1 week ago
0
362
Kuna watembeleaji 169 wapo online
Je una swali au tatizo lolote unatafuta majibu?







Chanzo: millardayo.com

Wabunge wanne wa Chadema, ambao waliachiwa na polisi kwa dhamana wamesimulia mateso waliyoyapata wakiwa rumande baada ya kukamatwa juzi.
Vigogo hao; Mbunge wa Mpanda Mjini Said Amour Arfi, Tundu Lissu (Singida Mashariki), Mustapha Akunaay (Mbulu) na Joyce Mukya (Viti maalumu), walikamatwa juzi baada ya wao na wafuasi wa chama hicho kutawanywa kwa mabomu ya machozi na polisi kwenye Viwanja vya Soweto, Arusha.
Wabunge hao waliachiwa baada ya kujidhamini wenyewe huku watu wengine 65 waliokamatwa pamoja nao wakiachiwa baada ya kudhaminiwa.
Wote wanatakiwa kuripoti kwenye kituo hicho Julai 22, mwaka huu na wataelezwa hatma ya suala hilo.

Neyman akishangilia baada ya kufunga bao

Wachezaji wa Brazil wakishangilia
Pichani ni baadhi ya wazazi wa wanafunzio waliopo na watarajiwa.

Ndugu zangu,
Huu si wakati wa kutafuta mshindi, maana, hapa tulipofikia sote tumeshashindwa. Ni wakati wa kutanguliza hekima na busara za hali ya juu. Na maamuzi mengine tunayotakiwa kuyafanya sasa yasitokane na mazoea ya siku za nyuma, bali, uzoefu mpya tunaoupata sasa.
Maggid Mjengwa,
Iringa.
Olle anajua kuwa baba yake ni mpenzi wa Man United, hivyo anacho cha kulinganisha kwa kusema..
-Kwamba Man United mwaka huu imetimiza mataji 20 ya ubingwa. Na mimi na mke wangu mpendwa leo tumetimiza miaka 20 ya ndoa yetu!
- Kwamba Man United hawachoshwi na ushindi. Na mimi na mke wangu hatuchoshwi na mapenzi!
Na Olle pia anaijua diplomasia kidogo, maana, hakumgusia kabisa kocha Alex Ferguson...!
Pichani nilipokuwa Zanzibar, 1988. Ilikuwa ni safari yangu ya kwanza kuvuka bahari ya Hindi.
Usiku Mwema.
Maggid,
Iringa.
Washukiwa wa kundi la wapiganaji wa kiisilamu nchini Nigeria, wamewaua wanafunzi tisa , katika shambulizi la pili ambalo limewalenga wanafunzi katika siku za hivi karibuni.
Washambuliaji wanaoaminika kuwa wanachama wa kundi la wapiganaji wa Boko Haram, waliwashambulia kwa risasi wanafunzi hao waliokuwa wamevalia sare za shule katika shule moja viungani mwa mji wa Maiduguri.
Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir, amewafuta kazi mawaziri wawili serikalini wanaohusishwa na sakata kubwa na mamilioni ya dola .
Bwana Kiir pia amewaondolea kinga dhidi yao wakiwa waziri wa fedha Kosti Manibe na mwenzake anayehusika na maswala ya baraza la mawaziri Deng Alor kushtakiwa na kuamuru kuanzishwa kwa uchunguzi dhidi yao
Na John Banda, Dodoma
JUMLA ya watu 19 wamepoteza maisha kati ya Januari na June mwaka huu kutokana na ajali zilizosababishwa na uzembe wa madereva wanaondesha Bodaboda.
Hayo yamesemwa na kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma David Misime alipokuwa akifungua mkutano kati ya jeshi hilo na waendesha Bodaboda uliofanyika katika Bwalo la Polisi kwa lengo la kutatua changamoto ya Ajali za mara kwa mara.
Kamanda Misime alisema katika kipindi hicho jumla ya ajali 48 sawa na asilimia 18.7, zilitokea na kati ya ajali hizo 17 zikiua watu 19 na nyingine 31 zikisababisha majuruhi 47 walioachwa na ulemavu wa kudumu, huku ajali 42 zikiwa zimesababishwa na Waendesha Bodaboda boda.

Mjumbe maalum wa Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika (SRCC) nchini Somalia, Balozi Mahamat Saleh Annadif ameshutumu vikali shambulio la kigaidi lililofanywa leo na magaidi wa Al-Shabaab katika makao ya Umoja wa Mataifa mjini Mogadishu.
"Tunalaani vikali shambulio hili la kinyama katika makao ya Umoja wa Mataifa mjini Mogadishu. Mashambulio haya yasiyofanikiwa yanayoendeshwa na Al-Shabaab yanalenga tu kuvuruga jitihada zinazochukuliwa na wananchi wa Somalia baada ya vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyodumu kwa zaidi ya ishirini na magaidi hao..

Marekani imetangaza kwamba itaanza majadiliano na kundi la Taliban baadaye wiki hii katika juhudi za kubuni mpango wa kumaliza zaidi ya muongo mmoja wa vita nchini Afghanistan.
Maafisa wa Marekani wanasema mazungumzo yataanza Alhamisi mjini Doha, mji mkuu wa Qatar. Maafisa wa yeo vya juu wa wizara ya mambo ya nchi za nje na White House wanatazamiwa kukutana na ujumbe wa Taliban katika kile kinachoelezwa ni mazungumzo ya awali.
Pichani ni makamanda wangu, mke wangu mpenzi na mimi.
Mlimani City, Aprili, 2012.
Maggid,
Iringa.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Mabalozi wateule wa Tanzania, wanaokwenda kuripoti kwenye Vituo vyao vya kazi nje ya nchi, wakati mabalozi hao walipofika Ofisini kwa Makamu Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Juni 19, 2013 kwa ajili ya kumuaga mhe. Makamu. Kutoka Kushoto ni Balozi Modest Mero, anayekwenda Umoja wa Mataifa, Geneva, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk, anayekwenda, Abu Dhabi UAE, Balozi Chabaka Kilumanga, anayekwenda Comoro, Balozi Wilson Masilingi, anayekwenda The Hague, Uholanzi na Balozi Liberata Mulamula, anayekwenda Washington D.C, Marekani. Picha na OMR

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi wateule wa Tanzania, wanaokwenda kuripoti kwenye Vituo vyao vya kazi nje ya nchi, wakati mabalozi hao walipofika Ofisini kwa Makamu Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Juni 19, 2013 kwa ajili ya kumuaga mhe. Makamu. Kutoka Kushoto ni Balozi Chabaka Kilumanga, anayekwenda Comoro, Balozi Mbarouk Nassoro Mbarouk, anayekwenda, Abu Dhabi UAE, Balozi Modest Mero, anayekwenda Umoja wa Mataifa, Geneva (kulia) ni Balozi Wilson Masilingi, anayekwenda The Hague, Uholanzi na Balozi Liberata Mulamula, anayekwenda Washington D.C, Marekani. Picha na OMR

Ujenzi wa bwawa la kufua umeme, nchini Ethiopia
Ethiopia na Misri wamekubaliana kufanya mazungumzo ya ziada juu ya athari za bwawa kubwa ambalo Ethiopia inalijenga kwenye mto Nile.
Wiki iliyopita Rais wa Misri, Mohammed Morsi alisema hataki vita lakini ataweka mapendekezo yote wazi yanayohusu majibu ya nchi yake kwa mradi wa bwawa hilo ambalo Misri inawasi wasi utapunguza sana kiwango cha usambasaji wake wa maji.

MSAJILI wa Vyama Vya Siasa nchini John Tendwa amesema ili kuhakikisha kuwa amani inaendelea kudumu ni muhimu kuwepo kwa uvumilivu na kuhueshimiana kati ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Taliban

Naibu waziri wa mambo ya nje wa Qatari Ali bin Fahd al-Hajri na Jan Mohammad Madani, mmoja wa maafisa wa Taliban akikata utepe katika ufunguzi rasmi wa ofisi y aTaliban huko Doha, Qatar.


Klabu ya Thai Port Football ya Thailand inatafuta wachezaji nchini Tanzania kwa ajili ya kucheza mpira wa miguu nchini humo na katika nchi nyingine barani Ulaya.
Kupitia kwa wakala wake, klabu hiyo imetuma taarifa kupitia Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ikitaka wachezaji wenye umri kuanzia miaka 15 hadi 28 kwa ajili ya kuwafanyia majaribio ambapo watakaofuzu watacheza nchini humo na katika klabu nyingine za Ulaya ambazo wana ushirikiano nazo.
Wachezaji wenye nia ya kufanya majaribio wanatakiwa kutuma taarifa za wasifu wao (CV) kwa klabu hiyo kwa njia ya emaili, wawe na pasi ya kusafiria pamoja na pasi ya mchezaji (player passport).

Saida Kalori ameongea na millardayo.com akiwa wilaya ya Mbeya na kusema amekua akipigiwa simu nyingi sana watu wakitaka kujua kama kafariki kweli, amekua akiambiwa taarifa mbalimbali kuhusu kifo chake… wengine wanasema kapata ajali ya boti iliyozama, wengine kapata ajali ya gari lakini ukweli ni kwamba hakuna lolote lililomtokea, ni mzima wa Afya.
(Millardayo-Saida) "Nimepigiwa simu zaidi ya 250 kutoka kwa watu mbalimbali kati ya saa 12 jioni na 9 usiku mpaka simu ikazima"Chanzo: millardayo.com
Rais wa TFF, Leodger Tenga
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linawashukuru washabiki kwa kujitokeza kwa wingi kwenye mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia kati ya Taifa Stars na Ivory Coast (The Elephants) iliyochezwa juzi (Jumapili) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Hispania U-21 wakishangilia ubingwa baada ya kuibamiza Italia 4-2

Hispania wakishangilia
1 week ago
0
362
1 week ago
1
420
1 week ago
2
537
2 weeks ago
1
643
2 weeks ago
1
644


Kwa video za matukio mbalimbali yanoyotokea Tanzania.
Ziara ya Rais Obama yazidi kuwatia kiwewe wasomi
MABOMU YA MACHOZI YARINDIMA Arusha
meza ya magazeti leo jumamosi