Subscribe:

Monday, February 06, 2012

Kama Socrates Angekuwepo Kwenye Mkusanyiko Huu !

Ndugu zangu,
Mwenye hekima ni  yule anayetambua kuwa hajui. Pichani ni leo jioni. Ni tukio la ajali ya magari mawili kukwaruzana kwenye makutano ya Mtaa Livingstone na Mkunguni eneo la Kariakoo.  Ajali hii niliishuhudia kwa macho yangu, maana,  nilisimama kando ya eneo hilo nikinywa maji ya madafu.

Kwanza madereva walishuka na kuanza kulaumiana. Kila mmoja anamwona mwenziye ndiye mwenye kosa. Wakafika wapiti njia wengine wawili.  Na ndani ya dakika tatu, kundi kubwa likakusanyika hapo.  Hapo kukawepo na wajuaji wa sheria za barabarani. Wengine wakajitokeza kuwa mahakimu wa shauri, na mashahidi pia wakapatikana, hata wale ambao hawakuwepo kabisa wakati tukio likitokea.

Inanikumbusha mwanafalsafa Socrates wa Uyunani ya Kale. Socrates alipokuwa akichipukia kama mwanafalsafa katika mji wa Athens alikumbana na upinzani mkubwa. Maana, Athens ilikuwa na Masophist walioaminika kuwa walijua mengi.

Ndio hao waliotafsiri mambo ikiwamo sheria pia. Ndio hao waliodhaniwa kuwa ni wajuzi wa kutunga mashairi pia. Ndio walioaminika kuwa waliujua ukweli. Lakini, kwa masophisti, ukweli ulikuwa ni relative. Kwao wao, ukweli ulikuwa ni ukweli kama ukweli una maslahi kwao. Hivyo basi, jambo ambalo lilisemwa kuwa ni ukweli leo, kesho laweza kuwa ni uongo kulingana na mazingira ya wakati huo.

Socrates aliona jinsi vijana wa Athens walivyokuwa wakipotoshwa na masophisti.  Akataka kuifanya kazi ya kifalsafa ya kuwatoa gizani watu wa Athens. Maana, alibaini wale alioambiwa kuwa ni magwiji wa sheria katika Athens hawakuwa na maarifa hata ya misingi ya sheria. Na wale alioambiwa kuwa ni magwiji wa kutunga mashairi katika Athens nzima, Socrates alibaini kuwa hawakujua hata  misingi ya kutunga beti za mashairi.

Unafanyaje basi kuwageuza watu waliokuwa wakiamini katika walichokiamini?  Kwamba Socrates ni nani kuwaambia  watu wa Athens kuwa wale waliodhani kuwa wanajua hawakuwa na walijualo.

Na kama Socrates angekuwepo kwenye mkusanyiko huu wa watu hapo Mtaa Livingstone na Mkunguni sijui  angeanzia wapi kuwaambia  wanaodhani kuwa wana maarifa ya  sheria za barabarani na hata kujivalisha  majukumu ya  kuwa mahakimu na mawakili , kwamba , kwa kuanzia, kuwa mkusanyiko huo ni wa kimakosa.

Wote hao pichani hawakupaswa kuwa hapo, maana ,  si tu ni  katikati ya barabara, bali  wameingilia kazi ya trafiki wa barabarani na pengine   hawajui hata misingi ya sheria, ikiwamo sheria za barabarani!
Maggid Mjengwa,
Dar es Salaam
Reactions::

Kuna Wanaume Wanaoyaogopa Maji Ya Madafu, Wanaogopa Kuvaa Misuli!



Ni imani potofu. Kuna wanaume wanapotoka bara wanaonywa, kuwa ukifika Dar es salaam usinywe maji ya madafu, utaota mabusha na utalazimika kuvaa msuli kama wafanyavyo wanaume wa Pwani. Si kweli. Maji ya madafu hayaoteshi mabusha. Na msuli ni vazi zuri tu kwa mwanamme. Akina Nchimbi wanahangaika bure.
Msuli ndio ungefanywa kuwa vazi la taifa. Ingependeza kwa mwanamke kupiga kitenge na mwanamme msuli! Pichani nakunywa maji ya madafu mtaa Mkunguni , Kariakoo leo jioni huku nikipata mawili matatu yenye hekima kutoka kwa mwuuza madafu, Mzee Yusuf wa Kibada, Kigamboni ' Kwa Magufuli!'.
Reactions::

Sumry Hii!

Nimeikuta gari hii maeneo ya kitwiru- Iringa likiwa safarini ,Mtazamo wangu kuwa  Gari hili linaweza fika safarini  ila ni kwa kuchelewa  usafiri huu unafanana na usafiri ambao tunatumia watanzania kutufikisha kwenye kilele cha maisha bora je tutafika.
Mdau wa Mjengwa Blog Iringa


  
Reactions::

VILLA SQUAD, SIMBA ZAINGIZA MIL 30/-

Release No. 017
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Februari 6, 2012
 

Mechi namba 107 ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Villa Squad na Simba iliyochezwa Februari 4 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 30,017,000.
 
Watazamaji waliokata tiketi kushuhudia mechi hiyo ni 8,698 ambapo kiingilio kilikuwa sh. 3,000 kwa viti vya bluu na kijani, sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, sh. 10,000 kwa VIP C na B na sh. 15,000 VIP A.
 
Baada ya kuondoa asilimia 18 ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) ambayo ni sh. 4,578,864.41 fedha zilizobaki zilikuwa sh. 25,438,135.59. Gharama za awali za mechi zilikuwa nauli ya ndani kwa waamuzi sh. 10,000, nauli ya ndani kwa kamishna wa mchezo sh. 10,000.
 
Posho ya kujikimu kwa mwamuzi wa akiba sh. 30,000, gharama za tiketi sh. 3,960,000, umeme sh. 300,000, usafi na ulinzi kwa uwanja sh. 2,350,000 na Wachina (Beijing Construction) sh. 2,000,000. Nyingine ni Jichangie ambayo ni sh. 200 kwa kila tiketi; kila klabu ilipata sh. 608,860 wakati Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) kilipata sh. 521,880.
 
Mgawo baada ya gharama za awali; uwanja na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kila moja ilipata sh. 1,503,853.56, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 751,926.78, gharama za mechi sh. 1,503,853.56, Baraza la Michezo la Taifa (BMT) sh. 150,385.36, DRFA sh. 601,541.42 na kila klabu ilipata sh. 4,511,560.68. 
 
MUJUNI KUPIGA KIPENGA RWANDA
Mwamuzi Israel Mujuni wa Tanzania ameteuliwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) kuchezesha mechi ya marudiano ya raundi ya mchujo ya Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya APR ya Rwanda na Tusker ya Kenya itakayochezwa jijini Kigali kati ya Machi 2, 3 na 4 mwaka huu.
 
Mujuni atasaidiwa na Samuel Mpenzu na Khamis Maswa kutoka Tanzania wakati mwamuzi wa akiba katika mechi hiyo namba 18 atakuwa Louis Hakizimana wa Rwanda.
 
Kamishna wa mchezo huo atakuwa Aboubacar Nkejimana kutoka Burundi.
 
Nayo Mafunzo ya Zanzibar katika mechi yake ya kwanza katika raundi ya mchujo ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya Muculmana de Maputo ya Msumbiji itakayofanyika mjini Zanzibar kati ya Februari 17, 18 na 19 mwaka huu itachezeshwa na waamuzi kutoka Shelisheli.
 
Bernard Camille ndiye atakayekuwa mwamuzi wa kati huku akisaidiwa na Steve Marie na Gilbert Lista. Mwamuzi wa akiba katika mechi hiyo namba 27 atakuwa Ramadhan Ibada wa Tanzania wakati Kamishna atakuwa Ali Waiswa kutoka Uganda.
 
Kwa mujibu wa CAF, timu 13 bora zenyewe zimeingia moja katika raundi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
 
Timu hizo ni Coton Sport (Cameroon), El Ahly (Misri), Djoliba (Mali), Stade Malien (Mali), MAS (Morocco), Raja (Morocco), Sunshine Stars (Nigeria), TP Mazembe (Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC), El Hilal (Sudan), El Merrikh (Sudan), EST (Tunisia), ESS (Tunisia) na Dynamos (Zimbabwe).
 
VIINGILIO UWANJA WA CHAMAZI- AZAM
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limefanyia marekebisho viingilio vya mechi za Ligi Kuu ya Vodacom zitakazochezwa katika Uwanja wa Azam ulioko eneo la Chamazi, Dar es Salaam.
 
Viingilio katika mechi za uwanja huo sasa vitakuwa sh. 1,000 kwa mzunguko na sh. 5,000 kwa jukwaa kuu badala ya vile vya awali vya sh. 3,000 kwa mzunguko na sh. 10,000 kwa jukwaa kuu. Mabadiliko hayo yalianza kwenye mechi ya jana kati ya Azam na JKT Oljoro.
 
Hata hivyo, viingilio hivyo havitatumika kwa mechi zitakazohusu mechi ambazo timu za Simba na Yanga zitacheza kwenye uwanja huo.
 
 
Powered by Sorecson : Creation de site internet
Boniface Wambura Mgoyo
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Reactions::

DAVID KAFULILA AKICHANGIA BUNGENI LEO

Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR –Mageuzi) David Kafulila akichangia bungen kuhusu namna bora ya  ukusanyaji wa mapato kupitia kodi zinazotozwa kwenye makampuni ya simu nchini ili kuongeza mapato ya serikali leo mjini Dodoma.
Picha na Aron Msigwa-MAELEZO
Reactions::

DKT BILAL APOKEA WANACHAMA WAPYA KATIKA MAADHIMISHO YA MIAKA 35 YA CCM KIBAHA VIJIJINI

 Baadhi ya Wanachama wapya waliojiunga na Chama cha Mapinduzi CCM, wakila kiapo baada ya kukabidhiwa kadi zao za uanachama na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 35 ya chama hicho zilizofanyika jana Februari 5, 2012 Wilaya ya Kibaha Vijijini.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi cheti, Katibu wa CCM wa Wilaya ya Mafia, Abdallah Mdimu, baada ya Wilaya hiyo kuibuka mshindi wa kwanza kwa ulipaji wa Ada za Wanachama, wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 35 ya chama hicho zilizofanyika Wilaya ya Kibaha Vijijini jana Februari 5, 2012
 Katibu wa CCM Wilaya ya Kibaha Vijijini, Mohamed Shaban, akimbeba juu juu mwanachama mpya, Omar Said Hunda, aliyekuwa mgombea Udiwani Kata ya Dutumi kwa tiketi ya CUF katika uchaguzi wa mwaka 2010, aliyejiengua katika chama hicho na kujiunga na CCM. Hapa mwanachama huyu alikuwa akipelekwa mbele ya mgeni rasmi Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal kwa ajili ya kukabidhi kadi yake wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 35 ya CCM, zilizofanyika Wilaya ya Kibaha Vijijini Mkoa wa Pwani, jana Februari 5, 2012.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipokea kadi ya mwanachama mpya kutoka CUF, Omar Said Hunda, aliyeamua kujiunga na CCM, wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 35 ya CCM, zilizofanyika Wilaya ya Kibaha Vijijini Mkoa wa Pwani, jana Februari 5, 2012. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
Reactions::

MAKAMU WA RAIS AAGANA NA BALOZI WA CHINA ALIYEMALIZA MUDA WAKE

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Balozi wa China nchini Tanzania, Liu Xinsheng, aliyefika ofisini kwake Ikulu Dar es Salaam leo Februari 6, 2012 kwa ajili ya kumuaga baada ya kumaliza muda wake nchini

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipokea zawadi ya kitabu cha China kutoka kwa Balozi wa China nchini Tanzania, Liu Xinsheng, aliyefika ofisini kwake Ikulu Dar es Salaam leo Februari 6, 2012 kwa ajili ya kumuaga baada ya kumaliza muda wake nchini. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
Reactions::

Watanzania watakiwa kulinda Utamaduni


 
Benjamin Sawe
 
Kitengo cha Habari
 
Zanzibar
 
Watanzania wametakiwa kulinda na kulinda na kuheshimu tamaduni ili waweze kusongambele na kujiletea maendeleo.
 
Hayo yamesemwa na Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Maendeleo ya Utamaduni Bi. Lily Beleko katika mafunzo kwa maafisa wa Idara mbalimbali  za serikali.
 
Akiongea kwenye mafunzo hayo Bi Beleko alisema lengo la mafunzo hayo ni kuelimisha umma wa watanzania kulinda,kuheshinu,ikiwa ni pamoja na kushirikiana katika nyanja za kiutamaduni.
 
Akifungua mafunzo hayo Kamishna wa Utamaduni na Michezo Zanzibar bwana Hamadi Bakari Mshindo alisema kuna umuhimu wa kulinda utamaduni na kuheshimu tamzaduni za mataifa mengine.
 
“Kuna umuhimu wa kulinda na kuheshimu tamaduni zetu na tamaduni za mataifa mengine lakini tuheshimu tamaduni zile zilizo nzuri pekee na kuacha tamaduni zisisoendana na mila mna tamaduni za mwafrika”.Alisema Bwana Mshindo
 
Bwana Mshindo alisema ni wajibu kwa kila mtanzania kulinda na kuheshimmu tamaduni za mwafrika na za mataifa mengine kwa ujumla.
Alisema mara nyingi kuna miradi mingi ya maendeleo inafanyika katika maeneo mbalimbali lakini tamaduni za sehemu husika zinakuwa hazifuatwi.
 
Aidha alisema kwa upande wa Zanzibar wameshaanza kutoa elimu jinsi ya kulinda na kuheshimu tamaduni za jamii mbalimbali
 
Reactions::

BUNGENI: HUU NI UTANI AU NINI?

Nami nimeona bunge likiahirishwa kabla ya muda kwa sababu muswada wa marekebisho ya sheria ya katiba haujaletwa kama ratiba ilivyoonyesha.Kila mtu hata mtoto anayejua kusoma alijua ratiba ya leo bungeni na kutokana na maslahi umma tulionao juu ya jambo hili tulikuwa kwa makumi mbele ya luninga tukisubiri kwa hamu muswada huu.Ghafla tangazo likaja kuwa kamati (???) haijakamilisha muswada hivyo mpaka kesho.Kumekuwa na hasira na matusi mazito mengine hatuwezi kuyaandika hapa dhidi ya Ndugai binafsi na bunge kama taasisi.Itoshe tu kusema kuwa uzembe huu wa makusudi na dharau kwa wananchi inayoendelezwa na bunge letu haina faida kwa taifa.Tumesikia kuwa kuna utata baina ya serikali na wabunge wa CCM juu ya maswada husika na inawezekana hii ni dalili kuwa serikali imenywea kwa wabunge hao kwani kabla ya kuahirisha bunge wabunge wa CCM wameambiwa wasizime simu wala kwenda mbali wataitana muda wowote.Hata mimi asiyesoma sana nadhani kuna kitu kitafanyika watakapoitana watu hawa.kama ni utabiri basi nautoa,kwa kuwa tumesikia kuwa wanapanga kukataa marekebisho ya sheria ya katiba basi kwangu mawili tu yatafanyika.Moja ni kama ilivyoanza kuleta dalili:piga danadana na weka mizengwe hadi jambo hili lisipate nafasi wakati huu ili ` tujipange`na au ita wabunge wa CCM wabembeleze, waombe au watishe ili wakubaliane na pendekezo la serikali.Yote mawili yamekaa vibaya kwa wale wahafidhina waliozomeazomea siku zile kinyume na matakwa ya wengi.Mzaburi anasema wamechimba shimo kubwa ila wametumbukia wenyewe.Na tusubiri tuone.
Msaidizi wa Mwenyekiti,Dar es salaam
Reactions::

SERENGETI BREWERIES LIMITED KUENDELEZA USHIRIKIANO NA TAASISI ZA FEDHA

Afisa Masoko Mwandamizi wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) katika mikoa ya Arusha na Manyara Joan Semuguruka akitoa salamu za kampuni hiyo kwa wafanyakazi wa benki mbalimbali (hawapo pichani) zilizoshiriki hafla ya 'Bankers Gala Night' iliyofanyika mkoani Arusha mwishoni mwa wiki.SBL kupitia bia yake ya Tusker Malt ilidhamini hafla hiyo.
Baadhi ya wafanyakazi wa benki tofauti nchini wakipatiwa utaratibu kabla ya kuingia katika hafla iliyowakutanisha pamoja wafanyakazi wa benki katika tukio lililojulikana kama 'Bankers Gala Night'.Tukio hilo lilifanyika mwishoni mwa wiki jijini Arusha na kudhaminiwa na Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) kupitia bia yake ya Tusker Malt.


KAMPUNI ya Bia ya Serengeti (SBL) kupitia bia yake ya Tusker Malt imeahidi kuendelea kutoa ushirikiano ndani ya sekta mbalimbali ikiwemo sekta ya kibenki katika lengo la kukuza maendeleo ya uchumi nchini.
Hii ilikuwa wakati wa hafla maalum ya wadau katika sekta ya kibenki iliyodhaminiwa na bia ya Tusker Malt na kuzileta pamoja taasisi za kifedha zikiwemo benki zinazoongoza kibiashara nchini.
Hafla hiyo ilifanyika katika Hotel ya Snow Crest jijini Arusha mwishoni mwa wiki ilitoa fursa maalum kwa wawakilishi wa taasisi mbalimbali za kibenki kuzungumza pamoja changamoto mbalimbali zinazoikabiri sekta ya fedha nchini.
Akizungumza wakati wa halfa, Afisa wa kampuni ya Serengeti wa Nyanda za Juu Kaskazini, Bw. Mapendo, alisema kuwa kampuni yake itaendelea kufanya kazi karibu na wadau wote ili kuleta maendeleo ya uchumi nchini.
Alisema hafla hiyo imetoa nafasi kubwa kwa wadau wa taasisi za kifedha haswa za kibenki kuungana pamoja na kubadilishana mawazo jinsi gani wanaweza kusonga mbele na kupanua sekta hiyo muhimu katika uchumi wa taifa.
Mapendo alisema SBL kupitia kinywaji chake cha Tusker Malt imedhamini hafla hiyo na kwamba itaendelea kushirikiana na sekta hiyo katika mambo mbalimbali kulingana na uwezo wake kifedha.
“Sekta ya kibenki inakuwa kwa kasi sana na hivyo kutoa fursa nyingi mbalimbali kwa nyanja zote mbili za kibiashara pamoja na ajira kwa watanzania walio wengi. Na fursa hizo huonekana zaidi wakati wa matukio muhimu kama haya.
"Tunaamini kwamba kupitia hafla hii, jamii ya wafanyabiashara itachukua na kuzifanyia kazi fursa zilizopatikana. Tunajivunia kuwa wadhamini wakuu wa tukio hili.
“Bia ya Tusker Malt imekuwa ikidhamini matukio mbalimbali nchini lakini mwaka huu tumedhamiria kuweka mkakati madhubuti ambao unaangalia zaidi biashara katika makampuni na makundi mengine ndani ya jamii,” aliongeza.
Kwa upande wake mwakilishi wa waandaaji wa tukio hilo Peter Morgan aliishukuru Tusker Malt kwa udhamini wake na kusema kuwa ni vyema SBL ikaendeleza wazo hilo zuri la kuwa na matukio kama hayo katika kanda mbalimbali nchini.
“Hili ni tukio la kukumbukwa ndani ya jamii ya wadau wa taasisi za kibenki. Tumeweza kuzikutanisha taasisi mbalimbali za kifedha pamoja si kukutana tu bali pia kuweza kubadilishana mawazo jinsi ya kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabiri sekta ya kibenki. Tunaishukuru bia ya Tusker Malt kwa udhamini wake,” alisema.
Reactions::

KITUO CHA UTAMADUNI CHA IRANI CHAADHIMISHA MAPINDUZI YA IRANI


Mkurugenzi mtendaji kituo cha utamaduni wa jamhuri ya kiislam Bw. Mortazar Sabour akiongea na waandishi wa habari kwenye maadhimisho miaka 33 ya mapinduzi ya kiislam ya yaliyotokea mwaka 1979 chini ya utawala wa Imamu Ayatolla Khomein yaliofanyika juzi katika kituo cha utamaduni cha Iran jijini Dar es salaam.
Kutoka fullshangweblog
Reactions::

Uchambuzi Wa Habari: Alichosema Ali Mufuruki


Ndugu zangu,

Kwenye gazeti la Mwananchi jana Jumapili kulikuwa  na habari ukurasa wa tano inayosema; “Mufuruki: Itikadi za kisiaa zinakwamisha wananchi”.  ( Mwananchi Jumapili, Februari 5, 2012)

Habari hiyo ilinivutia sana na ikawa ya kwanza kwangu kuisoma. Mwandishi Exuper Kachenje anaripoti, kuwa  Mwenyekiti wa Jukwaa la Maafisa Watendaji Wakuu wa Kampuni Binafsi nchini  Bw. Ali Mafuruki ametaja kuwa itikadi za kisiasa ni  vikwazo vikubwa  vilivyowanyima  na vinavyoendelea kuwanyima  wafanyabiashara wazalendo nafasi  wakiachwa nyuma  na kuwapendelea  wageni wanaoshikilia uchumi wa Tanzania kwa kiasi kikubwa.

Ali Mufuruki anasema; ” Vikwazo vikubwa kuliko vyote ambavyo mpaka leo vipo ni vile vilivyotokana na itikadi ya kisiasa ambavyo siyo tu ilimnyima nafasi mfanyabiashara mzalendo, bali pia iliwapendelea zaidi wasio wazalendo.”- Ali Mufuruki.

Mufuruki anazidi kubainisha, kuwa kwa muda mrefu Watanzania wengi wenye uwezo wa kufanya biashara kubwa walikimbilia kufanya kazi za kuajiriwa Serikalini, kwenye shughuli za za siasa huku wasio na uwezo  wa kupata ajira  wakihangaika na biashara ndogondogo na kuiacha sekta ya biashara kubwa kwenye mikono ya watu wenye asili ya kiasia.

Bwana Mufuruki akazidi kuwa mkweli na kusema, kuwa waasisi wa Uhuru wetu  walitilia mkazo zaidi udhibiti wa nguvu ya utawala wa kisiasa bila kujali nafasi ya wananchi wao katika kudhibiti nguvu za uchumi. Hilo, kwa mujibu wa Mufuruki, ndilo  lililowaacha  wenye uwezo zaidi kudhibiti nguvu za uchumi wa nchi kwa miaka mingi ijayo.

Mtazamo wangu;

Bwana  Ali Mufuruki amekuja na hoja  ya kizalendo, nzito na muhimu sana kwa nchi yetu kwa sasa.  Watanzania tumekuwa kama wagonjwa wa muda mrefu ambao,  waganga mbali mbali  tuliowapata wameshindwa kutwambia chanzo cha maradhi yetu. Hivyo basi, wameishia kujaribisha tiba , moja baada ya nyingine, bila mafanikio. Watanzania bado ni  wagonjwa kiuchumi.

Ali Mufuruki ametusaidia kujua chanzo cha maradhi yetu. Na yuko sahihi kabisa. Alichokisema Mufuruki mara kadhaa nimekiita kuwa ni ubaguzi wa kisiasa. Nchi yetu inasumbuliwa na ’maradhi ya  ubaguzi wa kisiasa’. CCM , kama ilivyokuwa kwa TANU, bado inaamini katika udhibiti wa nguvu za kisiasa.

Kuna mifano kadhaa  ya Watanzania wazalendo waliofilisika kibiashara kwa ’ dhambi ya kuwaunga mkono wapinzani’. Tuna mifano kadhaa ya wafanyabiashara Watanzania wenye asili ya kiasia ambao biashara zao zinashamiri kwa vile walichagua tangu enzi, kuwa wafadhili wa TANU na baadae CCM ambayo ina hamu ya kuendelea kudhibiti nguvu za kisiasa badala ya kuandaa mazingira ya wananchi wake wadhibiti uchumi wao.

Wakati CCM ikitimiza miaka 35, hoja ya Ali Mufuruki waichukulie kama changamoto.  Maana, zama za udhibiti wa nguvu za  kisiasa zimepita.  Kwenye pluralism kuna ustawi . Kwenye  ' Chama Kushika Hatamu' kuna kudumaa. Huwezi leo kuendelea na udhibiti wa nguvu za kisiasa kama wananchi wako hawana udhibiti wa nguvu za kiuchumi na badala yake udhibiti huo huko mikononi mwa wananchi wako wachache wenye asili ya kiasia au wageni wanaoitwa wawekezaji.

Na huu si wakati tena wa kuwa na wanasiasa wenye kutoa hadharani, kauli kama; ” Anayetaka biashara yake imwendeee vizuri aje CCM!”

Tubadilike ili tusonge mbele kiuchumi , na tuzidi kuwa Wamoja kama taifa.

Maggid Mjengwa,
Dar es Salaam.
Jumatatu, Februari 6, 2012
Reactions::

VODACOM NA CCBRT WAANZISHA KAMPENI DHIDI YA FISTULA



Reactions::

TUME YA UCHAGUZI: SOMO KUTOKA ZANZIBAR

Afisa msaidizi wa Tume ya uchaguzi jimbo la Uzini akiwa ofisini
Afisi ya Tume ya uchaguzi jimbo la Uzini

Kuna jambo zuri Tanzania bara yaweza kujifunza kutoka hapa karibu Zanzibar.Wao tume ya uchaguzi imeajiri watumishi wake yenyewe na inazo ofisi zake yenyewe.Kwetu bara tume haina watumishi inategemea wale wa Tamisemi.Hawa ni watu wa serikali au ikiwekwa vizuri hawa ni watu wa CCM.Ikiwa hili limesaidia tume ya uchaguzi Zanzibar kuwa huru na kutenda haki,hili ni swali tofauti kabisa.Ila lipo dogo la kujifunza kutoka Zanzibar.
Mdau wa Mjengwablog,Uzini Zanzibar
Reactions::

KAMPENI ZAPAMBA MOTO UZINI


Na Mdau wa Mjengwablog, Zanzibar
Reactions::

RAIS KIKWETE AKUTANA NA UJUMBE WA JIJI LA WURZUBURG

Picha na IKULU
       Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Jumapili, Februari 5, 2012, amekutana na kufanya mazungumzo na Meya wa Mji wa Wurzburg wa Ujerumani, Mheshimiwa George Rosenthal.
      Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika kwenye Ikulu Ndogo mjini Mwanza, Meya Rosenthal ameambatana na madiwani wanne, mkewe, Hanna Rosenthal na binti yake, Lisa Rosenthal.
      Ujumbe huo wa mji wa Wurzburg unatembelea Jiji la Mwanza kwa muda wa wiki moja ikiwa ni ziara ya kirafiki kati ya miji hiyo miwili uhusiano wa kindugu.
      Mji wa Wurzburg ulianzishwa miaka 1,300 iliyopita, una vyuo vikuu vitatu na wanafunzi kiasi cha 30,000 wanaosoma katika vyuo hivyo.
      Mji wa Wurzburg unalisaidia Jiji la Mwanza katika maeneo kadhaa ikiwa ni pamoja na utunzaji mazingira, afya, nishati. Pia miji hiyo miwili ina program ya kubadilishana wanafunzi  kwa maana ya wanafunzi wa miji hiyo miwili kutembeleana na pia Jiji la Wurzburg linaisaidia taasisi za kijamii za Jiji la Mwanza.
      Rais Kikwete amemwambia Meya Rosenthal kuwa Tanzania na Ujerumani zina uhusiano mzuri na wa karibu na Serikali yake imedhamiria kukuza na kuimarisha zaidi uhusiano huo.
      Rais pia amesifu uhusiano huo wa kindugu kati ya miji ya Mwanza na Wurzburg na ametaka miji hiyo kuimarisha uhusiano huo kwa sababu ni muhimu na unanufaisha pande zote mbili. Rais Kikwete yuko katika ziara ya siku tatu mkoani Mwanza.
Mwisho.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
05 Februari, 2012
Reactions::

RAIS KIKWETE AZINDUA KITABU CHA MZEE MSEKWA



Picha na IKULU
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com                                    


PRESIDENT’S OFFICE,
THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
press@ikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Jumapili, Februari 5, 2012, amezindua Kitabu kiitwacho Uongozi na Utawala wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika halfa fupi iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu Ndogo Mjini Mwanza.

Kitabu hicho kilichoandikwa na Makamu Mwenyekiti wa CCM, Mheshimiwa Pius Msekwa kinaelezea uzoefu wa miaka 25 ya Mzee Msekwa katika utumishi wa umma chini ya uongozi wa Baba wa Taifa, Mwalimu K. Nyerere.

Sherehe za uzinduzi wa kitabu hicho chenye kusara 156 zimehudhuriwa na viongozi mbali mbali wakiwamo mawaziri, viongozi waandamizi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) akiwamo Katibu Mkuu Mheshimiwa Wilson Mukama na viongozi wa Mkoa wa Mwanza.

Akizungumza kabla ya Mheshimiwa Rais Kikwete hajazindua kitabu hicho, Mzee Msekwa amesema kuwa moja ya mambo yaliyomchochea aandike kitabu hicho ni pamoja na changamoto aliyopata kuitoa Rais Kikwete kwa viongozi wastaafu wa umma kuchangia maendelea na historia ya Tanzania kwa kuandika vitabu kuelezea uzoefu wao katika utumishi wa umma.

Akizungumza mara baada ya uzinduzi wa kitabu hicho, Mheshimiwa Rais Kikwete amempogeza Mzee Msekwa kwa kuandika kitabu hicho na kuwataka wastaafu wengine wa utumishi wa umma kufuata mfano wa Mzee huyo kwa kuandika uzoefu wake katika kuwatumikia Watanzania.

Kabla ya kuwa Makamu Mwenyekiti wa CCM, Mheshimiwa Msekwa ameshika nafasi nyingi za madaraka katika Serikali na siasa ikiwa ni pamoja na kuwa Katibu wa Bunge, Makamu wa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Katibu Mtendaji wa chama cha TANU, Mtendaji Mkuu wa CCM, Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Rais Kikwete yuko katika ziara ya siku tatu mjini Mwanza ambako leo alikuwa Mgeni Rasmi kwenye Sherehe za Miaka 35 ya CCM zilizofanyika kwenye Uwanja wa CCM, Kirumba.

Mwisho.

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,

Ikulu.

Dar es Salaam.

05 Februari, 2012
Reactions::

Sunday, February 05, 2012

Nimetamani Sana Ku-Skii!

 Ndugu zangu,
Leo usiku kwenye  televisheni ya BBC nimeona picha ya theluji nyingi ikianguka Ulaya. Nimetamani sana ku-skii. Nilipoishi Ulaya nili-skii sana wakati wa winter. Hapo pichani nina skii kwa kufuata mkondo wa maji ya mto. Juu kuna barafu na theluji na chini kuna maji yanapita. Ni siku nyingi  sijaskii.
Maggid,
Dar es Salaam  ( Yenye jua na joto kali)
Reactions::

Bi Mkora; " Kwanini Wanaume Wengine Ni Waoga Wa Kutongozwa?"

Bi Mkora, 
Tusaidie. Baadhi ya wanaume ni waoga wa kutongozwa na wanawake. Hii ni kwa mujibu wa tafiti na uzoefu uliopo. Hapa kuna sababu za kijamii ikiwamo malezi, mila na desturi.
Bado inaonekana na wengi kama kitendo cha ajabu kwa mwanamke kuanza kuchukua hatua za kumtongoza mwanamme anayempenda ama kuvutiwa naye.
 
Kuna wanaume wanaoamini, kuwa jambo hilo si la ki-uanauke. Mwanamme bado anaamini kuwa jukumu la kuchukua hatua za kutongoza ni za kwake,kwamba ni yeye ndiye anayepaswa kuanza kumtongoza mwanammke. Akitongozwa anashtuka!
Inakuwaje basi,kama mwanamke atampenda ama kuvutiwa na mwanamme bila mwanamme huyo kuweza kusoma ishara za mapenzi, je, mwanamke huyo asubiri mpaka siku ile mwanamme atakapolala na kuota kuwa anapendwa na mwanamke huyo? Kazi kwako Bi Mkora na wengine mlio tayari kuchangia.
Mdau.
Reactions::

KILELE CHA SHEREHE ZA KUZALIWA CCM MWANZA KATIKA PICHA

Jk kati. Kushoto Msekwa,  Clement Mabina, kulia Mukama akipokea heshima ya gwaride











        Picha na IKULU na Bashir Nkoromo                                                                          
Reactions::

AJALI ENEO LA NDULI IRINGA

Ajali hii ilihusisha pikipiki na baiskeli katika eneo la Nduli mkoani Iringa. Barabara ni pana sana, lakini sijui ilikuwaje wakagongana. Mwendesha baiskeli aliyeketi alikuwa amepakia ulanzi.Inawezekana ni matokeo ya kilaji! 
Manyerere Jackton
Reactions::

DKT. BILAL MGENI RASMI MKESHA WA MAULID MNAZI MMOJA DAR

  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi, wakati alipowasili kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja katika shambrashambra za mkesha wa sherehe za Maulid, jijini Dar es Salaam jana Februari 04, 2012 usiku
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal(katikati) Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi na Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowasa, wakiwa katika sherehe za mkesha wa Maulid, zilizofanyika usiku wa kuamkia leo, jana usiku Februari 04, 2012, katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiteta jambo na Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowasa, wakati wakiwa katika sherehe za mkesha wa Maulid, zilizofanyika usiku wa kuamkia leo, jana usiku Februari 04, 2012, katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam
 Muumin wa dini ya kiislam kutoka Msikiti wa Suni Hanafi wa jijini Dar es Salaam, Muzamil Chaki, akiimba Qaswaida jukwaani kutoa burudani wakati wa mkesha wa sherehe za Mauilid zilizofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini jana usiku Februari 04, 2012
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Mohammed Gharib Bilal,
akisalimiana na Muumin wa dini ya kiislam kutoka Msikiti wa Suni Hanafi wa jijini Dar es
Salaam, Muzamil Chaki, baada ya muumini huyo kumaliza kutoa burudani ya Qaswaida jukwaani, wakati wa mkesha wa sherehe za Mauilid zilizofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini jana usiku Februari 04, 2012.
Picha ya pamoja
Picha na Muhidin Sufiani-OMR
Reactions::

Neno La Leo: Kikwete Ni Kama Mungu!


Ndugu zangu,

Ni Jumapili nyingine. Nina neno. Askofu Msaidizi wa Jimbo Katoliki la Bukoba , Dk. Methodius Kilaini ameongea na  mwandishi wa gazeti la Mwananchi  leo Jumapili, Februari 5, 2012.

 Askofu Kilaini ameulizwa juu ya kauli yake ya miaka ya nyuma alipokaririwa akitamka, kuwa Kikwete ni chaguo la Mungu.  Je, Kikwete ni chaguo la Mungu?

Askofu Kilaini anajibu; ” Nilichosema ni kwamba, sauti ya watu ni sauti ya  Mungu”.  Anajibu Askofu Kilaini  na kufafanua;  kwa vile Rais alichaguliwa na asilimia 80 ya watu, hivyo, amekubalika na watu. Anasema Askofu Kilaini.
Askofu Kilaini anatuleta kwenye mantiki hii; kuwa Kikwete ni kama Mungu, na hapa kwa vile Katiba yetu ya sasa nayo inampa nguvu nyingi Rais, basi, ni  nguvu zinazoweza kufanana na za Mungu.

Na Askofu Kilaini anatamani tutawaliwe na ’ dikteta’  ili mambo yetu yanyooke. Ndio,  Askofu Kilaini amekaririwa na gazeti la Mwananchi la leo Jumapili akitamka; kuwa ili nchi isonge mbele, inahitaji  kiongozi atakayeongoza  kwa ’ mkono wa chuma’.  Amemtaja Rais Paul Kagame kama mfano wa aina hiyo ya kiongozi.

Natumaini Askofu amenukuliwa vibaya na mwandishi, lakini,  kama alichosema ndicho, basi, natumaini hakumaanisha alichosema. Na kama amemaanisha alichosema, basi, napingana vikali na mafundisho hayo ya  Baba Askofu Kilaini.
Maana,  nchi yetu inachohitaji ni kiongozi na si mtawala.  Anayetumia ’ mkono wa chuma’- Iron Feast huyo anatawala, haongozi. Huyo atakuwa ni dikteta na si kitu kingine.

Ndio,  mtawala anayetumia ’ mkono wa chuma’ hutumia pia risasi za shaba kuwanyamazisha wanaopingana nae, hata kwa hoja tu. Samahani  Askofu Kilaini, Watanzania  tungependa tupate kiongozi na si mtawala. 
Na tunamshukuru Mungu kwa kutuepusha kuwa na mtawala anayeendesha nchi kwa ' mkono wa chuma'.

Na Kikwete huyu tuliye naye walau ameonyesha  uongozi kwa kutamani Tanzania ije kupata kiongozi. Ni kwa kupitia mabadiliko haya ya Katiba tunayokwenda kuyafanya.  Na ndio maana,  hata ndani ya chama chake kuna wanaojipanga kupingana nae ili azma ya  Kikwete kufanikisha mabadiliko makubwa ya Katiba ya nchi ishindikane.

Na ni matumaini yetu, kuwa Rais Jakaya  Kikwete atatumia nguvu hizi za mfano wa Mungu alizopewa na Katiba ya sasa katika  kuhakikisha Bunge linapitisha marekebisho ya sheria ya kuanzisha mchakato wa Katiba kama alivyoshauriwa na wadau nje ya CCM na akaafikiana nao.

Hakika, Rais Kikwete atakuwa mtu wa ajabu kama ataendekeza matakwa ya wachache wasiotaka mabadiliko ndani ya chama chake  na hivyo basi, kujinyima mwenyewe nafasi yake katika historia ya nchi hii. Maana, Kikwete huyu anaweza kuacha nyuma yake, kumbukumbu ya kudumu ’ Legacy’ ya kuwa ndiye Rais wa nchi, baada ya miaka 50 ya uhuru, aliyefanikiwa kuwafanya Wazanzibar kuendesha siasa zisizo na chuki miongoni mwao, lakini, aliyefuta pia ubaguzi wa kisiasa kwa Tanzania bara. Ni   kwa kuwezesha kuwepo kwa Katiba mpya ambayo, bila shaka, itasafisha njia ya kuwepo , mbali ya mambo mengine,  kipengele kitachoruhusu kuundwa kwa Serikali ya Mseto kama ilivyo kwa visiwani.

Naam, Kikwete wa sasa amekuwa ni kiongozi anayejitahidi sana kupima upepo. Huenda ameshabaini , kuwa Watanzania walio wengi, ni  wale asilimia 80 anaosema Askofu Kilaini, kuwa ni wenye kutaka mabadiliko.  Ndio, sauti ya watu ni sauti ya Mungu.  Anasema Askofu Kilaini.

Hivyo basi, na Kikwete bila shaka  anajua , kuwa CCM ni mkusanyiko wa wanachama milioni tano tu kati ya Watanzania milioni 40. Na kama Mungu, kama wananchi walio wengi   wanataka mabadiliko ya kimfumo kupitia Katiba. Basi, anapaswa kusikiliza sauti za wengi, hata kama wako nje ya chama chake.

Na  kama walio wengi wanatoa sauti za kupinga ongezeko la posho za wabunge. Rais anapaswa kusikiliza sauti za wengi.  Kwamba  anaweza kuacha ’ kubariki’ ongezeko la posho na umma ukabaki nyuma yake.  Maana, sauti za wananchi zapaswa kuwa sauti ya Rais,  kwa mantiki ya Askofu Kilaini. Ndio, Rais asipobariki  ongezeko la posho za wabunge bado atabaki na ’ waumini’ wengi tu.

Na je, wenzake ndani ya chama wakiamua kupiga kura ya kukosa imani na Kikwete?

Astaghafillulahi!  Hebu tema mate chini usije fikwa na laana. Hilo haliwezekani kamwe. Si tulimsikia Beatrice Shelukindo akipendekeza hilo kwa wabunge wenzake wa CCM juzi kule Dodoma. Akasimama Mbunge Ole Sendeka na kumtamkia Shelukindo; ” Futa kauli yako!” Na Shelukindo akasimama haraka na kukubali kufuta kauli yake.  Naam. Kikwete ni kama Mungu. Na yawezekana hataki Rais ajaye awe kama yeye. Kama hivyo ndivyo, basi, Mwenyezi Mungu ashukuriwe.

Kuna wakati , miaka ya mwanzoni mwa uhuru, Julius  Nyerere alipata kumwambia mwandishi wa habari wa Kimagharibi; ” Rais Afrika n i mtu mwenye nguvu sana. Akikohoa tu. Waliomzunguka watashtuka na kunong’onezana kwa kusema; ” Bwana mkubwa amekohoa!”.

Ndio, Rais Afrika anaweza kuamka asubuhi na kuamua kufanya chochote anachotaka, hata kama kutaifisha mashamba  na nyumba za watu.  Rais yuko juu ya kila kitu.

Na Katiba yetu ya sasa inasema , mbunge anapovuliwa uanachama wa chama chake anapoteza sifa ya kuwa Mbunge.  Lakini, hakuna mahali popote kwenye Katiba panaposema , kuwa Rais anapovuliwa  uanachama wa chama chake,   kuwa anapoteza sifa ya kuwa Rais.  Hivyo basi, kimsingi, Rais anaweza kuhama chama chake, akaingia chama kingine na akabaki kuwa Rais, kwa  mujibu wa Katiba ya sasa.

Naam,  haiyumkini kwa ’ waumini’ kumvua Mungu mamlaka yake. Lakini, waumini wanaweza  kujitenga au kutengwa na Mungu  wao. Mungu hawezi kukosa waumini wapya . Na waumini wale waliojitenga au kutengwa na Mungu wao wanaweza kuzibiwa njia  ya kwenda peponi, na Mungu wao.

Hakika, tunahitaji Katiba Mpya itakayotunusuru na balaa la siku moja kuamka na kukuta tuna mtawala anayetumia ’ mkono wa chuma’.  Ni Katiba mpya itakayotusaidia kumpata kiongozi  mkuu na viongozi wa kumsaidia kiongozi mkuu katika kuliongoza taifa letu n a si kulitawala. Na hilo ni Neno la Leo.

Mungu Ibariki Afrika, Mungu Ibariki Tanzania.


Maggid Mjengwa
Dar es Salaam,
Jumapili, Februari, 5, 2012
Reactions::

Makubwa Haya....

Sifael Paul na Amran Kaima
Mshituko! Katika hali isiyotarajiwa, mwanamuziki Judith Daines Wambura Mbibo a.k.a Lady Jaydee au Jide,  (pichani) amewahuzunisha mashabiki wake baada ya kuonesha picha ya jeneza lake litakavyokuwa siku akiaga dunia. LIWE NA RANGI ZA ZAMBARAU NA NYEUPE
Kupitia ‘blogu’ yake, Jide alitundika picha mbili za jeneza lenye rangi za zambarau na nyeupe, akiambatanisha na maelezo kuwa yuko mbioni kuwadondoshea simulizi kamili ya tukio hilo litakavyokuwa kupitia wimbo wake mpya.
Risasi Jumamosi liliinyaka ishu hiyo... Soma zaidi; http://www.globalpublishers.info
Reactions::

JK AONGOZA MATEMBEZI MIAKA 35 YA CCM

  Kikwete akimsalimia Katibu Mkuu wa CCM mstaafu, Philip Mangula kabla yamatembezi kuanza Ofisi ya CCM mkoa wa Mwanza. Kulia ni Katibu Mkuu Mstaafu Yussuf Makamba.
 Rais Kikwete akimsalimia Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye kabla ya matembezi hayo.
  Wananchi kutroka maeneo mbalimbali ya mkoa wa Mwanza wakiwa kwenye Ofisi ya CCM mkoa huo tayari kushiriki matembezi hayo.
Katibu Mkuu wa CCM Wilson Mukama akiwa na Makatibu wastaafu wa CCM, Yussuf Makamba na Philip Mangula kabla yamatembezi kuanza.
  Vijana wa Sungusungu wakijifua kabla ya matembezi kuanza.
Reactions::