Subscribe:

Sunday, May 27, 2012

Magazeti Leo Jumapili











Kunradhi,kuna shida kuapload picha,hivyo tunapata ugumu kuingiza magazeti.tunaendelea kujaribu.samahani kwa usumbufu wowote kwa uchelewaji huu.
Msaidizi wa Mwenyekiti,Dar.
Magazeti mengine yatafuatia hivi punde....
Reactions::

Mjumbe Maria William- " Mwenyekiti, Natafuta Mchumba Wa Kunioa, Awe Tayari Kupima Ukimwi"

Habari kaka, 
Naitwa dada Maria, kwasasa napatikana nje ya Tanzania. Naomba uniwekee tangazo langu kwenye blog yako kuwa natafuta mchumba ili tufike kwenye ndoa. Mchumba ninayemtafuta awe mwenye umri kuanzia miaka 35 mpaka 39. Awe na elimu ya chuo kikuu, awe mkristo, mkweli, mwaminifu, anayejishughulisha, asiyekuwa na watoto, pia awe tayari kupima Ukimwi. Kama anaishi nje ya Tanzania itakuwa vizuri zaidi ili iwe rahisi kukutana na kufahamiana vizuri. Namba yangu ya simu nitatoa baada ya kufahamiana na mhusika. Email yenye picha itapewa kipaumbele zaidi. Napatikana kwenye email: mariawilliam700@yahoo.com
Reactions::

John Shibuda Na Hoja Yake Ya Ukabila ( Makala, Mwananchi Jumapili)

Ndugu zangu,

Kuna wakati nilitua uwanja wa ndege wa Nairobi na kupanda teksi.  Nilishangaa sana pale dereva wa teksi alipojitambulisha kwangu kwa kutamka; “ I am Peter, and a Kikuyu”


Kwamba anaitwa Peter na kabila lake ni Mkikuyu. Kwa mimi Mtanzania hilo lilikuwa jambo la ajabu sana. Sijapata kujitambulisha kwa  jina na kabila langu katika maisha yangu yote. Si kawaida yetu Watanzania.

Katika nchi za wenzetu kuna tatizo la ukabila. Watanzania tuna bahati kubwa; hatuna ukabila. Labda ukabila wetu upo kwenye lugha ya Kiswahili. Udugu wetu  Watanzania umejenga sana kwenye lugha ya Kiswahili. Anayezungumza lugha ya Kiswahili ni mwenzako huyo, huulizi tena kabila lake.

Ndio, Watanzania hatuna ukabila wala udini. Wenye kutaka kupandikiza mbegu za chuki za ukabila na udini miongoni mwetu ni wachache sana, na hususan wanasiasa kwa malengo ya kisiasa. Tuwe makini sana.

Ona majuzi hapa, Mtanzania mwenzetu John Shibuda ameibua hoja ya ukabila. Nakubaliana na Shibuda kwenye hoja ya kutaka haki yake ya kutangaza nia ya kuwania Urais wa nchi hii iheshimiwe.

Shibuda ana haki hiyo. Na haitakuwa mara ya kwanza kwake kututangazia Watanzania nia yake hiyo.

Lakini, inasikitisha, kuwa hoja ya pili ya Shibuda imechangia kuua hoja yake ya kwanza; ni hoja ya ukabila.
Shibuda anaonekana kututaka Watanzania tujadili ukabila na hususan chama chake cha Chadema na ukabila ulio ndani ya chama hicho.

Shibuda ni mmoja wa viongozi ninaowaheshimu sana kwa mchango wao kwa taifa letu. Naamini, kuwa Shibuda anaheshimika na wengi wengine hapa nchini. Lakini, kwa kutuletea Watanzania hoja ya Chadema na ukabila,  nahofia Shibuda amepotea.  


Maana, hoja yake haina msingi. Imejengeka katika hisia kuliko uhalisia. Yumkini, Shibuda amekuja na hoja hii sasa, ama , kwa bahati mbaya, au kukusudia. Hilo la mwisho halina kusudi la kujenga, bali kubomoa. Inasikitisha.

Maana, hoja ya ukabila haina umaarufu katika nchi yetu kwa sasa. Watanzania wa sasa hatuendekezi ukabila. Kauli ya

Shibuda kuwa anabaguliwa katika chama chake cha Chadema  kwa vile ni Msukuma haikupaswa kutamkwa kwa  mtu kama Shibuda na haikupaswa kutamkwa na yeye na bado akaendelea kubaki katika chama anachoamini kina ubaguzi wa kikabila na huku mwenyewe akiwa mwathirika wa ubaguzi huo.

Na kwa vile hana ushahidi wowote wa kuthibitisha anachosema, Shibuda anachochea moto ambao Watanzania hatuutaki. Ukabila ni moto wa hatari, kama ilivyo kwa moto wa udini.

Kama Shibuda analalamika kuwa anabaguliwa kwa vile ni Msukuma, ingekuwaje basi, John Shibuda angeitwa Ramadhan Shibuda? Je, angeongeza dai la pili; kuwa anabaguliwa Chadema kwa vile ni Muislamu. Si Mkatoliki?

Kama Shibuda anadhani kauli zake za ukabila zinakisaidia chama chake cha zamani cha CCM, basi, napo anakosea; maana, kwa CCM kuhusishwa sasa na kauli za Shibuda za ukabila, kunakiharibia zaidi kuliko kukijenga kwa Watanzania walio wengi.  Lililo bora kwa CCM sasa ni kujitenga na kauli za Shibuda juu ya ukabila .


Maana, Watanzania wa leo si wa jana.  Ni wepesi sasa wa kubaini hila na ghilba za wanasiasa. Wengi wanaonekana kusikitishwa na hoja ya Shibuda juu ya kubaguliwa kwa vile ni Msukuma.  Wanasikitika kwa vile wanadhani hoja imejengeka katika hila na ghilba kwa wananchi.


Shibuda afahamu ukweli huu; Watanzania walio wengi  kwa sasa wanataka mabadiliko. Wanaiona sasa mishale ya saa ya mabadiliko ikisonga mbele. Wanamwona hata Rais wao, Jakaya Kikwete akisaidia kusukuma mabadiliko hayo.Ni mabadiliko ya kimfumo.


Hivi, ni Watanzania wangapi walifahamu kuhusu uwepo wa CAG miaka mitatu iliyopita?  Hakika, upinzani bungeni, ndani ya chama tawala, na uwepo wa ofisi ya CAG iliyopewa nguvu umeanza kurudisha matumaini ya Watanzania. Uwepo wa uwajibikaji wa viongozi.


Naam, Watanzania hawataki tena kurudi katika mfumo wa chama kimoja  kilichoshika hatamu. Majaribio yote ya kuua upinzani, kufuta fikra huru, yatazidi kulaaniwa na walio wengi katika nchi hii.

Hivyo, Shibuda hawezi tena leo kurudisha nyuma mshale wa saa ya mabadiliko; hata kwa ajenda ya ukabila. Nahitimisha.

Maggid Mjengwa,
Iringa
0788 111 765
Reactions::

Dr Mwakyembe Akesha Stesheni Ya Tazara ( Mwananchi)

Na Geofrey Nyang’oro
WAZIRI wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe  juzi usiku alikesha na abiria zaidi ya 1,000 waliokwama kwa saa 11 katika stesheni ya Shirika la Reli la Tanzania na Zambia (Tazara) jijini Dar es Salaam kutokana treni kukosa mafuta.
 
Kutokana na tatizo hilo, Dk Mwakyembe ambaye alifika katika stesheni hiyo mara baada ya kuwasili kutoka safarini India, aliahidi kuwashughulikia watendaji wa Tazara waliosababisha uzembe huo.
Dk Mwakyembe ambaye ametimiza siku 20 tangu alipoteuliwa na Rais Jakaya Kikwete kuongoza Wizara ya Uchukuzi, alifika eneo hilo baada ya abiria wawili kumpigia simu na kuomba aingilie kati tatizo hilo.
 Alifika stesheni katika hiyo saa 4:01 usiku na kukaa mpaka saa 6:30 usiku alipoondoka na hakukuwa na  kiongozi yeyote wa ngazi za juu wa Tazara aliyefika kushughulikia tatizo hilo.   

 Akutana na abiria Baada ya Dk Mwakyembe kuwasili na kuingia katika ukumbi wa kupumuzika abiria wanaposubiri kuondoa, wasafiri walimshangilia kwa nguvu mara baada ya kujitambulisha kuwa ni Waziri wa Uchukuzi na amefika kutatua tatizo linalowakabili, ingawa ni usiku akiwa ametoka safarini India.
Abiria hao waliokuwa na  jazba walimwelezea waziri huyo kuwa kufika kwake eneo hilo ni uzalendo ambao hawakuutegemea na kutaka awapatie majibu ya chanzo cha tatizo na namna atakavyolitatua.
 
Awali, Kabla ya kuingia ndani ya ukumbi huo, uliibuka mvutano wa chini kwa chini baina yake na baadhi ya watendaji na  wanausalama waliotaka asingie ukumbini  kwa hofu ya kufanyiwa vurugu abiria hao waliokuwa na hasiri.
Lakini Dk Mwakyembe aliwataka watendaji wamfungulie mlango ili aingie ndani ya ukumbi kukutana na abiria hao.
 
Alipofunguliwa mlango, Dk Mwakyemba akiwa ameongozana na baadhi ya wafanyakazi wa mamlaka hiyo waliokuwa zamu, aliingia ndani ya ukumbi na umati wa watu  walimzunguka huku kila mmoja akitaka kuwakilisha kilio chake.

Mmoja wa abiria hao alipasa sauti na akisema; “Tunataka uje huku, mpaka muda huu hatujaondoka,  hatuelewi chochote, hatujui kama treni itaondoka au hapana, na kama itaondoka itakuwa saa ngapi? Hawa Tazara wanadharau, wanatutesa! Tunaomba uje utusikilize na ueleze kama safari ipo au la”.   Dk Mwakyembe aliwatuliza akisema; “Tulieni, tulieni! Nimekuja hapa kwa sababu baadhi yenu wamenipigia simu kunieleza kuwa mmekwama hapa kwa muda mrefu na mnahiji  msaada ili muweze kuondoka.
 
“Mimi ndiye Waziri wa Uchukuzi, nimekuja kujionea mwenyewe na kuchukue  hatua. Ninawaahidi hali hii  katika kipindi hiki cha uongozi wangu haitajirudia.
Nitahakikisha ndani ya muda mfupi kunakuwa na mabadiliko makubwa.”
 
Baada ya maelezo hayo, abiria hao walianza kuzungumza  kwa mpangilio na kumweleza waziri huyo kuwa kitendo cha treini ya abiria kuchelewa kuondoka bila taarifa yoyote kinawasababisha usumbufu mkubwa.
Mmoja wa abiria hao, Paulo Michael alisema kama hali hiyo haitadhibitiwa inaweza kulipeleka taifa katika hali mbaya kwa kuwa wananchi wamechoka  na kukataa tamaa.
 
“Mheshimiwa hivi sasa wananchi wamekata tamaa, kama watendaji wa mamlaka hii  wataendelea kututesa namna hii …alilalamika Michael ambaye alionekana kukerwa na kitendo hicho.
Alisema watu wakiwamo wanawake na watoto, wanateseka kutokana na  uzembe wa watu wachache na kwamba, jambo hilo ni hatari kwa usalama wa nchi.
 
Akijibu hilo, Dk Mwakyembe alisema; “Kuhusu hili nawahakikishia kuwa halitatokea tena katika kipindi changu, natambua mmeumia, lakini nawaahidi kufanya mabadiliko, nipeni muda mfupi.”
Abiria hao waliendelea kupaza sauti wakimtaka waziri huyo kutoondoka eneo hilo hadi watakapoondoka kwa kuwa watendaji hao wanaweza kuwadanganya.

Hata hivyo, Waziri Mwakyembe kabla ya ombi hilo la abiria alikuwa ameahidi kuwa hataondoka eneo hilo hadi treni litakapoondoka.
 Dk Mwakyembe..... Soma zaidi; http://www.mwananchi.co.tz
Reactions::

Leo Ni Pentekoste!



Sunday, May 27, 2012
Liturgical Year B, Cycle II
Today's Mass
Pentecost
Readings for Mass
First Reading: Acts 2:1-11
Responsorial Psalm: Psalms 104:1, 24, 29-30, 31, 34
Second Reading: First Corinthians 12:3-7, 12-13
Gospel: John 20:19-23
Liturgical Colour,Red
Today's Rosary: The Glorious Mysteries
Reactions::

Makubwa Haya; Mchakamchaka Na SMG!

Iringa.
Reactions::

Ruaha Half Marathon Jana Jumamosi!



Reactions::

Saturday, May 26, 2012

Kutoka Facebook- Zitto Kabwe Anasema...

"Kama tunalipa wabunge sitting allowances, basi tulipe walimu standing allowance, polisi standing allowance!"-Dr.Slaa #CDMM4CJangwani. I am very proud that i dont pocket sitting allowances to any meeting i attend as an MP. 'Walking the talk'" -Zitto Kabwe
Reactions::

Umati Mkutano Wa Chadema Jagwani Hii Leo

Reactions::

Kutoka Facebook: Nape Asema; " Inatosha!"

"INATOSHA!! Mmewadanganya sana watu, utadhani wakivaa magwanda matatizo yao na ya nchi yanakwisha!! Mnatafuta biashara ya magwanda yenu!! Karibuni nazindua operation ya VUA GWANDA NA GAMBA VAA UZALENDO!! kinachopungua kwetu, Afrika na Dunia nzima ni UZALENDO, sasa tunakwenda kuwavua magwanda na magamba na KUWAVISHA UZALENDO na ndo DAWA INAYOHITAJIKA DUNIANI LEO. Stay tuned!!!! Soon operation hii itaanza tufute uongo!"- Nape Nnauye
Reactions::

CHADEMA Wafunga Barabara Kwa Saa 2 Baada Ya Mkutano

 Wananchi wakitembea kwa mtindo wa maandamano kutoka eneo la mkutano jangwani kuelekea ofisi za CHADEMA kinondoni.
 Mh.Mbowe na Mnyika wakiwa wamesimama kwenye gari wakati wa matembezi wakitoka kwenye mkutano
 Godbless Lema akiwa juu ya gari huku akishangiliwa na vijana jioni baada ya mkutano
 Mbowe akiwatania wanachama ofini kinondoni baada ya wananchi kuanza kudai chama kimfukuze John Shibuda.Alikuwa akijifanya hasikii wanachosema na hapa anajaribu kuwasikiliza zaidi.hata hivyo Mbowe aliwaondoa wasiwasi na kusisitiza kuwa chama kinao utaratibu wa kushughulika na viongozi wanaokiuka maadili ya chama na kuwaomba wawaamini kama viongozi kuwa wanaouwezo wa kulishughulikia jambo hilo na mengine
 Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe akiwaaga wananchi waliokuwa wamefurika makao makuu ya chama kinondoni walikofika wakitokea jangwani usiku huu
 Sehemu ya umati uliowasindikiza viongozi wa chadema toka jangwani hadi kinondoni.wamesambaa yapata saa 2 usiku.
 Viongozi wa chadema wakifurahia kadi nyingi za CCM zilizorudishwa leo jioni kwenye mkutano
Sugu akimwaga mistari.
Reactions::

Stars vs Malawi Hakuna Mbabe

Mpira umekwisha kama wanavyoonekana katika picha wachezaji wa Taifa Stars wakitoka nje ya uwanja kwenda mapumziko, Si Taifa Stars wala Malawi ambayo imepata goli, hata hivyo wamalawi wameshambulia mara nyingi katika lango la Taifa Stars katika kipindi cha kwanza, lakini uimara wa mabeki pamoja na Golikipa Juma Kaseja umesaidia Wamalawi hao kutopata goli ,  Taifa Stars yenyewe imefanya mashambulizi ya hatari mawili tu! hata hivyo haikuwa bahati yao ambapo mpaka mwisho wa mchezo huo timu hizo zimetoka sare ya 0-0. 
Mchezaji wa timu ya taifa Taifa Stars Mbwana Samata ambaye anacheza mpira wa kulipwa katika timu ya TP Mazembe nchini DRC Congo akijaribu kumtoka beki wa malawi Foster Namwela wakati timu hizo zikimenyana kwenye uwanja wa Taifa jioni hii
 Wachezaji wa timu ya taifa Taifa Stars wakiingia uwanjani jioni hii kwa ajili ya kupasha mwili kabla ya mpambano wake wa kirafiki na timu ya taifa ya Malawi The Flames
 Wachezaji wa timu ya Malawi wakipasha mwili kabla ya kuingia uwanjani kukwaana na Taifa Stars jioni hii kwenye uwanja wa Taifa.
Wachezaji wa akiba wa timu ya Taifa Stars wakijifua kabla ya mpambano huo jioni hii.Timu ya Malawi iko safarini kuelekea nchini Uganda ambako itakipiga na timu ya Uganda Cranes.
Mpambano huo unafanyika kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam
 
(Picha zote na Full Shangwe)
Reactions::

Mikwaju Ya Penalti Haifai

Blatter amependekeza juhudi zifanywe kutafuta mbinu ya kukamilisha mechi iliyokwisha kwa sare baada ya dakika 120
Rais wa shirikisho la kimataifa la soka, FIFA, Sepp Blatter, amemtaka Franz Beckenbauer, ambaye anashikilia madaraka ya rais wa Bayern Munich kama wadhifa wa kumheshimu, kufikiria juu ya mbinu mpya za kukamilisha mechi iliyokwisha sare, badala ya "msiba" kupitia mikwaju ya penalti.
Beckenbauer ni mkuu wa kikundi kilichoteuliwa na FIFA na kukabidhiwa jukumu la mapendekezo ya kubadilisha au kutunga sheria ambazo zitatumika katika michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2014.
"Soka inaweza kugeuka ikawa ni msiba ikiwa itaingia katika mikwaju ya penalti", ameelezea Blatter.
"Kandanda haifai kuwa mchezo wa mmoja kwa mmoja. Kandanda inapoingia katika mikwaju ya penalti, basi inapoteza kivutio".
Aliongezea: "Pengine Franz Beckenbauer na kundi lake la mapendekezo ya 2014 anaweza kutueleza suluhu, pengine sio sasa, lakini siku zijazo."
Ushindi wa fainali ya ligi ya klabu bingwa barani Ulaya msimu huu iliamuliwa kwa mikwaju ya penalti, wakati Chelsea walipopata ushindi, ilhali ni Bayern Munich waliovuma katika mechi nzima.
Hii ilikuwa ni mara ya kumi kwa fainali ya Ulaya kuamuliwa kwa mikwaju ya penalti.
Kabla ya mikwaju ya penalti kuanza kutumika katika miaka ya sabini, mechi sare ziliamuliwa kwa kuchezwa upya, na nyingi zilikwisha kwa sare tena.
Baadhi ya mechi pia ziliamuliwa kwa kurusha sarafu juu, mfano ikiwa ni nusu-fainali ya Ulaya mwaka 1968, wakati Italia ilipoishinda Sovieti baada ya kurushwa sarafu.
Zambia pia ilishinda Kombe la Mataifa ya Afrika kupitia mikwaju ya penalti mwaka huu, kwa kuishinda Ivory Coast.
Mara mbili Kombe la Dunia pia limeamuliwa kwa penalti, wakati Brazil ilipoishinda Italia mwaka 1994, na Italia ikaishinda Ufaransa katika mashindano ya 2006.
Source:BBC
Reactions::

Mbowe Akihutubia

Mh.Freeman Mbowe mwenyekiti wa CHADEMA taifa akitoa hotuba yake yenye hamasa kubwa



Reactions::

Rais Kikwete Aongoza Kikao Cha Baraza La Mawaziri

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiongoza kikao cha baraza la Mawaziri mjini Dodoma leo mchana(picha na Freddy Maro)
Reactions::

Taswira Kutoka Jangwani





Reactions::

Rais Kikwete Apokea Ujumbe Maalum Kutoka Kwa Rais wa Angola

Mjumbe maalum wa Rais wa Angola Dr.Andre de Oliveira Sango akiwasilisha ujumbe maalum kwa Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete Ikulu ndogo mjini Dodoma leo asubuhi(picha na Freddy Maro)
Reactions::

Dk.Slaa Anaongea

Dk.Slaa akihutubia sasa,anaongelea mambo mbalimbali,mfumuko wa bei,posho,viwanda,ugumu wa maisha,zomeazomea ya CCM nk.
Deo Munish Katibu mkuu wa BAVICHA akiteta jambo na mmoja aliyehudhuria mkutano.


Reactions::