Subscribe:

Wednesday, February 22, 2012

Jenifer Mgendi Kufanya Maajabu 2012


Salaam nyingi ziwafikie wapendwa.
Naamini kwa neema ya Mungu mmeuona mwaka. Mimi pia, namshukuru Mungu.

Nachukua fursa hii kuwajulisha nilipo na ninapokwenda kwa mwaka huu na naomba kama kawa muwafikishie watanzania na wasomaji wenu kwa ujumla mambo haya. Natanguliza shukurani zangu za dhati.

DHAHABU
Hii ni albamu yenye mkusanyiko wa baadhi ya nyimbo zangu za zamani kama vile Nini?, Nimrudishie nini Bwana, Nitafika lini?, Mbona washangaa njiani. Ulinipa sauti na nyinginezo ambazo zilitamba miaka ya 2001 na kurudi nyuma hadi mwaka 1995. Albamu hii tayari ipo madukani katika mfumo wa audio cd yaani ni ya kusikiliza. Maandalizi ya video hii yanafanyika na panapo manajliwa mwezi Agosti itakuwa imekamilika.

TEKE LA MAMA
Filamu hii ipo maddukani na imewashirikisha watu mbalimbali kama Bahati Bukuku, Christina Matai, Senga, Lucy Komba na Godliver a.k.a Bibi Esta. Sio filamu ya kukosa kuangalia na uzuri wake unaweza kuiangalia ukiwa umetulia na familia yako bila kuwa na wasiwasi wa kuanza kuwatuma watoto dukani ili wasione picha chafu.

SHEREHE ZA MIAKA 15 YA HUDUMA
Panapo majaliwa na Mungu, natarajia kufanya tamasha la kusherehekea na kumshukuru Mungu kwa miaka 15 tangu nianze huduma ya uimbaji. Tamasha au sherehe hiyo inatarajiwa kufanyika tarehe 05 Agosti, 2012 katika ukumbi wa Landmark Hotel.Video ya album ya Dhahabu itazinduuliwa siku hiyo pia.
Maandalizi ya tamasha hili yanaendelea na litapambwa na waimbaji mbalimbali watakaoimba live siku hiyo. Sio siku ya kukosa na wote wenye mapenzi mema wanaombwa kujitokeza kwa wingi. Tutaendelea kuhabarishana kuhusu tukio hili kadiri siku zinavyoendelea.

ALBAM MPYA
Maandalizi ya album mpya yanaendelea moyoni lakini rasmi kabisa yataanza mara baada ya tamasha la mwezi wa Agosti na album hii mpya inatarajiwa kuingia sokoni mwezi Aprili mwaka 2013, tukijaliwa uzima.
Reactions::

JK Meets UK's Foreign Minister


President Jakaya Mrisho Kikwete chats with UK’s Secretary of State for Foreign and Commonwealth Affairs of the Mr William Hague and thebParliamentary Under Secretary responsible for Africa, United Nations, economic issues, conflict resolution, and climate change Mr Henry Bellingham after their talks at the Foreign office in London today February 22, 2012. The UK will host a conference on Somalia tomorrow February 23, 2012 with the view to pulling together international effort to help Somalia to its feet after 20 years of sliding backwards, despite the efforts of the African Union, the United Nations and the international community, international policy towards the country.


PHOTO BY STATE HOUSE
Reactions::

Kwaresma Njema

Waumini zaidi ya bilioni moja wa madhehebu ya katoliki na waothodox ulimwenguni kote pamoja na wakristo kwa ujumla leo wameanza mfungo wa kwaresma.siku arobaini za kujinyima na kujitesa kwa ajili ya maandalizi ya ufufuko wa Bwana Yesu.Hili ni jambo la imani na limedumu kwa zaidi ya milenia mbili sasa.Wakristo huombwa na Kanisa kufunga kabisa siku ya jumatano ya majivu ambayo ilikuwa leo.Kuna theolojia kubwa na ngumu juu ya tendo hili la imani.Kufunga chakula na kujinyima anasa na vitu tunavyovipenda ili kuungana na wenye shida wakati huu.Naam tunategemea kuona matendo mema wakati huu na kwamba yatakuwa mazoezi mema ya kiroho na yataendelea hata baada ya pasaka.
 Kuna kupakwa majivu katika paji la uso na maneno tubuni na kuiamini injili husemwa ambamo waumini hujibu amina wakikumbushwa juu ya umuhimu wa kumrudia Mungu na kwamba tumetoka katika mavumbi na tutarudi kuwa mavumbi.Rangi za Zambarau hutumika zikiwa na maana ya toba.Naam nasi Mjengwablog tunawatakia Kwaresma njema.
Reactions::

Tetesi :Polisi Waua Tena Songea





Kuna raia wanauawa tangu juzi na matukio yanaripotiwa ila askari hawachukui hatua yeyote ile zaidi wanasema ushahidi hawajauona,usiku wa kuamkia leo limekua tukia la 5 raia kuuliwa na askari kama kawaida yao hawatoi ulinzi kwa raia wao.

Asubuhi raia (Watoto, vijana, wazee) wakaamua kuwatolea uvivu askari na kuandamana hadi kituo cha polisi kudai haki ya kulindwa na kuishi raia walikua wengi kuliko uwezo wa askari wa kile kituo hivyo waliona hapa wakiwa wakali kituo kitachomwa moto maaana walikuja na jazba raia wakawaambia taarifa ziko kwa mkuu wa wilaya raia bila simile wakaanza maandamano hadi kwa mkuu wa wilaya kufika huko naye akanawa mikono kama pilato akasema mkuu wa mkoa ndo liko mikononi mwake.

Raia hawakuishia hapo wakalianzisha hadi kwa mkuu wa mkoa huku wakiimba "TUMECHOKA KUUWAWA" hadi kwa mkuu wa mkoa, hapo ndo movie ilpoanzia kumbe raia wakati wanaenda kwa mkuu wa mkoa inaaminika simu zilipigwa kwa mkuu wa mkoa na askari wanaolinda (FFU) wakafunga geti hapo ndo ikawa vuta nikuvute raia wakaweka kambi nje huku wanaimba nyimbo "MKUU WA MKOA UNAWAOGOPA RAIA WAKO JIUZURU", muda si mrefu gari ya FFU likawasiri likiwa na askari wa kutosha kwa vile raia hawakua na silaha wala ugomvi wakaamua kubaki huku wanaimba.

Askari kama kawaida yao wakawa wanazidi kusogelea huku wakitoa ishara wananchi watawanyike huku wananchi wakigoma hawatoki hadi mkuu wa mkoa naye atoke nje hapo ndo askari wakaanza kufyatua risasi za moto na raia wawili wakafa.habari zikafika mjini raia wameuliwa na askari hapo ndo mji ukazizima raia wakaingia mitaani askari waliokua mitaani walianza kupata upinzani mkali hd askari wawili wamekufa hadi hivi sasa, imebidi jeshi liingilie kati na mji wote kufungwa hivi ss mjini ni makundi ya wanajeshi na askari ndo yametawala hakuna maduka wala mabenki yanayofanya kazi
 Kutoka Mabadiliko
Reactions::

Maonyesho Ya Harusi



Wito kwa wadau wa sekta ya maswala ya Harusi.
Maonyesho ya biashara ya harusi sasa ni maonyesho makubwa ya harusi nchini yanayojumuisha wadau mbalimbali katika sekta ya harusi kutoka sehemu mbalimbali nchini Tanzania kwa kuonyesha bidhaa zao na huduma kwa umma kwa ujumla.
“Ndoa ni moja kati ya nyakati za muhimu katika maisha ya binaadamu na sherehe za harusi ni moja kati ya nyakati chache zinazoleta marafiki, familia na jamii kwa ujumla wote kuwa pamoja. Hivyo bila ya msaada kutoka kwa wadau wa sekta ya mambo ya harusi utambuzi wa kuwa na ndoto ya Harusi bora haiwi yakinifu. Najivunia katika kutimiza ndoto kugeuka katika ukweli ”. Alisema mwanzilishi wa Harusi Trade Fair Mustafa Hassanali.
Katika mwaka wake wa tatu sasa, Maonyesho ya Biashara ya Harusi yatakuwa na mambo makuu matatu ,ambayo ni maonyesho yenyewe, majadiliano na maonyesho ya mavazi. Maonyesho yote yatakusanya zaidi ya wafanyamaonyesho 50 ambao watakuwa wakionyesha bidhaa zao na huduma, kwenye Majadiliano kutakua na wageni kadhaa ambao watakua ni wasemaji katika uwanja wao wa utaalamu , na kuzungumzia mambo yonayohitajika na yasioitajika na mambo yote yanayohusu harusi, Maonyesho ya mwaka ya Harusi yatahusisha zaidi ya wabunifu kumi wa mitindo na wamiliki wa maduka ya bidhaa za Harusi ,ambapo bidhaa zao hizo zitaonyeshwa na kuuzwa katika maonyesho ya mavazi ya Harusi ambayo yatafanyika tarehe 31 Machi- 2012 kuanzia saa 2 Usiku nakuendelea.
“Mwaka jana tulikua na wageni zaidi ya 1500 ambao walihudhuria maonyesho haya, tunatarajia wageni zaidi mwaka huu . Kuvuna faida za matumizi na sehemu pana na masoko ya karibu zaidi, tunawaomba wachuuzi wote wa mambo ya harusi kuchukua fursa hii ya kila mwaka ya kuonyesha katika maonyesho haya ya kipekee ya harusi nchini "Alisema Meneja wa Masoko wa Harusi Trade Fair Hamis K Omary .
Hadi sasa zaidi ya washiriki 18 wa maonyesho ya Harusi tayari wamedhibitisha kushirki,miongni mwao ni EndePa event planners, Mkoma Bay lodge iliyopo Pangani, kearsleys travel, Binti Afrika, Wedding Bells, Rose fashion designs, Blind Tiger, MH Gallery, Dia’s , Green Chef na cocktails, GRM production, Pure Beauty , Lotus Creative concepts ,kwa kutaja chache tu.
Harusi Trade Fair 2012 itafanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee kwa siku 3 mfululizo kuanzia tarehe 30 marchi- 1 Aprili kuanzia saa 4:00 asubuhi nakuendelea.

“ Tukiwa tunamalengo makubwa sana ya kutangaza Harusi Trade Fair na kuitangaza Tanzania kama mahali pa Harusi na kama sehemu ya kupumzikia kwa maharusi duniani, ningependa kuwashukuru washirika wetu wote kwa kutuunga mkono kwa miaka yote iliyopita na kuendelea kuomba mashirika na kampuni mbalimbali kutuunga mkono kwa kudhamini Harusi Trade Fair 2012’’ . Almalizia Afisa Mahusiano, Amisa Juma
Harusi Trade Fair 2012 imedhaminiwa na Clouds Media group, Global Outdoor Systems. H.Models and 361 Degrees


Kwa Maelezo zaidi tembelea www.harusitradefair.com
Reactions::

Kumbukumbu Ya Mama


.....KUMBU KUMBU
Ni miaka 23 sasa tangu umetutoka lakini sisi kama watoto wako pamoja na baba ulietuacha huku tunaona ni kama jana tu umeondoka maana umeenda kimwili lakini kiroho bado tupo nawe, na kamwe hatutaacha kukumbuka malezi yako bora!
Tukiwa kama familia (watoto wako pamoja na mumeo (baba)) daima hatuishi kukuombea DUA njema kila kukicha upate kupumzika kwa kwa amani huko uliko.
Ni matumaini yetu mungu anasikia dua zetu MAMA
Ni sis wanao wapendwa Mariam, Hussein, Salum, Mariam Hawa pamoja na Baba yetu (mumeo) Sheikh Suleiman haatuna la zaidi ila ni dua tunakuombea
INNA LILLAHI WA INNA ILAIHI RAAJIUN.

Regards:-
Salum Suleiman Lyeme (Sule Junior)
Entertainment writter (Freelance), Graphic Designer (Freelance) / Mwananch Communication Ltd
C.E.O of SULE'S Inc. & ENTERTAINMENT
+255 719 694086
+255 689 566027
+255 767 007515
www.mtotowakitaa.blogspot.com
Reactions::

Dkt. Bilal Korogwe Sekondari Beach Nkasi

 Makamu wa Rais wa Jamhuri  ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akikata utepe kuzindua rasmi jengo la Daharia la Shule ya Sekondari ya wasichana ya Korongwe Beach , iliyopo Wilaya ya Nkasi, wakati akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Rukwa na Katavi, jana Februari 21, 2012. Kulia kwake ni mkewe Mama Asha Bilal.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipanda Mti wa kumbukumbu nje ya  jengo la Daharia la Shule ya Sekondari ya wasichana ya Korongwe Beach , iliyopo Wilaya ya Nkasi, baada ya kuzindua Daharia hilo wakati akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Rukwa na Katavi, jana Februari 21, 2012. Nyuma yake ni  mkewe Mama Asha Bilal na Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Eng. Stella Manyanya
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwasili kwenye Uwanja wa Korongwe kwa ajili ya kuwahutubia wananchi wakati akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Rukwa na Katavi jana Februari 21, 2012.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akinawa maji ya Kisima cha kupampu yanayovunwa kwa mvua, kilichojengwa katika Kijiji cha Mwamapuli wakati alipokuwa katika ziara yake ya mkoa wa Rukwa na Katavi juzi.
Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Mkazi wa Kijiji cha Mwamapuli, Yacoub Jilala, ambaye ni mlemavu, baada ya kumaliza kuwahutubia wananchi wa kijiji hicho, alipofika kuzindua jengo la Ghara la mazao, akiwa katika ziara yake ya mkoa wa Rukwa na Katavi, juzi Februari 20, 2012. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
Reactions::

Maulidi Kisiwa Cha Tumbatu

 Rais wa Zanzibar Dk, Ali Mohd Shein akisalimiana na Masheikh na waheshimiwa mbalimbali alipohudhuria katika Kisiwa cha Tumbatu  Zanzibar kwa ajili ya kuzindua Maulidi makubwa ya Kusherehekea kuzaliwa Mtume Muhammad (SAW).
 -Rais wa Zainzibar Dk Ali Mohd Shein watatu kutoka kushoto akiwa pamoja na Masheikh na Viongozi mbalimbali waliohudhuria Uzinduzi wa Maulid makubwa ya kusherekea kuzaliwa Mtume Muhammad (SAW)katika kisiwa cha Tumbatu Zanzibar.
 

 Sheikh Othman Maalim akitoa mawaidha katika Uzinduzi wa Maulid makubwa ya kusherekea kuzaliwa Mtume Muhammad (SAW)katika kisiwa cha Tumbatu Zanzibar.

Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohd Shein akiwahutubia Waislamu na wananchi mbalimbali waliohudhuria katika Msikiti mkuu wa Tumbatu Zanzibar  alipozinduwa Maulidi makubwa yanayofanyika kila mwaka kisiwani humo.
 
PICHA ZOTE NA YUSSUF SIMAI MAELEZO ZANZIBAR. 
Reactions::

Upendo Kilahiro Tamasha La Pasaka

Na Mwandishi Wetu
>
> MWIMBAJI nguli wa muziki wa Injili mwenye sauti nyororo,
> Upendo Kilahiro amekuwa wa kwanza kuthibitisha kushiriki
> katika tamasha la Pasaka litakalofanyika Sikukuu ya Pasaka
> Aprili 8 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
>
> Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya tamasha hilo, Alex
> Msama ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Msama
> Promotions, alisema Dar es Salaam kuwa Kilahiro
> amemthibitishia kwamba atashiriki tamasha hilo.
>
> "Kilahiro tutakuwa naye kwenye tamasha, na naamini kwamba
> mwaka huu tamasha hili litakuwa bora zaidi kutokana na
> kushirikisha waimbaji wengi wakali," alisema Msama.
>
> Kwa mujibu wa Msama, tamasha hilo la aina yake, baada ya
> kufanyika Dar es Salaam, pia litarindima kwenye Uwanja wa
> Jamhuri mjini Dodoma Aprili 9.
>
> Tamasha la mwaka huu malengo yake makubwa ni kuchangisha
> fedha kwa ajili ya kuwasomesha watoto yatima na kuwasaidia
> mitaji wanawake wajane.
>
> Tamasha la Pasaka la mwaka huu litashirikisha waimbaji wa
> nyimbo za Injili kutoka nchi kadhaa za Afrika ikiwa ni
> pamoja na Kenya, Uganda, Rwanda, Jamhuri ya Kidemokrasia ya
> Congo, Afrika Kusini na Zambia.
>
> Akizungumza Dar es Salaam, Kilahiro alisema amepania kufanya
> mambo makubwa katika tamasha la mwaka huu, na atapanda
> jukwaani kuimba 'live' na bendi yake ya Upendo Kilahiro.
>
> "Natoa mwito kwa mashabiki wangu wasiwe na wasiwasi,
> watarajie kupata vitu vizuri na tofauti zaidi... watapata
> vitu vinono kwa vile tamasha hili linazidi kuwa bora zaidi.
>
> "Sikukuu ya Pasaka ni upatanisho kutokana na kifo cha Yesu
> Kristo aliyefia msalabani na kufufuka siku ya tatu...
> tutaienzi sikukuu hiyo kwa nderemo," alisema Upendo.
>
> Mwanamuziki huyo anayeabudu katika Kanisa la BCIC lililoko
> Mbezi Beach, Dar es Salaam (Kwa Askofu Gamanywa), alisema
> amejiandaa vyema kukonga nyoyo za mashabiki wake na mbali na
> kufanya mazoezi, pia atafunga na kusali ili Mungu amfanyie
> miujiza.
>
> Aliwaomba mashabiki wamiminike kwa wingi Uwanja wa Taifa,
> Dar es Salaam Aprili 8 na Jamhuri Aprili 9, kuona mambo
> mazuri aliyowaandalia na kuongeza kuwa kwa vile anamtukuza
> Mungu aliyemtoa kwenye shida na majaribu mengi ya Shetani,
> anaamini atawapa kile wanachotaka kutoka kwakwe.
>
> Alisema anatarajia kuimba nyimbo mbalimbali zikiwemo
> zilizotamba za Zindonga (alioimba kwa Kizulu), Unajibu
> Maombi na Ni Salama Rohoni. Kilahiro hivi sasa anatamba na
albamu yake mpya ya Ficho Langu aliyoirekodi nchini Canada.

Reactions::

Msweden Afariki Ajalini Arusha


RAIA mmoja wa Sweden aliyefahamika kwa jina la Gunnar ORG Gunnarson (19) amefariki dunia baada ya gari alilokuwa akisafiria kugongana na gari lingine. Kamanda wa polisi mkoani hapa, Thobias Andengenye alisema kuwa, tukio hilo limetokea febuari 18 mwaka huu majira ya saa 7;20 katika barabara ya Arusha-Moshi eneo la Kikatiti wilayani Arumeru mkoania Arusha. Alisema kuwa, siku tukio gari aina ya Range Rover lenye namba za usajili T 663 AYB lililokuwa likiendeshwa na Lusingu Lubero Mvungi (38) mkazi wa jijini Dar es Saalamu likitokea Arusha kuelekea Kia liligongana na gari aina ya Land Rover Defender lenye namba za usajili T 424 AYD mali ya Arunga Expedition Arusha Tours. Ambapo gari hilio lilikuwa likiendeshwa na Francis Paul (45) mkazi wa Sanawari lililokuwa likitoea Moshi kuja Arusha na kusababisha kifo cha Msweeden huyo ambaye alifariki akiwa anapakiwa kwenye ndege tayari kwa kwenda Nairobi kwa matibabu. Andengenye alisema kuwa, ajali hiyo ilitokea baada ya gari aina ya Range Rover kujaribu kulipita gari liliokuwa mbele yake na kisha kupoteza uelekeo na kwenda moja kwa moja kugongana na gari aina la Land Rover Defender. Aidha mbali na ajali hiyo kusababisha kifo hicho,pia ilisababisha majeruhi klwa kwa watu kumi na moja ambao ni John Halid (60) raia wa Denmark,Bjorn Hoj Glaetesthl (28)raia wa Denmark, ambao wote kwa pamoja wamepelekwa Nairobi kwa matibabu. Aidha alitaja majeruhi wengine kuwa ni Francis Paul(45) mkazi wa Sanawari ambaye amelazwa katika hospitali ya Mount Meru , Clemence Nicolous (32) mkazi wa Sakina ambaye alitibiwa na kuruhusiwa, Elibariki Nicolous (32) mkazi wa Sakina ambaye ametibiwa na kuruhusiwa. Aidha wengine ni Godfrey David (21) mkazi wa Lekulei ambaye ametibiwa na kuruhusiwa, Haruna Amir (31) mkazi wa Elikulei ambaye alitibiwa na kuruhusiwa, Sajun Mollel (20) mkazi wa Mianzini, naye alitibiwa na kuruhusiwa , Paulo Omben(34) mkazi wa Sakina ambaye alilazwa katika hospitali ya Mount Meru. Aliwataja majeruhi wengine kuwa ni Ombeni Masawe (26) mkazi wa Mianzini,ambaye amelazwa katika hospitali ya Mount Meru,na Lusingu Lubero Mvungi (38) mkazi wa Dar es salaam ambaye alitibiwa na kuruhusiwa. Aidha kutokana na tukio hilo,jeshi nla polisi mkoania hapa linaendelea kumshikilia dereva wa gari aina ya Range Rover ,Lusingu Lubero Mvungi (38) mkazi wa jijini Dar es salaam na kwamba pindi upelelezi utakapokamilika atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili. Wakati huo huo jeshi hilo limefanikiwa kuwakamata watu wawili wajulikanao kwa jina la Linah Christopher( 50)na Elizabeth Christopher(40) wa maeneo ya ungalimited wakiwa na misokoto 314 ya madawa ya kulevya aina ya bangi Kamanda alieleza kuwa mafanikio hayo yalitokana na mafanikio ya taarifa zilizotolewa na raia mwema ambapo mara baada ya taarifa hiyo walikwenda moja kwa moja katika nyumba ya mtuhumiwa huyo na walipopekua walifanikiwa kupata bangi hiyo ikiwa imehifadhiwa katika mfuko wa plastiki Hata hivyo watuhumiwa hao walikiri kuwa walikuwa wamehifadhi bangi hiyo kwa ajili ya kuuza ambapo jeshi la polisi limeshawafikisha watuhumiwa hao mahakamani ili kujibu tuhuma ambazo zinawakabili..
Kutoka fullshangweblog
.
Reactions::

Pinda Naye Mtemi Usukumani

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Mkewe Tunu wakicheza ngoma ya Watemi wa Kisukuma baada kupewa heshima ya kuwa Mtemi Masanja na Mkewe kuwa Ngole kwenye uwanja wa michezo wa Maswa wakiwa katika ziara ya mkoa wa Shinyanga Februari 20, 2012. Kushoto ni Mtemi Majebele ambaye ndiye alimpa heshima hiyo. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Reactions::

TanzMED Toleo la tatu, Afya kwa wote.


www.tanzmed.com
1.

Kwanini tunahitaji mabadiriko

Ni mwaka sasa tangu tuzindue tovuti yetu ya toleo la pili ya TanzMED (TanzMED V1.2). Ili kukidhi matakwa ya wanajamii, hatuna budi kupanua wigo zaidi na kuongeza ubora. Katika maoni mengi ambayo tumekuwa tukipata wengi wa wanajamii wamekuwa wakiuliza ni jinsi gani wanaweza kuuliza maswali kwa madaktari kwa urahisi zaidi huku watumiaji wengine wakifaidika na majibu ya madaktari?

Kwenye toleo hili jipya tumetilia mkazo sana ushirikiano kati ya madaktari wa TanzMED na wasomaji wetu. Pia tunadhamiria kuongea majadiliano baina ya wasomaji wetu.

Jumuika na TanzMED...

Hautakiwi kuwa mwanajumuiya(member) au kutumia jina lako la ukweli ili kuuliza maswali, hivyo hakuna haja ya kuogopa kuuliza swali. Tunakuletea TanzMED majadiliano. Jadiliana na daktari wako moja kwa moja!

Jadiliana sasa...
Na mengi mno yameboreshwa;
Utumaji maoni umerahisishwa zaidi, pokea makala za afya kwa urahisi zaidi, email zenye vikoo vya TanzMED.com, pata makala mpya punde tu zinapotumwa, muonekano usiochosha macho, TanzMED Application kwa iPhone(inakuja)...

Yote haya yanaenda sambamba na spidi yenye kiwango
Reactions::

TFF Yawabana Wanachama Kurekebisha Katiba

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Februari 21, 2012

Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ilikutana Februari 15 mwaka huu jijini Dar es Salaam na kufanya uamuzi kwa ajenda mbalimbali ikiwemo Marekebisho ya Katiba za Wanachama wa TFF, na pia ushauri wa kisheria ulioombwa kwake na Kamati ya Uchaguzi ya TFF.

Uamuzi uliofanywa kwa wanachama wote 40 wa TFF ni ufuatao; wanachama wote wanatakiwa kufanya marekebisho kwenye katiba zao katika maeneo matatu kwa mujibu wa maelekezo ambayo TFF ilitoa mwaka jana.

Maeneo hayo ni sifa za wagombea uongozi ambapo kwenye kipengele cha elimu ni lazima iwe kuanzia kidato cha nne, kutopeleka masuala ya mpira wa miguu katika mahakama za kawaida na kamati zao za uchaguzi kufanya kazi chini ya Kamati ya Uchaguzi ya TFF.

Hivyo hakuna mwanachama yeyote wa TFF anayeruhusiwa kufanya uchaguzi kwa sasa kama katiba yake ina upungufu au inakwenda kinyume na maelekezo kuhusu maeneo hayo matatu.

Kamati imetoa hadi Juni Mosi mwaka huu kwa wanachama ambao katiba zao zina upungufu katika maeneo hayo wawe wamefanya marekebisho ndiyo waendelee na uchaguzi kwa wale ambao muda wa uchaguzi umefika.

Ushauri wa Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji kwa Kamati ya Uchaguzi ya TFF ni kuwa katiba zote za wanachama ziwe na vitu hivyo vitatu.


Alex Mgongolwa
Mwenyekiti
Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji
Reactions::

CCM Arumeru Waanza Kuvurugana (Gazeti Mwananchi)


Tuesday, 21 February 2012 20:52

Moses Mashalla, Mussa Juma, Arumeru
SIKU moja baada ya wanachama wa CCM, Jimbo la Arumeru Mashariki kumpendekeza Sioi Sumari kuwa mgombea wake katika uchaguzi mdogo ujao, baadhi ya wanachama wa Umoja wa Vijana (UVCCM) wilayani humo, wamepinga uteuzi huo wakidai kuwa uchaguzi uligubikwa na mizengwe.

Juzi, mkutano Mkuu wa Jimbo hilo ulimchagua Sioi, mtoto wa aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo, marehemu Jeremiah Sumari kwa kura 361 akifuatiwa na William Sarakikya aliyepata kura 259, Elishilia Kaaya (176), Elirehema Kaaya (205), Anthony Musari (22) na Moses Urio (11).

Lakini jana, baadhi ya wajumbe hao wa UVCCM wakiongozwa na Mjumbe wa Baraza la Umoja Mkoani wa Arusha, Kennedy Mpumilwa walidai kwamba uchaguzi huo ni batili kwa kuwa ulitawaliwa na misingi ya rushwa.

Mpumilwa alidai kwamba uchaguzi huo ulijaa rushwa kila kona. Hata hivyo, hakuweka bayana kama walihongwa ili wamchague nani kati ya wagombea hao sita.

Alidai kwamba kigogo mmoja wa UVCCM ngazi ya mkoa aliyeongozana na kada mmoja wa jumuiya hiyo, walikuwa ndani ya gari karibu na eneo la uchaguzi wakigawa rushwa kwa wajumbe.

“Huu uchaguzi haufai kabisa baadhi ya wajumbe walihongwa. Ilikuwa ikitolewa 150,000 kwa kila mjumbe atakayekubali. Sasa hii CCM gani kama uteuzi tu hadi ufuate rushwa,” alidai Mpumilwa.

Alisema kwa jinsi mchakato wa uchaguzi huo ulivyofanyika, ni dhahiri chama hicho kimeingia katika mpasuko mkubwa ambao kama usipoangaliwa kwa makini, unaweza kukiathiri.

Mpumilwa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Uchumi na Fedha wa UVCCM Wilaya ya Arumeru, alisema baadhi ya wanachama wa umoja huo wilayani humo wamechukizwa na mambo yaliyojitokeza katika uchaguzi huo huku wengine wakitishia kuhamia upinzani wakati wowote.

“Nakwambia vijana wamechukizwa kabisa na kilichofanyika katika mchakato wa uchaguzi, sasa wengine wametishia kwenda upinzani wakati wowote,” alieleza Mpumilwa.

Aliutaka uongozi wa CCM taifa kuingilia kati suala hilo na kulipa uzito akidai kwamba lisipoangaliwa huenda likazua mpasuko mkubwa ndani ya CCM wilayani humo na kusababisha kulipoteza jimbo hilo wakati wa uchaguzi.

Hata hivyo, Katibu wa Itikadi na Uenezi ya wa CCM Mkoa wa Arusha, Loota Sanare alisema hadi jana hakuna mgombea yoyote kati ya hao sita ambaye alikuwa amepinga matokeo ya uchaguzi huo.

Alisema ushindi wa Sumari katika uchaguzi wa ngazi ya jimbo, siyo mwisho wa uteuzi na kwamba kuna vikao vya kamati ya siasa ya Wilaya ya Arumeru na baadaye vikao vya mkoa na Kamati Kuu (CC) ya CCM Taifa, ambayo ndiyo itakayomtangaza mgombea.
“Tumezipokea hisia za wana-CCM, Sioi ameongoza ni nafasi nzuri kwake lakini siyo mwisho wa uteuzi wake. Bado kuna mchakato mrefu mbele yake,” alisema Sanare.


Vigogo watimua mbio

Katika hatua nyingine, kushindwa kwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (Nec) wa Mkoa wa Arusha, Elishilia Kaaya katika kura hizo za maoni juzi, kuliibua huzuni kubwa kwa vigogo wa chama hicho huku baadhi yao wakiondoka ukumbini kabla ya matokeo.

Kaaya ambaye pia ni Mkurugenzi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), alikuwa anaungwa mkono na kundi la viongozi wa juu wa CCM na Serikali ambao wamejipambanua kuwa wanapambana na vitendo vya ufisadi. Mjumbe huyo wa Nec alishika nafasi ya nne baada ya kupata kura 176, nyuma ya Sumari, Sarakikya na Elirehema Kaaya.

Dalili za kubwagwa kwa kigogo huyo, zilianza kuonekana mapema nje ya ukumbi ambako baadhi ya madiwani na wana-CCM vijana, walikuwa wakiendesha kampeni nzito ya kutaka mgombea kijana ambaye ataweza kupambana na mgombea machachari wa Chadema, Joshua Nasari endapo atapitishwa na chama chake.

Pia, katika ukumbi wa kupigia kura, mara baada ya wagombea wote sita kujieleza, Sumari alikuwa akishangiliwa zaidi na kundi la vijana hali ambayo iliwasukuma baadhi ya vigogo kuanza kuondoka mapema ukumbini.

Chadema wachekelea

Akizungumzia uchaguzi wa jana, Nasari alisema amefurahishwa na uamuzi CCM kumpitisha Sumari kugombea akidai kwamba sasa anaamini kuwa ushindi wa chama chake utajulikana saa nne asubuhi Aprili Mosi.Soma zaidi www.mwananchi.co.tz
Reactions::

Dk Slaa Hatarini Kutiwa Mbaroni


Tuesday, 21 February 2012 20:52

Peter Saramba, Arusha
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Arusha imemwagiza Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa na mchumba wake, Josephine Mushumbuzi na mwanachama mwingine wa chama hichi, Aquilinne Chuwa kufika mahakamani hapo leo vinginevyo itatoa hati ya kukamatwa.

Agizo hilo la Mahakama limekuja baada ya Dk Slaa na Mushumbuzi kushindwa kufika mahakamani hapo jana kusikiliza kesi inayowakabili pia viongozi wengine waandamizi wa chama hicho, akiwamo Mwenyekiti, Freeman Mbowe.

Mbowe na viongozi wenzake hao wa Chadema jana walisomewa mashtaka mapya 13. Akisoma mashtaka hayo Wakili wa Serikali, Edwin Kakolaki alimwambia Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, Charles Magessa kuwa ongezeko hilo limetokana na mashtaka mapya matano baada ya marekebisho ya hati ya awali iliyokuwa na mashtaka manane.

Washtakiwa wote walikuwepo mahakamani wakati hati hiyo mpya ikisomwa isipokuwa Dk Slaa, Mushumbusi na Chuwa.

Kukosekana kwa watuhumiwa hao kuliufanya upande wa mashtaka kuomba itolewe hati ya kuwakamata kwa kosa la kutofika mahakamani bila taarifa.

Hata hivyo, ombi hilo lilikataliwa na hakimu Magessa aliyeamua kutoa siku moja kwa washtakiwa hao kufika leo na iwapo hawataitikia wito huo hati hiyo itatolewa.

Uamuzi wa Hakimu Magessa ulitokana na taarifa na ombi la Wakili wa utetezi, Albert Msando aliyeitaarifu mahakama kuwa washtakiwa hao walijichanganya kuhusu tarehe ya shauri hilo wakidhani ni leo badala ya jana na kwamba muda huo walikuwa njiani wakitokea Dar es Salaam na kuomba mahakama isitoe hati ya kukamatwa, badala yake waamriwe kufika leo bila kukosa.

Akisoma hati hiyo mahakamani hapo mbele ya umati wa wasikilizaji, Wakili Kakolaki alisema washtakiwa hao wanakabiliwa na makosa mawili ya kufanya fujo, mawili kutoa matamko yenye lengo la uchochezi na kushawishi kufanya kosa.

Katika shtaka la kwanza, washtakiwa wote 19 wanadaiwa kula njama ya kutenda kosa la kufanya fujo kati ya Januari 3 na 5, mwaka jana wakiwa eneo na sehemu mbalimbali za Manispaa ya Arusha.

Shtaka la pili linalowakabili washtakiwa 18 la kula njama kutenda kosa na kukaidi amri halali pia linadaiwa kutendeka kati ya Januari 3 na 5, 2011 wakati katika shtaka la tatu wanadaiwa kula njama ya kufanya kusanyiko lisilo halali lililoishia kwa wote kutenda kosa la nne la kula njama za kufanya vurugu.

Dk Slaa na Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo wanakabiliwa na shtaka la tano ambalo ni kula njama kutenda kosa la kutoa matamshi yenye lengo la kuleta uchochezi huku kwenye shtaka la sita linalomjumuisha Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba washtakiwa hao watatu wanadaiwa kushawishi watu kutenda kosa.

Ndesamburo peke yake anakabiliwa na shtaka la kutoa matamshi ya uchochezi ambayo anadaiwa kuwa mnamo Januari 5, mwaka jana alitamka maneno yenye nia ya kuamsha chuki dhidi ya Serikali na Rais Jakaya Kikwete akidaiwa kusema kuwa kitendo cha polisi kuwafyatulia mabomu ya machozi na risasi za moto viongozi na wafuasia wa Chadema waliokuwa wakiandamana kwa amani ni sawa na Rais kutia saini kuruhusu machafuko nchini.

Viongozi wengine wanaokabiliwa na kesi hiyo ambao walikuwepo mahakamani jana wakati hati mpya ikisomwa ni pamoja na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema na Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini.Soma zaidi www.mwananchi.co.tz
Reactions::

Tuesday, February 21, 2012

PSPF Yatoa Msaada Shuleni Chalinze

 Kaimu MKurugenzi Ukaguzi wa Ndani wa Mfuko wa Pesheni wa Utumishi wa Umma PSPF. Bw. Godfrey Ngonyani (kushoto) akikabidhi msaada wa Madawati 60 yenye thamani ya milioni tatu walioutoa leo kwa Mjumbe wa Kamati ya Shule Msingi Bwilingu, Chalinze Mkoa wa Pwani, Bi. Jacklin Kitego kulia na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Bi. Anifa Kombo.(Picha na Mpigapicha Wetu)
 Baadhi ya Wanafunzi wa  Shule ya Msingi Bwilingu, Chalinze Mkoa wa Pwani wakigombania kukaa kwenye madawati mapya walioletewa na Mfuko wa Pesheni wa Utumishi wa Umma PSPF.(Picha na Mpigapicha Wetu)

Kaimu MKurugenzi Ukaguzi wa Ndani wa Mfuko wa Pesheni wa Utumishi wa Umma PSPF. Bw. Godfrey Ngonyani (kulia) akizungumza na Wazazi na Wanafunzi pamoja na Bodi ya Shule ya Msingi

Bwilingu, Chalinze Mkoa wa Pwani wakati walipokwenda kukabidhi msaada wa Madawati 60 yenye thamani ya milioni tatu kushoto Mwenyekiti wa Kamati ya Shule, Bi. Anifa Kombo na Mjumbe wa Bodi ya PSPF Bw. Ramadhani Maneno.(Picha na Mpigapicha Wetu)
Reactions::

MeTL Yapania Kuwekeza Zaidi Zao La Mkonge




* Nusu ya mapato ya Serikali hutokana na zao hilo, imeweka bil 50/-
* Husaidia kuunda magari, ndege, ujenzi wa nyumba, karatasi, noti
* Imewekeza ekari 35,000 Tanga, Kilimanjaro, Pwani, Morogoro
* Bidhaa huuzwa soko la Mashariki ya Kati, Nigeria, Ulaya, India

Na Mwandishi Wetu


UTAJIRI wa nchi zilizoendelea duniani (G8) umefikiwa kwa kuzingatia uongozi wa nchi hizo kuwekeza kwenye viwanda, na asilimia 90 ya uwekezaji huo hutegemea uzalishaji wa bidhaa zitokanazo na mazao.


Ni asilimia 10 tu ya uzalishaji wa bidhaa katika viwanda hutegemea vitendea kazi ikiwemo mashine za aina zote na vyombo vya usafiri.


Kwa kutambua kuwa viwanda ndiyo chanzo cha ukuzaji uchumi wa nchi, msisitizo kwa viongozi wa ngazi za juu serikalini huelekezwa kwenye kilimo ambapo mkulima atakapozalisha mazao yawe ya chakula aweze kujikimu kwa chakula, lakini pia awe na ziada ambayo ataiuza kwa lengo la kujiongezea kipato.


Yapo mazao ya chakula na ya biashara, na mazao ya biashara hutegemewa kukuza pato la mkulima kwa asilimia kubwa kuliko ilivyo kwa wakulima wa mazao ya chakula. Pia kilimo cha mazao hayo hukuza pato la nchi kwa kuzingatia biashara za kimataifa.


Nchini Tanzania yapo mazao mengi ya biashara, na miongoni mwa hayo ni pamoja na buni, chai, korosho, tumbaku na mkonge.


Wakati baadhi ya wananchi kutokana na hali ya jiografia ya maeneo yao hulazimika kulima aina hiyo ya mazao, baadhi hulima mazao ya chakula ambayo ni mahindi, maharagwe, mchele, viazi, ndizi na mihogo.


Katika makala haya, kubwa linalobainishwa ni jinsi kilimo cha mkonge kilivyotoa ajira kubwa kwa vijana tofauti na ilivyo kwenye uwekezaji wa aina nyingine ya mazao, lakini ukweli wa hilo hauko wazi kwa wengi.


Sifa nyingi zinazobebwa na kilimo cha zao la mkonge ni pamoja na uchumi wa nchi ambapo nusu ya mapato ya Serikali hutokana na zao hilo, lakini pia robo tatu ya ukubwa wa kilimo ni wa zao la mkonge.


Asilimia 80 ya Watanzania wameajiriwa katika kilimo, hivyo kufanikisha sera ya Kilimo Kwanza na mfano wa wazi ni Kampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Limited (MeTL).


Kampuni hiyo imechangia kwa kiasi kikubwa katika sekta ya kilimo na kuinua kiwango cha uchumi na maendeleo ya nchi kwa ujumla.


Mwaka 1997, kampuni hiyo iliwekeza ekari 35,000 za mkonge katika mashamba kadhaa mkoani Tanga, Kilimanjaro, Pwani na Morogoro na imeweza kufanikisha biashara ya zao hili.


Kwa uwekezaji huo, zaidi ya wafanyakazi 300 wameajiriwa kwenye mashamba ya mkonge kwa ajili ya kushughulikia zao hilo, idadi ambayo ni kubwa kwa sekta binafsi katika utoaji ajira kwa Watanzania.


Miundombinu kama nyumba za wafanyakazi, kambi za wafanyakazi, matumizi ya barabara, huduma za shule na zahanati vimeanzishwa katika mashamba yote.


Akizungumza na mwandishi wa makala haya, Mkurugenzi Mkuu wa MeTL, Mohamed Dewji maarufu kama Mo, anasema kuwa vitu vingine kama magari na vifaa vya kilimo vimewekwa katika kila shamba, hivyo kampuni imewekeza sh. bilioni 50 katika kilimo hicho.


"Mkonge ni zao pekee ambalo halihitaji maji na linaloweza kuvunwa wakati wowote. Halina mipaka ya ukame... hili ndilo la kulipa kipaumbele kwani litawainua wakulima," anasema Dewji ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mjini (CCM).


"Shughuli za maendeleo ya kilimo zimetoa ajira kwa zaidi ya watu 5,000 wakati wa msimu wa kilimo na tumetoa mbinu za kilimo kupitia kwa wataalamu wetu hivyo kuboresha ufahamu wa wafanyakazi wetu," anasema Mkuu wa Kitengo cha Kilimo wa MeTL, Mamik.


Katika mikoa hiyo, MeTL huzalisha tani 6,000 za mkonge kila mwaka na wanazo ekari 10,000 za mashamba hayo ambapo dhamira kuu ni kulima kati ya tani 10,00 na 15,000 ili kufanikisha kupatikana soko la nje pia.


Mifuko iliyotengenezwa kwa mkonge (magunia) ni bidhaa iliyo bora, inasaidia kuhifadhi vizuri bidhaa zinawekwa ndani yake.


Katika jitihada za kuisadia Serikali, wamesaidia kuinua soko la mkonge kwa kuongeza uzalisahaji kutoka zamu moja ya wafanyakazi hadi tatu kwa siku na kuajiri watu 7,000.


Zao hili linatumika pia kutengenezea kamba katika kiwanda cha 21st Century Holdings Ltd kilichopo Dar es Salaam ambacho kilianzishwa mwaka 2001 ili kuipa nguvu kampuni katika kuendeleza zao la mkonge.


Kiwanda kinazalisha bidhaa mbalimbali zikiwemo kamba, mazulia, magunia na brashi ambapo pia wamekuwa wakiuza katika soko la Mashariki ya Kati, Nigeria, Ulaya na India.


Kitengo cha kilimo cha kampuni hiyo kinalenga kuchangia uchumi wa pato la taifa kupitia kilimo kwa kusisitiza sera ya Kilimo Kwanza ambayo imeanzishwa kwa nia ya kuleta mabadiliko ya kilimo kwa wakulima na taifa lao.


Ni wakati muafaka wa wawekezaji kuona kwa jicho la pembeni mambo ambayo yanaweza kuleta mapinduzi ya maendeleo kupitia kilimo kama walivyotangulia kufanya baadhi ya wawekezaji hususan kwenye eneo la kilimo cha mazao ya chakula, lakini pia bila kusahau kilimo cha mazao ya biashara.


Mkonge unavyotajirisha


Mamik anasema kupanda hadi kuvuna mkonge kwa mara ya kwanza huchukua miaka mitatu, lakini katika kipindi hicho, mkulima anaendelea kufaidi mavuno kutokana na mazao mengine kama mahindi na maharagwe ambayo hupandwa sambamba na mkonge.


"Kwa maana hiyo, mkulima anaanza kupata mavuno tangu mwaka wa kwanza anapoanza kulima na anaendelea hivyo kwa miaka mitatu. Baada ya hapo mazao mengine hayawezi tena kuendelea kustawi lakini kuanzia hapo anaanza kuvuna mkonge hivyo kumudu kununua mazao hayo mengine ya chakula."


Kuhusu mapato yanayotokana na mavuno kwa hekta moja, mkuu huyo wa kitengo anasema mkulima anaweza kupata wastani wa sh. 600,000 kwa mwaka, hiyo ikiwa ni baada ya kutoa gharama zote za uendeshaji.


Anafafanua kwamba zao la mkonge ni lile lisilo na msimu maalumu wa kupandwa wala ule w kuvunwa na hatua hizo zikifikia pia hufanyika bila shida wakati katika soko la dunia kukiwa na uhakika wa mauzo yenye tija kwa wakulima.


Vilevile mahitaji ya kutumia mkonge yanaendelea kuongezeka katika suala la uzalishaji bidhaa kama vifaa vya ujenzi, vifaa vya magari, chakula cha mifugo, mbolea na uzalishaji wa nishati huku bei ya mkonge ikiwa imefikia dola 1000 kwa singa za daraja UG.


Matumizi ya mkonge


Mamik anayataja matumizi ya zao hilo ambayo wengi wetu tunayajua. Haya ni pamoja na kutengenezea kamba, mazulia na magunia. Lakini anakwenda mbali na kutaja mengine ambayo wengi hawayajui. Haya ni pamoja na kusaidia katika uundaji wa magari na ndege, ujenzi wa nyumba, karatasi (noti na vifuko vya majani ya chai).


Lakini mbali ya matumizi hayo, mkonge unatumika pia katika kuzalisha umeme, kutengeneza nishati mbadala ya ethanol, mbolea na chakula cha mifugo.
Reactions::

Amina Mrisho Aula Sensa


TAARIFA KWA VYOMBO
VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Bibi Amina Saidi Mrisho kuwa Kamishna wa Sensa ya Mwaka 2012.Aidha, Rais Kikwete amemteua Bibi Seraphia R.Mgembe kuwa Mratibu wa Mpango wa Kurasimisha Raslimali na Biashara za Wanyonge Tanzania
(MKURABITA).Taarifa iliyotolewa na kutiwa saini Dar es Salaam leo, Jumanne, Februari 21, 2012, na Kaimu Katibu Kiongozi, Bwana Peniel Lyimo imesema kuwa uteuzi huo umeanza jana, Februari 20, mwaka huu, 2012.
Taarifa ya Bwana Lyimo imesema kuwa kabla ya uteuzi wake, Bibi Amina Mrisho alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani.Katika taarifa tofauti iliyotolewa na kutiwa saini pia mjini Dar es Salaam leo, Jumanne,
Februari 21, 2012, na Katibu Mkuu Ikulu, Bwana Peter Ilomo, imesema kuwa uteuzi huo wa Bibi Mgembe umeanza pia jana, Jumatatu, Februari 20, 2012.

Bwana Ilomo amesema katika taarifa yake kuwa kabla ya uteuzi wake Bibi Mgembe alikuwa Mkurugenzi wa Utawala na Fedha wa MKURABITA. Bibi Mgembe anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bwana Ladislaus Salema ambaye amestaafu kwa mujibu wa sheria.

Imetolewa na: Kurugenzi ya Mawasiliano
ya Rais, Ikulu.
Dar es Salaam.
21 Februari, 2012
Reactions::

NHIF Wasaidia Wajawazito Tanga

 Mkuu wa Mkoa wa Tanga Chiku Galawa akiteta jambo na Mkurugenzi Mkuu wa NHIF bwn. Imanuel Humba, kushoto ni Mwakilishi wa kfw,
Dk Kai Gesing kabla ya uzinduzi wa mradi huo, ambao huko chini ya usimamizi wa NHIF kwa Mikoa ya Tanga na Mbeya kwa majaribio.
 Mkuu wa Mkoa wa Tanga Chiku Galawa akikata utepe kuashiria uzinduzi wa mradi  wa kuwasaidia kupata huduma bora kwa hakina mama wajawazito  na watoto walio chini ya umri wa miaka 5,hususani maeneo ya vijijini.
 .Pichani mmoja wa wanufaika wa mradi KfW akipokea kitambulisho cha kupata huduma za afya kwa niaba ya wenzake 600 kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga Bi Chiku Galawa,wanaoshuhudia pemben kulia ni Mkurugenzi mkuu wa NHIF bwn Imanuel Humba na Dr. Sweya ambaye ni meneja wa Mradi kutoka NHIF.
 Naibu Mkurugenzi Mkuu bwn. Hamis Mdee akiteta jambo na Mkurugenzi Mkuu kuhusu namna ambavyo mradi huo unavyotekelezeka kwa kasi Mkoani Tanga kabla ya kuanza kwa mkutano wa uzinduzi.
akina mama wajawazito waliowawakilisha wenzao 600 wakati wa kupokea vitambulisho vya huduma za afya wakiwa kwenye picha ya pamoja na wafadhili wa mradi (kfW)  na NHIF.
Na Grace Michael 
Reactions::

Leo Mama Wa Makamanda Wangu Asingenielewa Kama...




Ningeweka kambi Msamvu kwa Bi Mkora. Naam, wa ubani wangu leo kaniandalia mlo maridhawa hivi baada ya kutoka safari ndefu ya Dar. Viazi vya kusaga kwa jibini. Samaki wa maji chumvi aliyeokwa na viungo kama pilipili manga. Kisha kakamuliwa ndimu. Na pilipili shamba juu.Ndio raha hiyo ya kuwa na mwandani wako.  Ama hakika, mwenda tezi na homo hurejea ngamani!

Reactions::

WATEJA 700 WA MPESA WAJAZWA VITITA VYA FEDHA


• Ni kupitia promosheni ya tuma fedha kwa MPESA na ushinde
• 35 Milioni zaenda kwa wateja katika wiki ya kwanza

Wateja 700 wa Vodacom MPESA wamejishindia kiasi cha shilingi 35 Milioni katika wiki ya kwanza ya
promosheni ya tuma fedha kwa MPESA na ushinde ilyozinduliwa wiki iliyopita ambapo jumla ya Shilingi 480
milioni kushindaniwa.

Washindi hao ambao kila mmoja amejishindia kiasi cha shilingi 50,000 katika droo za kila siku. Mbali na
droo ya kila siku promosheni hiyo itachezesha droo moja kubwa kw akila mwezi kwa kipindi cha miezi
mitatu zitakazotoa washindi wa Shilingi 10 Milioni kila mmoja.

“Hadi kufikia leo promosheni hii imeshatoa washindi mia saba, haya ni matokeo ya mwitikio mzuri wa wateja
wetu kushiriki na hii inatupa faraja kwetumkwa kuwa lengo la Vodacom ni kuwafanya wateja wetu kuwa na
furaha watumiapo huduma yetu ya MPESA na kuwawezesha.” Alisema Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom
Bw. Rene Meza

Kupitia droo hiyo washindi mia moja hujishindia shilingi 50,000 kila mmoja ambazo mshindi huingiziwa moja
kwa moja katika akunti yake ya MPESA.
.
Mwamavita amesema huduma ya MPESA imekuwa sehemu muhimu katika maisha ya wananchi ambayo
imerahisha na kubadili maisha yao tangu ilipoanzishwa Aprili, 2008, na hii inaenda sambamba na azma ya
Vodacom ya kuthamini mchango wa wateja wake kuunga mkono huduma hiyo kwa kuwawezesha na pia
kuifanya kuzidi kuwa huduma bora,salama,ya uhakika na rahisi..
“Ni msimu mwengine ambapo tunatoa nafasi kwa wateja wetu kufurahia huduma bora,rahisi,salama na
ya kuaminika ya Vodacom MPESA kwa gharama nafuu zaidi sokoni kutoka kampuni inayoongoza soko la
huduma za simu za mkononi nchini. Alisema Bw. Rene katika taarifa yake kwa vyombo vya habari..
“Matumizi ya huduma ya Vodacom MPESA yamekuwa yakiongezeka kwa kasi sana, na hii inatufanya
wakati wote kuongeza kasi ya kuifanya huduma ya MPESA kuendelea kuwa huduma bora zaidi sokoni na
yenye tija kwa wateja wetu inayotoa huduma za kibenki kupitia simu ya mkononi. Kadri mteja anavyotuma
pesa kwenda kwa mteja wa MPESA aliyesajiliwa au ambae hakusajiliwa ndivyo anavyojiweka katika nafasi
ya juu ya kushinda zawadi katika promosheni hii”Aliongeza Bw. Rene

Huduma ya Vodacom MPESA ina mtandao wa mawakala zaidi ya elfu kumi na tano nchi nzima na wateja
zaidi ya milioni nane kati yao zaidi ya milioni mbili wakifanya miamala – kutuma na kupokea fedha kwa
kipindi cha mwezi mzima mfululizo.

Kupitia huduma ya MPESA mteja wa Vodacom aliyejisajili na huduma hiyo anaweza kufanya manunuzi

About Vodacom
Vodacom Tanzania Limited is Tanzania’s leading cellular network offering state-of-the-art GSM communication services to
more than 9 million customers across the country. Vodacom Tanzania is a subsidiary company of Vodacom Group (Pty)
Limited, South Africa.

Vodacom Tanzania has deployed state of the art technology, thereby enhancing its product portfolio and positioning
itself as the market leader for any communication solution. For voice, data, leased lines, PABX connectivity, international
connectivity, WiMAX solutions, remote communication solutions over satellite or banking solutions, Vodacom Tanzania
addresses the need.

ama kulipia huduma mbalimbali za ikiwemo umeme – LUKU, DAWASCO,DSTV,Muda wa maongezi,
kuchangia michango ya harusi,kusaidia misiba, ada, n.k ndani ya nchi na hata kutokea nje ya nchi.

Mbali na promosheni hii wateja wa MPESA kwa sasa wanafurahia pia ofa mbalimbali ikiwemo ya punguzo
la asilimia 75 katika gharama za kutuma fedha kwa MPESA mabapo sas amteja anatuma fedha kwa
kiwango cha chini kabisa cha shilingi 50 kuanzia shilingi 500 hadi elfu kumi, nyongeza ya bonasi ya asilimia
25 mteja anaponunua muda wa maongezi wa hewani kupitia MPESA.
Reactions::

SUGU NA RUGE WAPATANISHWA

Waziri wa habari Nchimbi, Joseph Mbilinyi , Ruge Mutahaba, na Tundu Lissu wakiwa pamoja baada ya kupatanishwa , na kumaliza ugomvi wa muda mrefu.

MJENGWA BLOG INAWAPA PONGEZI 
KWA UKOMAVU WALIO ONYESHA VIJANA HAWA  WAPIGANAJI.
Reactions::

BABU ROBERT BADO NGANGARI

HAPPY BIRTHDAY MR ROBERT MUGABE
 
Akitimiza miaka 88 leo Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe aliyetawala toka uhuru wa nchi nchi hiyo1980,  leo amesema bado ataendelea kugombea uraisi wa nchi hiyo mpaka pale atakaposema mwenyewe imetosha.............

Reactions::

Nimerudi Iringa, Msamvu Hata Mwendo Sikupunguza!

 Ndugu zangu,
Nimerudi nyumbani Iringa jioni hii nikitokea Dar. Msamvu nimepita bila hata kupunguza mwendo. Kuepuka maneno ! Nimeanza pia kufikiria kuweka kituo Goma, Mvomero. Niwe napumzika hapo. Tuung'oe mzizi wa fitna za Msamvu. Nitakachokikosa ni chakula cha Bi Mkora tu!
Vinginevyo, Iringa ni shwari. Kuna dalili za mvua. Huko njiani nimeona mazao yakiwa yamenyauka kwa jua katika maeneo mengi. Kuna tishio la njaa mwaka huu.
Maggid, 
Iringa.
Reactions::

Ubunifu Huu

Kutoka Global publishersblog
Reactions::