI WASIOJULIKANA.

WADAU HILI NI KOSA…???

KWA MASIKITIKO MAKUBWA TUNAPENDA KUWATAARIFU KUWA KAZI ZOTE ZA MWAKA HUU 2011
ZILIZOPENDWA NANYI WADAU NA NYINGINE ZIKITOKANA NA MCHANGO WA NINYI WADAU NA
WASOMAJI ZIMEPOTEA KWA LUGHA NYINGINE (ZIMEFUTWA/ZIMEPOTEZWA) KWA SABABU AMBAZO
ZINATUTIA SHAKA NA KUTUPA HISIA KUWA NI ZA KIPINZANI.

TUSINGEPENDA KUSEMA MENGI NA WALA KUTAJANA MAJINA ILI KWA WEMA KABISA NA HEKIMA
TUNAPENDA KUSISITIZA KUWA UPINZANI WA KUHARIBIANA SI MZURI NA HAUJENGI WALA KULETA
MAFANIKIO KWANI MWISHO WA UBAYA NI AIBU.

HAIPENDEZI KUONGEA HAYA YOTE HAPA ILA YAKIZIDI NI AFUENI YA MOYO NI KUONGEA NA KUSEMA
WAZI TUMECHOKA KUHUJUMIWA.

ASANTE KAKA MAKWAIYA KWA MSAADA WAKO, MKUBWA MICHUZI TUNAKUSHUKURU BILA
KUMSAHAU MZEE WA FULL SHANGWE NA WENGINE KWA MISAADA MBALIMBALI NA USHAURI
MLIOTUPA KWETU.

WADAU WA MOBLOG TUKO PAMOJA NATUTAENDELEA KULIJENGA TAIFA LETU KWA AMANI, UPENDO
NA MATUMAINI.

TUNAWAPENDA, TUNAWATHAMINI, TUNAWAHESHIMU NA TUTAFANYA KAZI PAMOJA NA TUTAFIKA

PALE TUNAPOKUSUDIA.

MUNGU IBARIKI MO BLOG NA WADAU WAKE WOTE.

Endelea kuperuzi MO BLOG www.mohammeddewji.com/blog
Reactions::

Mimi Na Mke Wangu; Ni Mechi Ndani Ya Mechi!



Ni ziada ya mapenzi!
Reactions::

Oscar Salathiel Kambona; Upande Wa Pili Wa Shilingi ( 2)

-Ziara mbili za ughaibuni zilizovunja urafiki wa Nyerere na Kambona

Na Maggid Mjengwa,


KUNA wakati nilimsikia Ahmad Rashid akitoa hoja bungeni. Wakati huo mbunge huyo wa CUF alikuwa kiongozi wa upinzani bungeni. Ahmad Rashid aliomba kambi ya upinzani bungeni ibadilishwe jina na badala yake iitwe kambi ya ushindani bungeni. Ni kwa vile neno ‘upinzani’ linatafsiriwa vibaya na wananchi. Spika Samwel Sitta alisimama na kutamka; “ Mtaendelea kuitwa hivyo hivyo kambi ya upinzani, kwa vile nyinyi ni watu wa kupingapinga tu!”



Na maneno haya ya Samwel Sitta yanatokana na historia yetu. Maana, haya ni makosa ya kihistoria yaliyofanywa na waliojenga msingi wa taifa letu. Na ndio tunayoyaona hata katika mfarakano wa miaka hamsini iliyopita kati ya Julius Nyerere na Oscar Kambona.


Na mara ile, mwaka 1965, TANU ilipoaachana na mfumo wa vyama vingi na kuasisi mfumo wa Chama kimoja Kambona alipata kutamka; ” Kwanini tupige marufuku ya vyama vingine vya siasa wakati tunajua wananchi walio wengi wanaipigia kura TANU?” Kambona akaongeza kusema; ” Bila shaka, umaarufu wa TANU utabaki kwa muda mrefu, lakini, je, pale umaarufu wa TANU utakapopungua, ina maana tuwe madikteta?” Alihoji Kambona.


Nimepata kukumbushia mara kadhaa, kuwa historia ni mwalimu mzuri. Na wanadamu hatupaswi kuwa vipofu wa historia yetu wenyewe. Kuifumbia macho historia yako ni kujiandalia njia ya kutumbukia korongoni, kwa kujitakia. Tunapoadhimisha miaka hamsini ya uhuru wa Tanganyika tuna lazima ya kuipitia na kuitafakari historia yetu. Kwa macho makavu na maangavu, tuangalie nyuma tulikotoka. Tuangalie tulipo sasa. Ndio, tufanye hivyo ili tuutafute mwelekeo mwema wa nchi yetu hata kwa miaka mingine hamsini ijayo.



Tuna maswali mengi ya kujiuliza, moja kuu ni hili; Je, ni nchi ya namna gani tutayotaka kuijenga na hata kuvirithisha vizazi vijavyo? Kwa maneno mengine; ni jamii gani tunayotaka kuijenga? Sisi wa ’ Kizazi Cha Azimio’ tulikuwa wadogo sana katika miaka kumi ya mwanzo ya uhuru na hata utekelezaji wa Azimio la Arusha. Nimezaliwa Ilala, Dar es Salaam, Machi 11, 1966.



Ndio, kuna mema mengi tuliyoyaona, lakini, tukitafakari sasa, kuna mabaya mengi pia tuliyoyashuhudia. Tuna wajibu wa kusimulia mema na mabaya hayo kwa manufaa ya Watanzania wa kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.


Kati ya kumbukumbu zangu mbaya za wakati huo ni jinsi tulivyowaona wazazi wetu wakiishi kwa hofu. Waliogopa kushutumu mamlaka hadharani na kwa sauti. Waliishutumu Serikali na hata kiongozi mkuu wa nchi kwa kunong’ona. Wazazi wetu walimwogopa hata mjumbe wa nyumba kumi.


Ni ukweli, kuwa kwa wakati ule, Serikali na chama tawala havikuwa na uvumilivu wa sauti za upinzani.


Na siku zote, mamlaka bila upinzani huzaa kiburi na majigambo. Huzaa hali ya kutokujali na kukosa usikivu. Taratibu, huzaa hali ya kujisikia u-bwana mkubwa. Hali hii ikiachwa ikaendelea, basi, husababisha madhara makubwa kwa nchi. Huleta hasara kubwa kwa nchi, kiuchumi na kijamii.


Juma la jana nilimalizia kwa kuandika, kuwa makala haya ni jaribio la kuvunja ukimya wa juu ya nini kilitokea takribani miaka hamsini iliyopita. Ni mmoja tu wa mfano , wa jinsi umma ulivyofichwa ukweli wa juu ya nini hasa kilitokea kikasababisha mfarakano wa waliopata kuwa viongozi wa mstari wa mbele kwenye harakati za kuanzishwa kwa TANU na kudai uhuru wa Tanganyika; Julius Kambarage Nyerere na Oscar Salathiel Kambona.



Kuna aliyesoma makala yangu ya juma la jana na kuniuliza; ” Maggid, hivi wewe huogopi?” Ni kweli, kama ningeandika haya mwaka 1976 nilipokuwa mtoto wa umri wa miaka kumi tu, basi, vyombo vya dola vingenishukia mithili ya mwewe anayekishukia kifaranga cha kuku. Sio tu mimi ningeswekwa rumande ya watoto, bali hata mama na baba yangu wangetikiswa na dola kwa ’ dhambi’ ya kumzaa mtoto mwenye fikra za ’ kipinzanipinzani ’ na ’ kihainihaini’. Mtoto ’ anayepingapinga’ tu!



Na hapa ndipo kwenye moja ya mapungufu makubwa ya waliojenga msingi wa taifa letu; kuchukia wenye kufikiri tofauti na watawala. Na zaidi kuwachukia wenye ’ akili’ ya kufikiri na kuutumia vema welewa wao- hostility towards execelency. Si tunajua, kuwa utotoni tulisikia kuna maadui wa nchi wa aina mbili; maadui wa nje na wa ndani. Wapinzani ama wenye kufikiri tofauti ndimo walimowekwa wanaoitwa ’maadui wa ndani!’



Niseme tu, mfulilizo wa makala haya ni moja ya makala zangu muhimu tangu nianze kushika kalamu na kuandika makala magazetini. Na naandika nikiwa sina hata chembe ya hofu. Ni kwa sababu moja kuu; kuwa yanahusu historia yetu na mustakabali wa nchi yetu. Sote tuna wajibu wa kuandika historia yetu.



Hii ni nchi yetu. Hatuna sababu za kuionea aibu historia yetu, badala yake, tujivunie, kuwa tuna historia. Na ni unyonge na utumwa kusubiri wasomi kutoka Marekani na Ulaya waje kutafiti na kutuandikia historia yetu. Historia yako isimulie mwenyewe. Hivyo basi, tuna wajibu wa kuifanya kazi hiyo. historia itusaidie kutukumbusha machungu na furaha ya tuliyoyapitia kama taifa. Si kwa kuandika tu, hata kwa kusimulia machache tuliyoyashuhudia.



Niliahidi kuchambua zaidi juu ya marafiki hawa watatu; Kambona, Nyerere na Kawawa. Nitafanya hivyo sasa.


Naam. Julius na Oscar walikuwa viongozi vijana sana katika Tanganyika huru ya wakati huo. Ikumbukwe, wakati tukipata uhuru, Nyerere alikuwa na miaka 39 na Oscar alikuwa na miaka 36. Hawa walikuwa ni vijana waliokabidhiwa dhamana kubwa ya kuingoza nchi kubwa ya Tanganyika. Naamini, walikuwa ni wenye dhamira njema kwa taifa hili; Julius, Oscar, Rashid na wenzao wengine katika TANU.

Ukweli unabaki, kuwa Oscar Kambona hakuikimbia nchi yake kwa kashfa ya kuiba fedha ya Serikali au ufisadi mwingine. Na kwa utafiti mdogo tu niliofanya, nilichobaini, ni ukweli kuwa marafiki hawa wawili; Oscar na Julius walikuwa na mgongano wa tofauti ya kimaono ya kisiasa yaliyoathiri hata urafiki wao.

Maana, haiyumkini Kambona aliyeaminiwa na Nyerere akaja kuwa Katibu Mkuu wa kwanza wa TANU, akawa Waziri wa kwanza wa Elimu wa Tanganyika huru, akaja kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani na hata kwa wakati mmoja kushika wizara mbili; Waziri wa Ulinzi na Waziri wa Mambo ya Nje. Kwamba, aje tena baadae kutuhumiwa uhaini na hata kushukiwa uraia wake.



Ndio, kwangu mimi, ya Kambona na Nyerere ilihusu zaidi mgongano wa tofauti za kimaono ya kisiasa . Na ukiingia kwa undani kwenye maandiko na simulizi utaupata ushahidi wa haya. Na kwa hakika, ili siasa ya nchi istawi, basi, inahitaji uwepo wa migongano ya kifikra. Hivyo basi, siasa ni migongano ya kifikra yenye kuhitaji majadiliano endelevu.



Tunaona, kuwa migongano ya kifikra kati ya Oscar na Julius ilianza kuonekana dhahiri katika ziara mbili walizozifanya kwa pamoja katika mataifa mawili tofauti. Ziara ya Marekani mwaka 1963 na ziara ya Uchina mwaka 1965. Na hapo katikati kuna jambo lililoopelekea uwepo wa mahusiano ya mashaka kati ya Julius na Oscar. Ni uasi wa jeshi wa Janauri 20, 1964.



Uasi ule ulipelekea Nyerere na Kawawa waende mafichoni, inasimuliwa walijihifadhi eneo la Kigamboni. Mjini alibaki Oscar Kambona aliyeshiriki kikamilifu kuwatuliza wanajeshi wale. Kimsingi, katika kipindi kile cha maasi, Kambona, kama angetaka, alikuwa na fursa ya kutwaa mamlaka ya nchi akisaidiwa na jeshi. Inasemwa, kuwa akiwa Waziri wa Ulinzi, Kambona alikubalika sana jeshini.



Baada ya ziara ya Marekani akiwa na Oscar Kambona mwaka 1963 ambako Rais John Kennedy alimsifia sana Nyerere kwa kuonyesha uwezo wa kiungozi , miaka miwili baadae, mwaka 1965, Nyerere na msafara wake akiwamo Oscar Kambona walikwenda China kwa mara ya kwanza na kulakiwa na Mwenyekiti Mao Tse Tung. Nyerere akiwa kwenye gari la wazi na mwenyeji wake Mao , alishangiliwa na Wachina wapatao milioni moja waliojipanga barabarani.


Pale Ilala tulikoishi, nakumbuka nikiwa na umri wa miaka sita tu, usiku mmoja pale viwanja vya shule ya msingi Boma tuliangalia sinema ya ziara ya Julius Nyerere Uchina . Nyerere aliiona China na alivutiwa sana. ” What we have seen in China is relevant to us”. Nimemsikia Nyerere akiongea hayo kwenye kipande cha filamu ya zamani kilichopo mtandaoni . ” Ana maana, walichokiona China kinaweza kikafanyika kwetu. Na Julius alianza kwa kubadilisha hata staili yake ya mavazi, yakafanana na ya Mwenyekiti Mao, na wengine katika TANU wakamwiga.


Ni nini kilitokea kwenye Mkutano wa TANU wa Januari, mwaka 1967 na kabla ya hapo. Mkutano uliopelekea kumalizika kabisa kwa urafiki wa Nyerere na Kambona. Fuatilia toleo lijalo.
Reactions::

Wednesday, June 29, 2011

Janga La Mgao Wa Umeme; Makamba Amkingia Kifua Ngeleja

MWENYEKITI wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, Januari Makamba, amesema siyo sahihi kumlaumu Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), kwa tatizo la umeme nchini.Akizungumza mjini hapa jana, Makamba alisema sekta ya umeme nchini imepita vipindi vitatu tofauti; kabla ya miaka ya 90 na baada kuanzia mwaka 1996 hadi mwaka 2000, hivyo suala hilo limekuwa na historia.
“Kimsingi siyo sahihi kumlaumu waziri wala Tanesco yenyewe, matatizo hayo yalikuwapo na waziri ameyakuta. Cha msingi kama Taifa, tushikamane na tuone tatizo hilo kama janga na tuungane kupambana nalo,” alisema Makamba.
Akifafanua historia hiyo, Makamba alisema uendelezaji umeme nchini kabla ya mwaka 1996, Tanesco ilikuwa ikijiendesha kwa ufanisi mkubwa ikiwa inamilikiwa na serikali kwa asilimia zote.
“Kipindi kilichofuata ni mwaka 1997 hadi 2006, Tanesco iliwekwa katika orodha ya mashirika yanayotakiwa kubinafsishwa, lakini hakuna hatua iliyochukulia hadi mwaka 2006 uamuzi huo ulipobatilishwa,” alisema Makamba na kuongeza:
“Wakati wote huo ikisubiri kubinafsishwa, hakuna uwekezaji uliofanyika katika shirika hilo wakati uchumi wa taifa ulikuwa unaendelea kukua kwa kasi kubwa kufikia kiwango cha asilimia saba na mahitaji ya umeme, yakiongezeka maradufu.”
Kwa mujibu wa Makamba, baadhi ya miradi iliyotokana na uwekezaji mkubwa ni migodi ya madini na kampuni za simu, lakini wakati huohuo taifa lilikumbwa na ukame katika vyanzo vyake vya kuzalisha umeme wa maji, ikiwamo Mtera na Kidatu na taifa likaingia gizani.
Alisema mipango mingi iliyobuniwa ianze kutekelezwa 2008 ambayo ilitarajiwa itakapokamilika ingezalisha megawati 645, hadi sasa ni miwili ndiyo imefankiwa; Ubungo (Megawati 100) na Tegeta (Megawati 45).
unatarajiwa kukamilishwa na mkopo kutoka China wa dola 400 milioni za Marekani.
Uwezo wa kitaifa hivi sasa wa kuzalisha umeme kama vyanzo vyote vya kuzalisha umeme vitafanya kazi ni megwati 1,100, ambacho Makamba alisema hakitoshi wateja wanaokadiriwa kufikia milioni sasa.

Kwa mujibu wa Makamba, tatizo la umeme litakwisha iwapo serikali itaweka juhudi za makusudi kuwekeza katika uzalishaji umeme na kuweka kando tofauti za kisiasa.
Alisema, iwapo juhudi zitafanyika haraka za kufanya uwekezaji mkubwa katika uzalishaji wa umeme kitaifa, kwa kutumia vyanzo vingine mbali na maji yanayozalisha asilimia 55 ya umeme wote nchini, taifa litaondokana na uhaba wa umeme.Chanzo; Gazeti Mwananchi
Reactions::

Mwanamke Wa kwanza Kuongoza IMF

Waziri wa Fedha wa Ufaransa Christine Lagarde ameteuliwa kuwa mkurugenzi mkuu wa shirika la fedha duniani IMF.    Waziri wa Fedha wa Ufaransa Christine Lagarde ameteuliwa kuwa mkurugenzi mkuu wa shirika la fedha duniani IMF.Kufuatia uteuzi huo Ufaransa itakuwa imeshikilia kiti hicho kwa miaka 26 kati ya miaka 33 iliyopita.
Christine Lagarde mwenye umri wa miaka 55, alikuwa mwanamke wa kwanza kuteuliwa waziri wa fedha katika muugano wa nchi saba zilizostawi maarufu kama G-7.
Lagade anatarajiwa kujiuzulu kutoka serikali ya Ufaransa ili kuandikisha historia ya kuwa mwanamke wa kwanza kuwahi kuongoza shirika la fedha duniani IMF.
Uteuzi wake umefuatia kujiuzulu wa mfaransa mwenzake Dominique Strauss Kahn, baada ya kukabiliwa na kashfa ya ubakaji.
Sio wengi walioshangazwa na uteuzi wa wakili huyo wa zamani ambaye ana sifa nzuri kote duniani.
Amekuwa msuluhishi wa matatizo mengi ya kiuchumi yanayokumba mataifa kadhaa barani ulaya katika miaka ya hivi karibuni.
Kabla ya kuteuliwa kwake alikuwa ameungwa mkono na China na India na hivyo kuteuliwa kwake kama mkurugenzi mkuu wa shirika hilo la fedha duniani ilikuwa jambo lililotarajiwa.
Kuna maelewano ambayo hayajanakiliwa kuwa raia wa mataifa ya bara ulaya pekee ndio wanaopaswa kuteuliwa kuhudumu kama mkurugenzi mkuu wa IMF huku raia wa marekani wakipewa nafasi za kuongoza benki kuu ya dunia.
Mataifa yaliostawi yanataka kupewa nafasi kuu katika siasa za dunia, lakini huu ni wakati mgumu kwa mataifa ya ulaya huku mzozo wa kiuchumi wa Ugiriki ukitishia kuathiri mataifa mengine katika kanda hiyo.
Muungano wa ulaya na IMF zimeishurutisha serikali ya Ugiriki kupunguza matumizi yake ili kuendelea kupata msaada kutoka kwao.
Lagarde amekuwa katika mstari wa mbele kujaribu kutatua matatizo hayo ya nchi wanachama wa EU.BBC
   
Reactions::

Madaktari Na Wauguzi Watakiwa Kufanya Kazi Kwa Bidii Ili Kuokoa Maisha Ya Wagonjwa; Asema Mama Salma

Na. Aron Msigwa – MAELEZO.
, Moroni, COMORO.
Madaktari na wauguzi wametakiwa kufanya kazi kwa bidii na kujituma ili kuokoa maisha ya wagonjwa wanaowahudumia.
Wito huo umetolewa leo na Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) alipotembelea wodi ya watoto katika hospitali ya Rufaa ya El Maarouf iliyoko mjini Moroni nchini Comoro kuona namna huduma za afya zinavyotolewa kufuatia mwaliko wa mke wa Rais wa nchi hiyo Bi. Hadija Aboubacar Ikililoi Dhoinine.
Amesema wataalam wa Afya wana dhamana kubwa ya maisha ya wagonjwa wanaowahudumia huku akisisitiza umuhimu wa madaktari na wauguzi kutoa huduma za afya kwa watoto wadogo kutolewe kwa uangalifu, umakini na kwa kuzingatia umri walionao.
“Napenda kusisitiza kuwa huduma za afya kwa watoto ni za msingi sana katika taifa lolote lile,ukiboresha afya za watoto ina maana unakuwa na taifa lenye afya bora hali inayopelekea kuwa na taifa lenye viongozi bora wa baadaye”
Amefafanua kuwa nchini Tanzania kupitia Taasisi anayoiongoza ya Wanawake na Maendeleo(WAMA) suala la afya kwa watoto ni moja ya jukumu linalopewa kipaumbele na kusifu juhudi zinazofanyika kuwaokoa watoto walio chini ya miaka mitaano nchini Comoro.
Ameongeza kuwa nchini Tanzania taasisi ya WAMA kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa sekta ya afya inashiriki kikamilifu katika kutoa elimu kwa wanawake na watoto dhidi ya maambukizi ya Virusi vya Ukimwi na kuhakikisha kuwa watoto wadogo wanaozaliwa wanakuwa salama.
“ Lazima tukubali kuwa eneo la watoto ni nyeti sana na tuna kila sababu ya kufanya kila juhudi kuhakikisha kuwa watoto wanaozaliwa hawafi mara tu baada ya kuzaliwa huku tukitekeleza malengo ya milenia ambayo nchi zetu zinayatekeleza yakiwemo upunguzaji wa vifo vya akina mama na watoto pamoja na mapambano dhidi ya ugonjwa wa Ukimwi” amesema mama Salma.
Aidha amefafanua kuwa juhudi zaidi zinahitajika katika nchi zinazoendelea kuhakikisha kuwa watoto wadogo wanaozaliwa wanalindwa kwa kuwapatia mahitaji muhimu ya kiafya ikiwemo uzuiaji wa vifo vya watoto wadogo na utoaji wa elimu kwa wanawake kuhusu uzazi salama na uzingatiaji wa matumizi ya vituo vya afya pale wanapoona dalili hatarishi kwa watoto wao.
Kwa upande wake mke wa Rais wa Comoro Bi. Hadija Aboubacar Ikililoi Dhoinine amefurahishwa na ziara ya mama Salma Kikwete hospitalini hapo na kueleza kuwa ujio wake nchini humo utaendeleza zaidi uhusiano wa muda mrefu uliokuwepo kati ya Tanzania na Comoro huku akibainisha kuwa sekta ya afya katika nchi yake inaendelea kupiga hatua licha ya kukabiriwa na vikwazo mbalimbali.
Naye mganga mkuu wa wodi ya watoto katika hospitali hiyo Dkt. Said Hassani amesema kuwa idara yake itaendelea kufanya kazi kwa bidii ili kuboresha afya za watoto na kupunguza vifo vya watoto wanaozaliwa na wale walio chini ya miaka mitano huku akiomba uhusiano kati ya nchi ya Tanzania na Comoro katika sekta ya afya uendelee kudumishwa zaidi.
Reactions::

Nape Azidi 'Kukanyaga Mafuta' CCM




1. MAMIA  ya wananchi wakiwa katika mkutano wa hadhara uliofanyika mjini Mtwara 28/6.2011
 
2. Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, CCM, Nape Nnauye akijadiliana jambo na Mbunge wa Lindi mjini, Hasnain Mohammed Murj wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika  mjini Mtwara  28/6/2011
 
3. Aliyekuwa mwanachama wa CUF na mgombea udiwani kwa tiketi ya chama hicho katika uchaguzi mkuu uliopita, Mohamed Chiungulumana akikabidhi kadi ya chama hicho kwa Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye alipotangaza kurejea CCM kwenye mkutano uliofanyika 28/6/2011 mjini Mtwara. Jumla ya wanachama 154  wa CUF walijiunga na CCM katika mkutano huo.Kuhsoto ni Katibu wa NEC Oganaizesheni, Asha Abdallah Juma. Picha zote: Bashir Nkoromo
 
Reactions::

" Shangazi Hujambo?"

Katibu wa NEC, Oganaizesheni CCM, Asha Abdallah Juma akizungumza na mtoto  Fatma Mohammed, alipomkuta kwenye mkutano wa hadhara wa CCM uliofanyika kijiji cha Mpapura Mtwara vijijini. Picha: Bashir Nkoromo.
 
Reactions::

Wazee Wanafuatilia Mkutano Wa Nape

Wazee wa Kijiji cha Mpapura, Mtwara Vijijini, Abdurahmani Dadi (70) na Dadi Hamis (65) wakifuatilia kwa makini , Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara katika kijiji hicho 28/6/2011. Picha: Bashir Nkoromo.
 
Reactions::

EASTERN AND SOUTHERN AFRICA CARGO LIMITED- UK

We are an import/export company based in the United Kingdom with global dealings. We offer specific services to suit each individual client.


Whether you require a single service or an annual requirement,ESAC LTD will treat you with care, consideration and most of all the best solution for your requirements. We pride ourselves in our service and welcome any job regardless of size.


ESAC LTD is proud to announce this service for those who wish to send urgent consignments or smaller items,Quick goods to East Africa and many other destinations.

*OUR AIRFREIGHT SERVICES ARE WORLWIDE £2.70 PER KILO £38.00 Customs Entry Fees. Our minimum weight is 100KG.


We ship all types of cargo to Africa at subdued rates, i.e. containers, trucks, cars, machines etc. we also sell used vehicles & machinery from UK.
RORO


Saloon & 4X4 TO DAR OR MOMBASA

TRUCKS from $81.50 per cubic metre
TRUCKS from $81.50 per cubic metre

CONTAINER

20ft CONTAINER TO DAR



40ft CONTAINER TO MOMBASA
40ft CONTAINER TO DAR, TANGA & ZANZIBAR

Bill of Lading will be processed in 3-5 working days if you pay full amount ;"GAURANTEE"


Also we provide the service to West frica, please ring us to get a quotation.


Note: For our customers who are outside UK, but would like to buy fromUK, we can buy to match your specifications weather is cars, trucks, machinery, hospital equipments and other goods, please do not hesitate to contact us. We will buy and ship your good/s timely and as per your requirements.

At Eastern and Southern Africa Cargo LTD, we aim to: -
* Put the Customer First *

*Like many other international business our price may vary due exchange rates and currency fluctuation*
* Provide High Quality Service*




--


--

Regards,

CEO: Bernard Chisumo
Eastern & Southern Africa Cargo Limited (ESAC)
(Exporters & Importers )
Tel No: +44 783 369 2695, +44 0148 221 4949 (North England - HQ)
Tel No: + 44 118 954 5890, +44 79000 43224 (South England office)
132 Victor Street, HULL, HU9 2EY- East Yorkshire
REG NO:07609023. VAT NO:113 999 585
Reactions::

Mapacha Watatu!

Reactions::

Tuesday, June 28, 2011

Mama Salma Kikwete Yuko Comoro





1- Mke wa Rais mama Salma Kikwete(nguo nyekundu) akipata ufafanuzi wa vifaa mbalimbali vya kutengenezea simu katika moja ya darasa la kituo cha mafunzo EMDAD kilichopo mjini Moroni nchini Comoro, June 28/2011.

Picha no 2 na 4. Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya WAMA mama Salma Kikwete(aliyevaa baibui) akiwa na mke wa Rais wa Comoro mama Hadija Aboubacar Ikililoi Dhoinine (kulia) wakipata maelezo kutoka kwa waziri wa afya wa Comoro Mwanafuraha Mohammed (wa tatu kutoka kulia) kuhusu mtoto ambaye yuko chini ya uangalizi wa madaktari baada ya kuzaliwa katika Hospitali ya Rufaa ya El Maarouf mjini Moroni Comoro - June 28/2011.

Picha no 3 - Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) akiangalia aina ya samaki ambaye amehifadhiwa katika makumbusho ya Taifa mjini Moroni, Comoro. Samaki huyo yuko katika orodha ya samaki wasiotakiwa kuvuliwa nchini humo, (mwenye nguo za kijani) ni mwenyeji  wake mke wa Rais wa Comoro mama Hadija Aboubacar Ikililoi Dhoinine - June 28/2011.

Picha no 5 - Rais wa Kikundi cha Mtandao wa Wanawake na Maendeleo cha Moroni, Comoro Bi. Jacqueline Assoumani (kushoto) akitoa maelezo kwa Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mama Salma Kikwete (katikati) alipotembelea na kuiangalia shughuli mbalimbali za kikundi hicho, kushoto kwake ni mke wa Rais wa Comoro mama Hadija Aboubacar Ikililoi Dhoinine. June 28/2011 . Picha zote na Mwanakombo Jumaa, MAELEZO.
Reactions::

Mdau Anauliza; " Mliokulia Enzi Za Mwalimu, Je Haya Ni Ya Kweli?"

Anony wa Jun 28th; 02:10:00 inawezekana ni kweli wachangiaji wengi ni wale wa 1980's and 1990's. Mimi binafsi nimezaliwa 1979 na sijui mengi kuhusu maisha ya wakati wa utawala wa Nyerere. Naomba nikuulize maswali kadhaa kuhusu nyerere ili niweze kufanya utafiti zaidi.

Jee ni kweli kwamba wanafunzi wengi wa shule za dar-es-salaam walikuwa wakikaa sakafuni na wakiuza ubuyu na kalimati za mwalimu?

Jee. ni kweli mlikuwa mkipanga foleni kwa masaa kadhaa mkusubiri gari la ugawaji?

Jee ni kweli mlipigia mswaki jivu na mkaa?

Jee ni kweli mlifua nguo kwa kutumia harita?

Jee ni kweli mlikula ugali wa njano wa mahindi ya kutoma marekani?

Jee ni kweli kwamba watu walikuwa wakivaa midabwada? (au nguo zenye viraka?)

Jee ni kweli ulikuwa ukimtembelea ndugu yako darisalama ni lazima balozi wa nyumba kumi ajulishwe madhumuni ya ujio wako na utakaa siku ngapi?

Jee ni kweli kwamba ulikuwa ukikamatwa na kilo 10 za sukari unakamatwa kwa ulanguzi na uhujumu uchumi?

Jee ni kweli ulikuwa umekaa kijiweni basi unakamatwa na askari wa nguvu kazi na unashitakiwa kwa uzurulaji na uzembe na unapelekwa sehemu yoyote ya nchi?

Jee ni kweli kwamba safari ya kutoka dar-es-salaam kwenda bagamoyo ilichukua kutwa nzima na wengine walisafiri safari hiyo kwa kupanda magari ya mizigo? (lorries)

Jee ni kweli kwamba mlivaa viatu vya matairi ya gari? (katambuga)

Jee ni kweli kwamba Tanzania bara haikuwa na TV station wakati Zaizibar walikuwa nayo?

Jee ni kweli kwamba demokrasia ya wakati huo ilikuwa unachagua rais au kivuli kwa kura ya ndiyo au hapana?

Jee ni kweli wakulima wakubwa walipokonywa mashamba yao na yakafanywa kuwa mashamba ya ushirika?

Jee ni kweli kwamba kila familia(kaya) iliwahi kupewa kadi ya ugawaji ambayo inaamua kwamba unaruhusiwa kununua kilo kadhaa za mchele/sukari/ngano?

Naomba tuu unielimishe katika maswali yangu haya.
Reactions::

Lowassa Katika Viwanja Vya Bunge Leo

Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa akiteta na Katibu Mkuu katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Peniel Lymo kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Reactions::

Matunda..Mchanganyiko

...Tayari kwa kuliwa. Leo asubuhi katika viwanja vya maonesho ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) jijini Dar es Salaam. Pakiti moja shiliki 1000.Picha na Victor Makinda.
Reactions::

Serikali Ya Japani Yatoa Msaada Wa Mafuta Ya Kupikia

Balozi wa Japani nchini Hiroshi Kanagawa, akimakabidhi msaada wa mafuta ya kupikia katibu mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Mbarak Abdul Wakil, leo asubuhi Bandarini Dar es Salaam. Msaada huo wa mafuta ya kupikia umetolea na serikali ya Japani kwa Serikali ya Tanzania kwa ajili ya kuwasaidia wakimbizi waliopo katika kambi mbali mbali nchini.

Balozi wa Japan Hiroshi Kanagawa akielekeza jambo kwa mwakilishi wa shirika la Chakula la Umoja wa Mataifa (WFP) Ronald Simanda wakati wa makabidhiano ya msaada huo. Picha zote na Victor Makinda
Reactions::

Jengeni Tabia Ya Kuandika Wosia Wenu Mkiwa Hai, Asema Sitta

Serikali inawashauri wananchi wote kujenga tabia ya kuandika wosia wakati wa uhai wao ili kuepusha usumbufu unaoweza kutokea wakati wa kufuatilia kesi za mirathi na kusababisha watoto wao kuishi maisha ya taabu na kuongeza wimbi la watoto waishio katika mazingira magumu.
Akijibu swali kwa niaba ya waziri wa Katiba na Sheria, Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta alisema masuala ya mirathi nchini hutawaliwa na sheria tatu. Alizitaja sheria hizo kuwa ni za kimila ambazo hutumika ikiwa marehemu aliishi kwa kufuata mila na desturi za kabila lake, sheria ya kiislamu ambayo hutumika ikiwa marehemu alikuwa mfuasi wa dini hiyo na sheria ya Urithi ya India ya mwa 1865 iliyopokelewa na mahakama za Tanganyika na ambayo hutumika ikiwa marehemu hakuwa muumini wa dini ya kiislamu au hakuwa akifuata mila na desturi za kabila lake.
Alisema serikali haina mamlaka ya kubatilisha sheria za kidini hata kama zitaonekana kuwa zina mwelekeo wa ukandamizaji. Kwa upande wa sheria za kimila Mheshimiwa Sitta alisema mahakama zina uwezo wa kuzitangaza sheria hizo kuwa ni batili endapo zitakuwa zinakiuka misingi ya haki iliyomo katika Katiba au sheria za nchi.
Alisema katiba ya nchi ni sheria mama na haiko chini ya mila kwa kuwa ndani ya katiba misingi ya kuheshimu dini imewekwa. Aliongeza kuwa katiba imetoa uhuru wa kila mmoja kuwa na dini yake.
Mheshimiwa Sitta amewatahadharisha walio katika ndoa wakiwa na dini tofauti kuwa masharti ya mirathi katika dini ya kiislamu ndiyo yatakayotumika wakati wa kudai mirathi.
Mheshimiwa Sitta alisema suala la mirathi litaendelea kuwa na utata kwa kuwa bado tunatawaliwa na mfumo dume ambao si mzuri hivyo wananchi wanapaswa kuendelea kuelimishwa ili kuondokana na mfume dume.
Reactions::

Match Your Personality, Taste And Style With INTERIOR DECOS

And here we are; http://www.interiordecos.com
Reactions::

Aliyekuwa Rais Wa Zambia Chiluba Azikwa

Marehemu Fredrick Chiluba na mkewe Regina mjini Lusaka       
Aliyekuwa Rais wa Zambia Frederick Chiluba amezikwa kwenye mji mkuu, Lusaka, kufuatia kifo chake wiki moja iliyopita.
Mamia ya waombolezaji, walioongozwa na Rais Rupiah Banda, walihudhuria mazishi hayo.
Bw Chiluba alifariki dunia nyumbani kwake mwishoni mwa juma- sababu ya kifo chake hakijtangazwa kwa umma mpaka sasa.
Aliiongoza Zambia kwenye demokrasia kwa kuanzisha vyama vingi mwaka 1991, lakini urais wake uligubikwa na madai ya rushwa.
Mwandishi wa BBC Mutuna Chanda mjini Lusaka alisema Wazambia wengi wanaamini udhaifu wa Bw Chiluba usiangaliwe sana na badala yake akumbukwe kwa kumaliza utawala wa chama kimoja.
Amezikwa pembeni mwa aliyekuwa Rais wa nchi hiyo Levy Mwanawasa, katika makaburi maalum kwa ajili ya Marais.
Bw Mwanawasa, aliyemrithi Bw Chiluba, alifariki dunia mwaka 2008.
Maelfu ya watu walishuhudia mazishi ya Bw Chiluba kupitia televisheni ya taifa na kwenye skrini kubwa ziliozwekwa nchini kote.
Viongozi wakuu kutoka nchi za kigeni waliohudhuria mazishi hayo ni Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Jospeh Kabila na waziri mkuu wa Zimbabwe Morgan Tsvangirai.BBC
Reactions::